Wahamiaji haramu 49 kutoka Ethiopia wakamatwa Tanzania

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Feb 24, 2012
5,011
9,879
Watu 49 wanaodaiwa kuingia Tanzania bila utaratibu wakitokea Ethiopia wamekamatwa jana jioni Jumanne Novemba 3, 2020 na jeshi la uhifadhi na Misitu kikosi cha Tanapa katika hifadhi ya Taifa Saadani.

Wamekamatwa katika kijiji cha Saadani, kando ya Bahari ya Hindi, Bagamoyo mkoani Pwani.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Jumatano Novemba 4, 2020 na Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi, Paschal Shalutete inaeleza kuwa uongozi wa hifadhi ya Saadani umewakabidhi washukiwa hao kwa jeshi la Polisi na Idara ya Uhamiaji kwa hatua zaidi za kisheria.

“Tanapa inaendelea kusisitiza na kutoa onyo kwa wale wote wenye dhamira ya kutumia hifadhi za Taifa kwa vitendo ambavyo ni kinyume na sheria za nchi kuacha mara moja.”

“Jeshi la uhifadhi na misitu limejipanga vema kuhakikisha kuwa maeneo ya hifadhi yanaendelea kuwa salama kwa shughuli za uhifadhi na utalii na si vinginevyo,” imeeleza taarifa hiyo.
 
Wangejua hali ngumu ilivyo huku kwetu Tanzania, basi wangebakia huko huko kwao.
Niulize mimi niliekaa Ethiopia huku kwetu kwa Hali tuliyonayo bado ni heaven ukilinganisha na Ethiopia.

Watu wanakunywa kahawa ndo chakula Cha usiku. Kahawa kavu hamna kashata wa karanga. Watu wamekonda Hadi unawaonea huruma.

Watu kula kiazi Cha kuchemsha tu ni anasa. Nyie Duniani Kuna watu Wana shida saana. Ukitembea kwenye nchi hizo unapiga magoti unasema Mungu Asante kwa upendeleo wako wa kupafanya Tanzania pawe home.

Ni hatari!
 
Watu 49 wanaodaiwa kuingia Tanzania bila utaratibu wakitokea Ethiopia wamekamatwa jana jioni Jumanne Novemba 3, 2020 na jeshi la uhifadhi na Misitu kikosi cha Tanapa katika hifadhi ya Taifa Saadani.

Wamekamatwa katika kijiji cha Saadani, kando ya Bahari ya Hindi, Bagamoyo mkoani Pwani.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo Jumatano Novemba 4, 2020 na Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi, Paschal Shalutete inaeleza kuwa uongozi wa hifadhi ya Saadani umewakabidhi washukiwa hao kwa jeshi la Polisi na Idara ya Uhamiaji kwa hatua zaidi za kisheria.

“Tanapa inaendelea kusisitiza na kutoa onyo kwa wale wote wenye dhamira ya kutumia hifadhi za Taifa kwa vitendo ambavyo ni kinyume na sheria za nchi kuacha mara moja.”

“Jeshi la uhifadhi na misitu limejipanga vema kuhakikisha kuwa maeneo ya hifadhi yanaendelea kuwa salama kwa shughuli za uhifadhi na utalii na si vinginevyo,” imeeleza taarifa hiyo.
Pamoja na kuwa Ethiopia wanamiradi mikubwa mingi ya maendeleo na uchumi wao unakuwa lakini watu wao bado wanakimbia kwao, kulikoni?!
 
Niulize mimi niliekaa Ethiopia huku kwetu kwa Hali tuliyonayo bado ni heaven ukilinganisha na Ethiopia.

Watu wanakunywa kahawa ndo chakula Cha usiku. Kahawa kavu hamna kashata wa karanga. Watu wamekonda Hadi unawaonea huruma.

Watu kula kiazi Cha kuchemsha tu ni anasa. Nyie Duniani Kuna watu Wana shida saana. Ukitembea kwenye nchi hizo unapiga magoti unasema Mungu Asante kwa upendeleo wako wa kupafanya Tanzania pawe home.

Ni hatari!

mkuu msamehe tu ameshiba dona anachora tu sasa kwa kutumia simu.

mtz ni kiumbe ambaye ana uhakika wa kula milo mitatu bila kuwa na ramani rasmi,ila analia maisha magumu.
 
Kuna mataifa kusafiri ndiyo utamaduni wao,kitu kingine wengi wao siyo Waethiopia ni Waeritrea,Waethiopia na wasomali safari wameanza kitambo sana kuwakuta kwenye hizi njia za panyaaa ni mara mojamoja sana.
 
Niulize mimi niliekaa Ethiopia huku kwetu kwa Hali tuliyonayo bado ni heaven ukilinganisha na Ethiopia.

Watu wanakunywa kahawa ndo chakula Cha usiku. Kahawa kavu hamna kashata wa karanga. Watu wamekonda Hadi unawaonea huruma.

Watu kula kiazi Cha kuchemsha tu ni anasa. Nyie Duniani Kuna watu Wana shida saana. Ukitembea kwenye nchi hizo unapiga magoti unasema Mungu Asante kwa upendeleo wako wa kupafanya Tanzania pawe home.

Ni hatari!
Mzee unajua hao wanaosafiri wanakuwa na mtaji wa dola ngapi? Hawa wanaosafiri sio wanaosgindia kahawa
 
Niulize mimi niliekaa Ethiopia huku kwetu kwa Hali tuliyonayo bado ni heaven ukilinganisha na Ethiopia.

Watu wanakunywa kahawa ndo chakula Cha usiku. Kahawa kavu hamna kashata wa karanga. Watu wamekonda Hadi unawaonea huruma.

Watu kula kiazi Cha kuchemsha tu ni anasa. Nyie Duniani Kuna watu Wana shida saana. Ukitembea kwenye nchi hizo unapiga magoti unasema Mungu Asante kwa upendeleo wako wa kupafanya Tanzania pawe home.

Ni hatari!
Mungu ahsante kwa kuwa Tanzania...alhamdulillah
 
mkuu msamehe tu ameshiba dona anachora tu sasa kwa kutumia simu.

mtz ni kiumbe ambaye ana uhakika wa kula milo mitatu bila kuwa na ramani rasmi,ila analia maisha magumu.
Tanzania ni pahala pa ajabu mno, watu wengi wasio na kazi rasmi wanakula na kunywa Kama wafanyakazi wa nchi nyingine.

Imagine kwa mtu anaeishi Rwanda kula mchele wa kutoka mbeya Tanzania ni heshima na nembo ya mafanikio coz wengi wanakula mchele kitumbo wa kutoka Pakistan mchele haunukii.. mchele Kama ugali!

Wakati Kibongo Bongo watoto hata wa vijijini wanakula wali vizuri tu! Kuna watoto huko Mbarali-Mbeya wali kwao umewakifu!
 
Mzee unajua hao wanaosafiri wanakuwa na mtaji wa dola ngapi? Hawa wanaosafiri sio wanaosgindia kahawa
Muethiopia hanaga budget wala plan ndo maana wanaishiaga kukamatwa kizembe njiani.

Waeritrea at least wao huwa Wana budget, plan, na vision.

Nimekaa nao wote Hawa pale border ya Moyale Kenya wakiwa wanapanga mipango yao ya kusafiri nawajua vyema uzuri.
 
Niulize mimi niliekaa Ethiopia huku kwetu kwa Hali tuliyonayo bado ni heaven ukilinganisha na Ethiopia.

Watu wanakunywa kahawa ndo chakula Cha usiku. Kahawa kavu hamna kashata wa karanga. Watu wamekonda Hadi unawaonea huruma.

Watu kula kiazi Cha kuchemsha tu ni anasa. Nyie Duniani Kuna watu Wana shida saana. Ukitembea kwenye nchi hizo unapiga magoti unasema Mungu Asante kwa upendeleo wako wa kupafanya Tanzania pawe home.

Ni hatari!
Changamoto nini huko hata watu wa vijijini kwenye mashamba wanaashida Kama hizo au Ni wale wa mjini maaana vijijini unaweza kuta wanalima mazao ya chakula au sehemu kubwa ya Nchi ina ukame?
Hebu funguka kidogo utueleweshe maana kwa serikali yetu hiii Nasikia wadau wanasema tutakuwa Kama Ethiopi.​
 
Changamoto nini huko hata watu wa vijijini kwenye mashamba wanaashida Kama hizo au Ni wale wa mjini maaana vijijini unaweza kuta wanalima mazao ya chakula au sehemu kubwa ya Nchi ina ukame?
Hebu funguka kidogo utueleweshe maana kwa serikali yetu hiii Nasikia wadau wanasema tutakuwa Kama Ethiopi.​
Tatizo kubwa kule ukame.. sehemu kubwa ya ardhi Haina rutuba kwa hiyo chakula kinapatikana kidogo saana. Majirani zao wote hawana chakula Cha kutosha iwe kenya, Eritrea, Somalia na Sudan wote Wana njaa Kali.

Isitoshe! Uchumi wao ni hovyo saana wameweka hela yote kwenye kujenga matreni, mareli na mabarabara ilhali uchumi wao kwa mtu mmoja mmoja ni taabani.

Ethiopia Kuna njaa balaa! Watu wamekonda Kama watakufa kesho.
 
Tatizo kubwa kule ukame.. sehemu kubwa ya ardhi Haina rutuba kwa hiyo chakula kinapatikana kidogo saana. Majirani zao wote hawana chakula Cha kutosha iwe kenya, Eritrea, Somalia na Sudan wote Wana njaa Kali.

Isitoshe! Uchumi wao ni hovyo saana wameweka hela yote kwenye kujenga matreni, mareli na mabarabara ilhali uchumi wao kwa mtu mmoja mmoja ni taabani.

Ethiopia Kuna njaa balaa! Watu wamekonda Kama watakufa kesho.

mbaya zaidi kipimo cha uchumi ni pato la taifa kwa mwaka yaani GDP,ethiopia ni miongoni mwa nchi zenye uchumi mkubwa africa.
 
mbaya zaidi kipimo cha uchumi ni pato la taifa kwa mwaka yaani GDP,ethiopia ni miongoni mwa nchi zenye uchumi mkubwa africa.
Gross Domestic product ni wizi kabisa kupimia nchi za Africa. Mnaweza kufa na njaa huku Dunia inajua nyie wa kishua kumbe deep down mambo ni mperampera.

Maana hata maji kunywa shida Ethiopia sababu Kuna ukame. Imagine hata kushindia maji haiwezekani sababu hayapatikani kirahisi.

Kuna nchi watu wanaishi kama wako jehanamu kabisa na Kuna wengine wanaishi Kama wako heaven Hapa Hapa Duniani kwa Mungu.

UAE Kuna baadhi ya vituo vya daladala vina air conditioning.
 
Niulize mimi niliekaa Ethiopia huku kwetu kwa Hali tuliyonayo bado ni heaven ukilinganisha na Ethiopia.

Watu wanakunywa kahawa ndo chakula Cha usiku. Kahawa kavu hamna kashata wa karanga. Watu wamekonda Hadi unawaonea huruma.

Watu kula kiazi Cha kuchemsha tu ni anasa. Nyie Duniani Kuna watu Wana shida saana. Ukitembea kwenye nchi hizo unapiga magoti unasema Mungu Asante kwa upendeleo wako wa kupafanya Tanzania pawe home.

Ni hatari!
Yaani ukitoka Addis Airport hizo taxi, lazima uhisi umepotea, ukiachia Sheraton, yaani kuna watu wanaishi maisha magumu SANA, acha wakimbie nchi, jamani..

Pilots wao ni maskini hela wanalipwa peanuts, niliwaangalia wale watu nikaelewa kwanini wanakubali kukaa ndani ya container kwenda Sauzi.

Everyday is Saturday............................... :cool:
 
Back
Top Bottom