Wahamiaji 31 wagunduliwa kwenye lori Ufaransa

Wahamiaji 31 wagunduliwa kwenye lori Ufaransa

beth

JF-Expert Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
3,881
Reaction score
6,377
Polisi nchini Ufaransa imegundua uwepo wa wahamiaji 31 waliokuwa nyuma ya lori ikiwa ni pamoja na watoto ambao hawakuwa na mzazi ama mlezi.

Kulingana na mwendesha mashtaka wa umma mjini Nice nchini Ufaransa, kwenye tukio la jana Jumamosi maafisa hao wa polisi waligundua uwepo wa wahamiaji hao wakati wakifanya ukaguzi wa kawaida wa barabarani.

Miongoni mwa wahamiaji hao ni watoto wasio na wazazi wala walezi, na waligunduliwa wakati wa ukaguzi huo kwenye mji wa La Tubier ulioko karibu na mpaka wa Italia.

Mwendesha mashitaka huyo amesema wahamiaji wote 31 waliokuwa kwenye lori ni raia wa Pakistan. Dereva wa lori ambaye pia ni raia wa Pakistan alikamatwa na mamlaka za Ufaransa.

Wahamiaji hao pia hatimaye walikabidhiwa kwa mamlaka za Italia, hii ikiwa ni kulingana na gazeti la Ufaransa la Nice-Martin.

Waendesha mashitaka, pamoja na mambo mengine watafanya uchunguzi kuangazia iwapo matukio kama haya yanahusiana na biashara haramu ya binadamu. Na iwapo watagundua kwamba hakuna mahusiano, dereva wa lori hilo atashitakiwa kwa kuwasaidia watu hao kuingia kinyume cha sheria za uhamiaji, hii ikiwa ni kulingana na shirika la habari la AFP.
 
Hivi kwa nini wasikimbilie Oman,Qatar,United Emirates au Saudi Arabia ? Kwa nini wanakimbilia Ulaya ? Wakati Oman maisha mazuri kuliko France ?
 
D😀😀😀.... Fuatilia vizuri operation za hao wauwaji wanazozifanya katika hizo nchi, yaani mpaka juzi kati Pakistan ilikua inalalamika kuwa marekani inauwa watu wasiokua na hatia kwa kutumia drone zisizokua na rubani, karibia maelf ya raia wa nchi hio wameuwawa na marekani bila ya hatia yyte, wakatishia kuripua ndege za marekani ambazo zitakua zinaendeleza operation zake nchini humo, apo kidogo marekani akapunguza fujo zake
Pakistan ni nchi salama kabisa haijawahi vamiwa na marekani au NATO Kwa hy point yako ni irrelevant
 
Pakistani raia wake wana haki ya kwenda nchi za ulaya na marekani kwa sababu nchini mwao kuna wanajeshi ambao wanaendeleza operation za kuuwa watu wasiokua na hatia, kama hutaki wageni nchini mwako basi usiingilie nchi za wengine
Pakistan ni nchi salama kabisa haijawahi vamiwa na marekani au NATO Kwa hy point yako ni irrelevant
 
Kwa nini wapakistan wanakimbilia kwa makafiri kwa nini wasifanye nchi yao iwe kama akhera ili wengine wapende kupakimbiliapo?
... ha ha ha! Swali muhimu sana hili japo halitapata majibu kamilifu. Watakuambia wamerikani na mayahudi wameiharibu Pakistan.
 
D😀😀😀.... Fuatilia vizuri operation za hao wauwaji wanazozifanya katika hizo nchi, yaani mpaka juzi kati Pakistan ilikua inalalamika kuwa marekani inauwa watu wasiokua na hatia kwa kutumia drone zisizokua na rubani, karibia maelf ya raia wa nchi hio wameuwawa na marekani bila ya hatia yyte, wakatishia kuripua ndege za marekani ambazo zitakua zinaendeleza operation zake nchini humo, apo kidogo marekani akapunguza fujo zake
Unajua maana vita ni kama vile Afghanistan na Iraq zilivyo vamiwa si hivyo vya pakistan
 
Kwa nini wapakistan wanakimbilia kwa makafiri kwa nini wasifanye nchi yao iwe kama akhera ili wengine wapende kupakimbiliapo?
Hasa viongozi wao ndio wanafiki wakubwa, wakiwa kwao uwadanganya wanao waongoza kwamba makafiri na elimu yao ya magharibi ni watu wa jehanamu.
Lakini ajabu ni kwamba hao viongozi wao uwapeleka watoto wao Ulaya kwenda kusoma kwa makafili ili wapate elimu bora, na isitoshe pia wao wenyewe ukimbilia Ulaya kwenda kutafuta maisha bora.
 
Kwa nini wapakistan wanakimbilia kwa makafiri kwa nini wasifanye nchi yao iwe kama akhera ili wengine wapende kupakimbiliapo?
Unazingua kijana hii tambua Dunia haiwezi kuwa Sawa kila mtu anaangalia kwenye fursa ndio anakimbilia km walivyo baadhi ya Africa wanakimbilia ulaya pia baadhi yawatu ulaya wanakimbilia Africa kila mmoja kwake anaona fursa IPO Kwa upande wa mwingine
Mzungu anakimbilia Africa kuwekeza
Mwafrica anakimbilia ulaya kufanya Kazi
Kwahiyo usishangae mpakistani kukimbilia ulaya
Huwenda atawewe pia mkoa, Kijiji,/nchi uliyokimbilia kutafuta rizki hukuzariwa hapo.
 
Back
Top Bottom