beth
JF-Expert Member
- Aug 19, 2012
- 3,881
- 6,377
Polisi nchini Ufaransa imegundua uwepo wa wahamiaji 31 waliokuwa nyuma ya lori ikiwa ni pamoja na watoto ambao hawakuwa na mzazi ama mlezi.
Kulingana na mwendesha mashtaka wa umma mjini Nice nchini Ufaransa, kwenye tukio la jana Jumamosi maafisa hao wa polisi waligundua uwepo wa wahamiaji hao wakati wakifanya ukaguzi wa kawaida wa barabarani.
Miongoni mwa wahamiaji hao ni watoto wasio na wazazi wala walezi, na waligunduliwa wakati wa ukaguzi huo kwenye mji wa La Tubier ulioko karibu na mpaka wa Italia.
Mwendesha mashitaka huyo amesema wahamiaji wote 31 waliokuwa kwenye lori ni raia wa Pakistan. Dereva wa lori ambaye pia ni raia wa Pakistan alikamatwa na mamlaka za Ufaransa.
Wahamiaji hao pia hatimaye walikabidhiwa kwa mamlaka za Italia, hii ikiwa ni kulingana na gazeti la Ufaransa la Nice-Martin.
Waendesha mashitaka, pamoja na mambo mengine watafanya uchunguzi kuangazia iwapo matukio kama haya yanahusiana na biashara haramu ya binadamu. Na iwapo watagundua kwamba hakuna mahusiano, dereva wa lori hilo atashitakiwa kwa kuwasaidia watu hao kuingia kinyume cha sheria za uhamiaji, hii ikiwa ni kulingana na shirika la habari la AFP.
Kulingana na mwendesha mashtaka wa umma mjini Nice nchini Ufaransa, kwenye tukio la jana Jumamosi maafisa hao wa polisi waligundua uwepo wa wahamiaji hao wakati wakifanya ukaguzi wa kawaida wa barabarani.
Miongoni mwa wahamiaji hao ni watoto wasio na wazazi wala walezi, na waligunduliwa wakati wa ukaguzi huo kwenye mji wa La Tubier ulioko karibu na mpaka wa Italia.
Mwendesha mashitaka huyo amesema wahamiaji wote 31 waliokuwa kwenye lori ni raia wa Pakistan. Dereva wa lori ambaye pia ni raia wa Pakistan alikamatwa na mamlaka za Ufaransa.
Wahamiaji hao pia hatimaye walikabidhiwa kwa mamlaka za Italia, hii ikiwa ni kulingana na gazeti la Ufaransa la Nice-Martin.
Waendesha mashitaka, pamoja na mambo mengine watafanya uchunguzi kuangazia iwapo matukio kama haya yanahusiana na biashara haramu ya binadamu. Na iwapo watagundua kwamba hakuna mahusiano, dereva wa lori hilo atashitakiwa kwa kuwasaidia watu hao kuingia kinyume cha sheria za uhamiaji, hii ikiwa ni kulingana na shirika la habari la AFP.