Habari wadau poleni na majukumu ya kujenga Taifa.
Moja kwa moja kwenye mada .Nimekuwa nikifuatilia tabia za hawajamaa kwenye matukio yote ya kiserikali mfano sensa na uchaguzi .Hawa jamaa huwa wako makini sana ili uwapate lazima uwape nyama .
Mfano sensa ya mwaka juzi walipewa nyama iliwahesabiwe. Haya jana tena wamepewa nyama ili wajiandikishe kwenye daftari la wapiga kura kwenye serikali za mtaa .
Maana yake ninini nikwamba jamaa wameshaona hawana cha kupoteza sisi mtupe nyama tule nyie muendelee kujipitisha.
Haingii kwenye akili yani watuwazima na akili zao wakajiandikishe halafu mshindwe kuheshimu sanduku la kura.
Kiufupi nyie muendelee kujipitisha wapeni watu nyama.
Namalizia kwa kusema "NI MWENDO WA KUGARAGARA."