Elections 2010 Wagombea Ubunge Morogoro kwa CHADEMA warejesha form; Waahidi makubwa

Ramos

JF-Expert Member
May 13, 2010
498
130
Wagombea ubunge kwa Majimbo ya Morogoro Mjini na Morogoro Kusini mashariki kupitia CHADEMA wamerejesha form zao leo na kuahidi kufanya makubwa endapo wakichaguliwa.

Mwanasheria Amani Mwaipaja ambaye anagombea kwa chama hicho Morogoro mjini amewaambia waandishi wa habari kuwa endapo atachaguliwa atatumia jitihada na uwezo wake wote kuhakikisha kuwa mji huo unapata hadhi na heshima yake kama zamani. Ameyataja maeneo atakayoweka nguvu kubwa kuwa ni maji, barabara, maeneo ya wafanyabiashara wadogo na vikundi vya kujiendeleza kiuchumi hasa kwa wanawake.

Naye Bw. Aquiline Magalambula ambaye anagombea katika jimbo la Morogoro kusini mashariki ameahidi kuweka nguvu kubwa katika kuboresha upatikanaji wa maji safi na salama, umeme vijijini, barabara na kilimo.

(nimeshindwa ku-upload picha; naomba wadau mnielekeze)
 
Wagombea ubunge kwa Majimbo ya Morogoro Mjini na Morogoro Kusini mashariki kupitia CHADEMA wamerejesha form zao leo na kuahidi kufanya makubwa endapo wakichaguliwa.

Mwanasheria Amani Mwaipaja ambaye anagombea kwa chama hicho Morogoro mjini amewaambia waandishi wa habari kuwa endapo atachaguliwa atatumia jitihada na uwezo wake wote kuhakikisha kuwa mji huo unapata hadhi na heshima yake kama zamani. Ameyataja maeneo atakayoweka nguvu kubwa kuwa ni maji, barabara, maeneo ya wafanyabiashara wadogo na vikundi vya kujiendeleza kiuchumi hasa kwa wanawake.

Naye Bw. Aquiline Magalambula ambaye anagombea katika jimbo la Morogoro kusini mashariki ameahidi kuweka nguvu kubwa katika kuboresha upatikanaji wa maji safi na salama, umeme vijijini, barabara na kilimo.

(nimeshindwa ku-upload picha; naomba wadau mnielekeze)

Heshima kwako Ramos,

Mkuu ingekuwa jambo la maana kama ungeweka profile za wagombea ubunge na ikiwezekana weka profile za wagombea wa vyama vyote vinavyoshiriki kugombea ubunge huko Morogoro ili wanajamvi tuyasome na kuwachambua.Ukianza kuleta wagombea wa chama chako tu utakuwa huwatedei haki wanajamvi na watanzania kwa ujumla.

Wanajamvi wa majimbo mengine tafadhali tuleteeni yanayojiri kwenye majimbo yenu.
 
Nitazitafuta mkuu. Ilitokea tu kuwa wakati wanarejesha hawa wa CHADEMA nilikuwa around, nikalinasa tukio...
 
Back
Top Bottom