Wagombea ubunge kwa Majimbo ya Morogoro Mjini na Morogoro Kusini mashariki kupitia CHADEMA wamerejesha form zao leo na kuahidi kufanya makubwa endapo wakichaguliwa.
Mwanasheria Amani Mwaipaja ambaye anagombea kwa chama hicho Morogoro mjini amewaambia waandishi wa habari kuwa endapo atachaguliwa atatumia jitihada na uwezo wake wote kuhakikisha kuwa mji huo unapata hadhi na heshima yake kama zamani. Ameyataja maeneo atakayoweka nguvu kubwa kuwa ni maji, barabara, maeneo ya wafanyabiashara wadogo na vikundi vya kujiendeleza kiuchumi hasa kwa wanawake.
Naye Bw. Aquiline Magalambula ambaye anagombea katika jimbo la Morogoro kusini mashariki ameahidi kuweka nguvu kubwa katika kuboresha upatikanaji wa maji safi na salama, umeme vijijini, barabara na kilimo.
(nimeshindwa ku-upload picha; naomba wadau mnielekeze)
Mwanasheria Amani Mwaipaja ambaye anagombea kwa chama hicho Morogoro mjini amewaambia waandishi wa habari kuwa endapo atachaguliwa atatumia jitihada na uwezo wake wote kuhakikisha kuwa mji huo unapata hadhi na heshima yake kama zamani. Ameyataja maeneo atakayoweka nguvu kubwa kuwa ni maji, barabara, maeneo ya wafanyabiashara wadogo na vikundi vya kujiendeleza kiuchumi hasa kwa wanawake.
Naye Bw. Aquiline Magalambula ambaye anagombea katika jimbo la Morogoro kusini mashariki ameahidi kuweka nguvu kubwa katika kuboresha upatikanaji wa maji safi na salama, umeme vijijini, barabara na kilimo.
(nimeshindwa ku-upload picha; naomba wadau mnielekeze)