OgwaluMapesa
JF-Expert Member
- May 24, 2008
- 10,942
- 437
Ni kufuru iliyopitiliza inayoonyeshwa na baadhi ya wagombea watia nia ya kuutaka urais ambapo wanatumia fedha kupita kiasi katika zoezi la kusaka wadhamini huko mikoani.
Kwa wale wagombea ambao ni viongozi wa kiserikali wamekuwa wakitumia rasilimali za kiserikali kama vile magari, ndege, basi pamoja na madereva wa serikali katika mbio za urais.
BERNARD MEMBE
Membe amekuwa akitoa elfu arobaini (40,000/-) kwa kila mtu anayekuja kumdhamini katika urais. Pia anatembea na kundi la wasanii na watu maarufu ambao huwalipa kiasi cha Tsh. laki tatu (300,000/-) kwa kila mtu, kwa kila siku.
Wale wasaidizi wake ama wapambe wake wa karibu huwalipa kiasi cha Tsh. laki tano (500,000/-) kwa kila mtu, kila mtu.
Hapo achilia mbali gharama za kukodisha magari, gharama ya mafuta kwa wanaotumia magari binafsi na posho za madereva na walinzi.
Tusisahau ni Membe huyu huyu anayejipambanua kupiga vita rushwa na ufisadi wakati matendo anayoyafanya mikoani yanadhihirisha kubariki rushwa nchini.
Pia Membe anasaidiwa na tajiri mkubwa Afrika ambaye amekuja kuwekeza kusini mwa Tanzania
MAKONGORO NYERERE
Huyu ni mtoto wa Baba wa Taifa Mwl J.K Nyerere ambaye anajinasibu mara zote kuwa ni mtu safi asiye na doa, mpiga vita ufisadi nchini na mtu maskini.
Kwa mujibu wa taarifa za kina zinaonyesha Makongoro naye anatumia pesa kama kawaida katika zoezi hili la kusaka wadhamini.
Makongoro hutoa kiasi cha Tsh. elfu kumi (10,000/-) hadi elfu ishirini (20,000/-) kwa kila mtu anayedondoka wino wa kumdhamini kwa kila mkoa anaopita kusaka wadhamini.
Kama haitoshi Makongoro huambatana na kundi la wapambe na waandishi wa habari ambao huwalipa kiasi cha Tsh. elfu hamsini (50,000/-) kwa kila mtu kila siku.
Sote tujiulize mtu maskini yupo hivi? Pesa zote hizi za kuwalipa watu amezitoa wapi? Kama huyu si fisadi basi tumwiteje?
MWIGULU NCHEMBA
Huyu ni Naibu waziri wa fedha ambaye amejitosa katika kinyang'anyiro cha urais akiwa mmoja wapo wa watia nia kijana kabisa.
Mwigulu yeye hutoa kiasi cha Tsh. Elfu ishirini na tano (25,000/-) kwa kila mtu anayejitokeza kumdhamini.
Pia Mwigulu anatembea na wapambe wake maarufu kama "masalia wa chadema" pamoja ambao huwapa posho ya Tsh. laki moja kila siku pamoja na kugharamikia mafuta ya magari yao.
Pia Mwigulu huambatana na mpiga picha wake aitwaye Festo Sanga pamoja na aliyekuwa msaidizi wake wa Unaibu katibu wa CCM (Myeka) aitwaye Rubein ambaye huwalipa posho ya Tsh. laki mbili kwa kila siku. Pia hutoa hela ya mafuta ya gari lao.
Mwigulu huzunguka na gari la serikali na kutoa posho kwa madereva wote wa msafara.
SOSPETER MUHONGO
Muhongo amekuwa akitoa kiasi cha Tsh. elfu thelathini (30,000/-) kwa kila mtu anayejitokeza kumdhamini.
Pia Muhongo huzunguka na wapambe wake wapatao 50 ambao huwalipa kiasi cha Tsh. Elfu hamsini kwa kila mtu kila siku ambapo amewakodishia coaster wanalozunguka naye.
LAZARO NYALANDU
Nyalandu yeye huzunguka kwa kutumia ndege ya TANAPA na kutumia magari ya serikali kila mkoa anapokuwa.
Nyalandu hutoa kiasi cha Tsh. elfu ishirini (20,000/-) kwa kila mtu anayejitokeza kumdhamini.
Wapambe wake huwapa kiasi cha Tsh. laki moja kila siku ambapo hutembea na wapambe wasiopungua 30 kwenye kila mkoa.
SAMWEL SITTA
Sitta yeye anatumia basi maalum la wizara ya uchukuzi ambalo lina mpaka sebule ndani yake. Basi hilo hupanda yeye pamoja na wapambe wake. Katika msafara wake gari lake la serikali linakuwepo pia kwenye msafara.
Wasaidizi wake huwalipa Tsh. laki moja kwa kila siku kwa kila mtu. Pia hugharamikia mafuta ya basi pamoja na kutoa posho kwa madereva wake.
Sitta hutoa kiasi cha Tsh. elfu kumi na tano kwa kila mtu anayejitokeza kumdhamini.
Sitta ni maarufu sana kwa kupiga vita mafisadi lakini matendo yake yanaonyesha ana punje za ufisadi mdomoni.
STEVEN WASIRA
Wassira ni mmoja wapo wa wagombea ambaye anakumbukwa kwa kipindi cha nyuma kutuhumia na mahakama kwa kutoa rushwa wakati wa uchaguzi na hivyo kuvuliwa ubunge wake na mahakama.
Wassira amekuwa akizunguka na gari la serikali na kutoa kiasi cha Tsh. elfu ishirini tu kwa kila mtu anayejitokeza kumdhamini.
JANUARI MAKAMBA
Makamba amejitokeza katika mbio za kuisaka ikulu ambaye amekuwa akinunua kadi za watu kumdhamini kwa Tsh. elfu ishirini kwa kila mtu.
Januari hutumia gari la serikali katika kampeni zake.
JOHN POMBE MAGUFULI
Magufuli anazunguka mikoani kwa kutumia gari la serikali lenye plate number inayosomeka W UJ na hutoa kiasi cha elfu ishirini kwa kila mtu anayejitokeza kumdhamini.
DR. TITUS KAMANI
Kamani naye amejitosa kugombea na hutoa kiasi cha Tsh. elfu ishirini na tano (25,000/-) kwa kila mtu anayejitokeza kumdhamini. Amefanya hivyo katika mkoa wa Mwanza.
EDWARD LOWASSA
Edward Lowassa ambaye ni Waziri mkuu wa zamani anazunguka mikoani kwa kutumia gari binafsi na magari mawili ya wasaidizi na walinzi wake wapatao 10.
Lowassa huwalipa wasaidizi na walinzi wake kiasi cha Tsh. elfu kumi kwa kila siku.
Magari yake huwekwa mafuta na tajiri mmoja toka Arusha aliyejitolea kutoa huduma hiyo.
Kwa wale wanao mdhamini urais hupata fursa ya kusalimiana na kupiga picha nao na na kisha mpambe wake hutoa kiasi cha Tsh. elfu tano kwa baadhi ya wanaomdhamini Lowassa
..... Itaendelea .....
Kwa wale wagombea ambao ni viongozi wa kiserikali wamekuwa wakitumia rasilimali za kiserikali kama vile magari, ndege, basi pamoja na madereva wa serikali katika mbio za urais.
BERNARD MEMBE
Membe amekuwa akitoa elfu arobaini (40,000/-) kwa kila mtu anayekuja kumdhamini katika urais. Pia anatembea na kundi la wasanii na watu maarufu ambao huwalipa kiasi cha Tsh. laki tatu (300,000/-) kwa kila mtu, kwa kila siku.
Wale wasaidizi wake ama wapambe wake wa karibu huwalipa kiasi cha Tsh. laki tano (500,000/-) kwa kila mtu, kila mtu.
Hapo achilia mbali gharama za kukodisha magari, gharama ya mafuta kwa wanaotumia magari binafsi na posho za madereva na walinzi.
Tusisahau ni Membe huyu huyu anayejipambanua kupiga vita rushwa na ufisadi wakati matendo anayoyafanya mikoani yanadhihirisha kubariki rushwa nchini.
Pia Membe anasaidiwa na tajiri mkubwa Afrika ambaye amekuja kuwekeza kusini mwa Tanzania
MAKONGORO NYERERE
Huyu ni mtoto wa Baba wa Taifa Mwl J.K Nyerere ambaye anajinasibu mara zote kuwa ni mtu safi asiye na doa, mpiga vita ufisadi nchini na mtu maskini.
Kwa mujibu wa taarifa za kina zinaonyesha Makongoro naye anatumia pesa kama kawaida katika zoezi hili la kusaka wadhamini.
Makongoro hutoa kiasi cha Tsh. elfu kumi (10,000/-) hadi elfu ishirini (20,000/-) kwa kila mtu anayedondoka wino wa kumdhamini kwa kila mkoa anaopita kusaka wadhamini.
Kama haitoshi Makongoro huambatana na kundi la wapambe na waandishi wa habari ambao huwalipa kiasi cha Tsh. elfu hamsini (50,000/-) kwa kila mtu kila siku.
Sote tujiulize mtu maskini yupo hivi? Pesa zote hizi za kuwalipa watu amezitoa wapi? Kama huyu si fisadi basi tumwiteje?
MWIGULU NCHEMBA
Huyu ni Naibu waziri wa fedha ambaye amejitosa katika kinyang'anyiro cha urais akiwa mmoja wapo wa watia nia kijana kabisa.
Mwigulu yeye hutoa kiasi cha Tsh. Elfu ishirini na tano (25,000/-) kwa kila mtu anayejitokeza kumdhamini.
Pia Mwigulu anatembea na wapambe wake maarufu kama "masalia wa chadema" pamoja ambao huwapa posho ya Tsh. laki moja kila siku pamoja na kugharamikia mafuta ya magari yao.
Pia Mwigulu huambatana na mpiga picha wake aitwaye Festo Sanga pamoja na aliyekuwa msaidizi wake wa Unaibu katibu wa CCM (Myeka) aitwaye Rubein ambaye huwalipa posho ya Tsh. laki mbili kwa kila siku. Pia hutoa hela ya mafuta ya gari lao.
Mwigulu huzunguka na gari la serikali na kutoa posho kwa madereva wote wa msafara.
SOSPETER MUHONGO
Muhongo amekuwa akitoa kiasi cha Tsh. elfu thelathini (30,000/-) kwa kila mtu anayejitokeza kumdhamini.
Pia Muhongo huzunguka na wapambe wake wapatao 50 ambao huwalipa kiasi cha Tsh. Elfu hamsini kwa kila mtu kila siku ambapo amewakodishia coaster wanalozunguka naye.
LAZARO NYALANDU
Nyalandu yeye huzunguka kwa kutumia ndege ya TANAPA na kutumia magari ya serikali kila mkoa anapokuwa.
Nyalandu hutoa kiasi cha Tsh. elfu ishirini (20,000/-) kwa kila mtu anayejitokeza kumdhamini.
Wapambe wake huwapa kiasi cha Tsh. laki moja kila siku ambapo hutembea na wapambe wasiopungua 30 kwenye kila mkoa.
SAMWEL SITTA
Sitta yeye anatumia basi maalum la wizara ya uchukuzi ambalo lina mpaka sebule ndani yake. Basi hilo hupanda yeye pamoja na wapambe wake. Katika msafara wake gari lake la serikali linakuwepo pia kwenye msafara.
Wasaidizi wake huwalipa Tsh. laki moja kwa kila siku kwa kila mtu. Pia hugharamikia mafuta ya basi pamoja na kutoa posho kwa madereva wake.
Sitta hutoa kiasi cha Tsh. elfu kumi na tano kwa kila mtu anayejitokeza kumdhamini.
Sitta ni maarufu sana kwa kupiga vita mafisadi lakini matendo yake yanaonyesha ana punje za ufisadi mdomoni.
STEVEN WASIRA
Wassira ni mmoja wapo wa wagombea ambaye anakumbukwa kwa kipindi cha nyuma kutuhumia na mahakama kwa kutoa rushwa wakati wa uchaguzi na hivyo kuvuliwa ubunge wake na mahakama.
Wassira amekuwa akizunguka na gari la serikali na kutoa kiasi cha Tsh. elfu ishirini tu kwa kila mtu anayejitokeza kumdhamini.
JANUARI MAKAMBA
Makamba amejitokeza katika mbio za kuisaka ikulu ambaye amekuwa akinunua kadi za watu kumdhamini kwa Tsh. elfu ishirini kwa kila mtu.
Januari hutumia gari la serikali katika kampeni zake.
JOHN POMBE MAGUFULI
Magufuli anazunguka mikoani kwa kutumia gari la serikali lenye plate number inayosomeka W UJ na hutoa kiasi cha elfu ishirini kwa kila mtu anayejitokeza kumdhamini.
DR. TITUS KAMANI
Kamani naye amejitosa kugombea na hutoa kiasi cha Tsh. elfu ishirini na tano (25,000/-) kwa kila mtu anayejitokeza kumdhamini. Amefanya hivyo katika mkoa wa Mwanza.
EDWARD LOWASSA
Edward Lowassa ambaye ni Waziri mkuu wa zamani anazunguka mikoani kwa kutumia gari binafsi na magari mawili ya wasaidizi na walinzi wake wapatao 10.
Lowassa huwalipa wasaidizi na walinzi wake kiasi cha Tsh. elfu kumi kwa kila siku.
Magari yake huwekwa mafuta na tajiri mmoja toka Arusha aliyejitolea kutoa huduma hiyo.
Kwa wale wanao mdhamini urais hupata fursa ya kusalimiana na kupiga picha nao na na kisha mpambe wake hutoa kiasi cha Tsh. elfu tano kwa baadhi ya wanaomdhamini Lowassa
..... Itaendelea .....