Tape measure
JF-Expert Member
- Nov 26, 2015
- 1,988
- 3,688
kwanza kabisa niwaombe radhi ambao nitawakwanza kutokana na imani zao lakini pia niseme kutokufahamu ama kukutana na jambo fulani haiondoi uhalisia wa uwepo wa jambo husika.
Nirudi kwenye mada "Waganga wa jadi" kwa waliokulia vijijini si ajabu kusikia fulani ni mchawi ama koo fulani usioe kwakuwa ni wachawi hivyo basi ikitokea magonjwa ama matukio ambayo sio ya kawaida mfano mchanga kurushwa juu ya bati usiku wa manane au mapaka na bundi kupiga kelele kwa boma yao majira ya usiku, magonjwa yasioonekana hospital na mengineyo huhusishwa na mambo ya kishirikina na hapa ndipo MGANGA hupata riziki yake.
Binafsi nimewahi kushuhudia mambo mengi ya kichawi na yanayotisha nakumbuka mwaka 1999 alikuja mganga kutokea wilaya ya Rombo kipindi hicho kuna mzee alikua anasumbuliwa na mambo mengi yaani kama wehu muda mwingine na kupiga makelele.
ilipofika usiku majira ya sa 2 kazi ikaanza alichukuliwa kuku wakaenda nae shambani chini ya mti mkubwa wa mkenge( Albizia gumifera) huo mti ulikuwa na unene wa zaidi ya 300cm. umri wake ni zaidi ya miaka 100 huwezi kuamini baada ya yule kuku kufukiwa chini ya ule mti. Mti ulianza kutikisika na kupuputisha majani gafla ukaja upepo mkali ulioambatana na miale kama ya radi . Mganga alitoa maagizo pia itafutwe ngombe jike na achinjwe mtoni majira ya saa sita mchana hiyo shughuli ikafanyika kwa ustadi mkubwa siku hiyo sikuwepo mtaani nilitamani ningeshuhudia.
Tukio jingine nakumbuka ilikuwa ni kwenye milima ya Usangi kuna mganga mmoja ambaye yeye hutumia maruhani yaani mkienda kwake mnakaa kama mpo nyumba ya ibada watu wote kwa pamoja kisha yeye ndio anaanza kuelezea matatizo ya kila mmoja kadri atakavyojisikia yaani hapo hamna siri kama unatembea na mke wa mtu atakuambia kila kitu huyu binafsi niliamini kuwa Mungu yupo kwani ata ukitaka akueleze jana umekula chakula gani atakuambia. huyu nilitani kumuhoji lakini kutokana na wingi wa wateja wake sikufanikiwa.
Tukio lingine nakumbuka kuna kwa mganga anapatikana sijui ni tarakea ama ni wilayani panaitwa nimesahau kidogo hapa nilistajabu ya FIRAUNI huyo mama ambaye ndio mganga aka mtaalamu anaweka manukato na kuyawasha kwenye kitu kama bakuli then anakuwekea moshi wake ukuingie huku mmejifunika na shuka/kitenge/kitambaa ama kanga yani kama una mapepo lazima yaongee.
Baada ya hapo anafanya sala kwa lugha zake za kiarabu kisha mnaelekea shambani mnakaa pande mbili moja wanaume.na mwingine wanawake .....HAPA NDIO NILICHOKA KABISA DUU mnavua nguo zote mnabaki kama mlivozaliwa wababa. watoto asee dunia ina siri na mambo mengi sana ya ajabu na kutisha pia imani ni kitu si cha mchezo kabisa usishangae wafuasi wa Kibwetere kufungiwa katika kanisa na kisha wote kuungua kwa moto mpaka kuwa majivu wakiamini kesho yake ambayo ni 27/3/2000
wangejikuta mbinguni wamekaa na malaika na Mungu wanakula na.kunywa.
Mkishavua nguo mnapanga mstari kuna jiwe unakaa apo kisha yeye anachota maji ambayo yapo kwenye pipa hayo maji amechanganya na dawa anakumwagia kama vile inaoga na wanawake pia wanafanya ivyo yaani unaona KE na ME livee🤫🤫. leo hii nikisikia sijui freemason watu wanasali uchi wala sishangai kwani haya mambo yapo tu.
Tukio lingine ni Tanga kuna mganga anaitwa singano ni jina la ukoo hili nazani yeye anatibu na kutoa mapepo na mavitu kama hayo anawateja wengi lakini ni maskini wa kutupa ana moyo safi kama huna pesa anakutibia hata bure unampa ata buku 3 ukipona utarudi peke yako kumlipa deni lake .......KILICHONISTAJABISHA KWA HUYU anatoa kinga hii unameza moyo wa mnyama anachinjwa kisha moyo wake unachanganywa na dawa unapewa unameza moyo ukiwa bado unapumia ....sijui nisemeje apo nieleweke kirahisi.....moyo inategemeana unaweza kuwa moyo wa paka, sungura, kuku ni wewe na chaguo lako.....

Kilichonostajabisha zaidi kuna mganga anapatikana wilaya ya magu mkoa wa mwanza yaani huyu mtaalamu anafanya kazi na watu zaidi ya 10 ambao ni wasaidizi wake katika utafiti wangu kuna kitu cha kustajabisha sana nilikiona wanachukua viatu, ndala na sandals za watu nazani huziokota mitaani zilizochakaa kisha zinachemshwa na kuchanganywa na Dawa......
ushauri wangu hapa kama unama viatu yaliyochakaa na huvivai usitupe kwenye taka bora uvitie moto kwani WAGANGA ni watu wa.ajabu sana. pia kuna uwezekano mkubwa akawa na uhusiano wa karibu na wakina nanii...... hapa sina uhakika sana.........🤫🤫.
Tukio jingine ni mkoa wa morogoro wakazi wa wilaya ya Ulanga vijiji vya lupiro, kichangani, ikunguwa nazani mnawajua watalaamu wenu wa mvua mnaowaita MBUYU....kweli tembea uone mengi.
kuna mtaalamu mwingine sijui mganga huyu mambo yake nmeyasahau ni zamani sana anapatikana nane nane morogoro mjini huyo alikuwa ni kama.tapeli fulani kwani huwa anawatisha wateja wake mfano anamwambia kuwa hii dawa natakiwa nikaitafute baharini sijui natakiwa nikamkamate nyoka aina ya Black mamba kisha anakutajia bei kubwa ata laki 8 au millions kadha asee kuna siri nyingi sana huku duniani



.
Tukio jingine kuna mganga yupo wilaya ya longido njia ya kwenda Namanga mkoa wa Arusha huyu ana masharti ya ajabu kweli kwanza anafanya kazi siku 3 tu kwa wiki na nje ya boma lake amezungusha mawe na kuyapaka chokaa ikitokea mtu akakanyaga mawe hayo siku hiyo hafanyi kazi mpaka kesho yake usiombe ikatokea umeenda kwake alafu wewe ndio ukakanyaga wenzio watatamani kukumeza huyu mzee ni tajiri sana ana ngombe zaidi ya 200 nyumba yake ni za asili lakini amezijenga eneo kubwa sana pia kuna gari spesho yani kazi yake ni kupeleka watu kwake ni hiace inasemekana kuwa utajiri wake mwingi unatokana na asante kutoka kwa wateja wake baada ya kufanikiwa ........ nyuma ya pazia kuna mengi sana.
Nimalze kwa kusema Dawa watoazo waganga wengi za kuoga, kujipaka sijui kufukiza na mambo kama hayo nyingi ni home remedies mfano hutumia mkaa na kuusaga unakuwa kama unga ndio unapewa ukaogee
wakati mwingine hutumia chumvi hii pia husagwa na unaweza kuambiwa uogee na pia uweke kwa chai
.
MUNGU yupo pia shetani yupo na UCHAWI upo pia waganga wapo utofauti wa mganga na mchawi ni kuwa kuna wakati waganga wanaondoa na kuharibu mipango ya kichawi pia wanafanya mambo ya kichawi kama kufifisha nyota na kuuwa watu lakini kiuhalisia mganga hana tofauti sana na mchawi.
Nirudi kwenye mada "Waganga wa jadi" kwa waliokulia vijijini si ajabu kusikia fulani ni mchawi ama koo fulani usioe kwakuwa ni wachawi hivyo basi ikitokea magonjwa ama matukio ambayo sio ya kawaida mfano mchanga kurushwa juu ya bati usiku wa manane au mapaka na bundi kupiga kelele kwa boma yao majira ya usiku, magonjwa yasioonekana hospital na mengineyo huhusishwa na mambo ya kishirikina na hapa ndipo MGANGA hupata riziki yake.
Binafsi nimewahi kushuhudia mambo mengi ya kichawi na yanayotisha nakumbuka mwaka 1999 alikuja mganga kutokea wilaya ya Rombo kipindi hicho kuna mzee alikua anasumbuliwa na mambo mengi yaani kama wehu muda mwingine na kupiga makelele.
ilipofika usiku majira ya sa 2 kazi ikaanza alichukuliwa kuku wakaenda nae shambani chini ya mti mkubwa wa mkenge( Albizia gumifera) huo mti ulikuwa na unene wa zaidi ya 300cm. umri wake ni zaidi ya miaka 100 huwezi kuamini baada ya yule kuku kufukiwa chini ya ule mti. Mti ulianza kutikisika na kupuputisha majani gafla ukaja upepo mkali ulioambatana na miale kama ya radi . Mganga alitoa maagizo pia itafutwe ngombe jike na achinjwe mtoni majira ya saa sita mchana hiyo shughuli ikafanyika kwa ustadi mkubwa siku hiyo sikuwepo mtaani nilitamani ningeshuhudia.
Tukio jingine nakumbuka ilikuwa ni kwenye milima ya Usangi kuna mganga mmoja ambaye yeye hutumia maruhani yaani mkienda kwake mnakaa kama mpo nyumba ya ibada watu wote kwa pamoja kisha yeye ndio anaanza kuelezea matatizo ya kila mmoja kadri atakavyojisikia yaani hapo hamna siri kama unatembea na mke wa mtu atakuambia kila kitu huyu binafsi niliamini kuwa Mungu yupo kwani ata ukitaka akueleze jana umekula chakula gani atakuambia. huyu nilitani kumuhoji lakini kutokana na wingi wa wateja wake sikufanikiwa.
Tukio lingine nakumbuka kuna kwa mganga anapatikana sijui ni tarakea ama ni wilayani panaitwa nimesahau kidogo hapa nilistajabu ya FIRAUNI huyo mama ambaye ndio mganga aka mtaalamu anaweka manukato na kuyawasha kwenye kitu kama bakuli then anakuwekea moshi wake ukuingie huku mmejifunika na shuka/kitenge/kitambaa ama kanga yani kama una mapepo lazima yaongee.
Baada ya hapo anafanya sala kwa lugha zake za kiarabu kisha mnaelekea shambani mnakaa pande mbili moja wanaume.na mwingine wanawake .....HAPA NDIO NILICHOKA KABISA DUU mnavua nguo zote mnabaki kama mlivozaliwa wababa. watoto asee dunia ina siri na mambo mengi sana ya ajabu na kutisha pia imani ni kitu si cha mchezo kabisa usishangae wafuasi wa Kibwetere kufungiwa katika kanisa na kisha wote kuungua kwa moto mpaka kuwa majivu wakiamini kesho yake ambayo ni 27/3/2000
wangejikuta mbinguni wamekaa na malaika na Mungu wanakula na.kunywa.
Mkishavua nguo mnapanga mstari kuna jiwe unakaa apo kisha yeye anachota maji ambayo yapo kwenye pipa hayo maji amechanganya na dawa anakumwagia kama vile inaoga na wanawake pia wanafanya ivyo yaani unaona KE na ME livee🤫🤫. leo hii nikisikia sijui freemason watu wanasali uchi wala sishangai kwani haya mambo yapo tu.
Tukio lingine ni Tanga kuna mganga anaitwa singano ni jina la ukoo hili nazani yeye anatibu na kutoa mapepo na mavitu kama hayo anawateja wengi lakini ni maskini wa kutupa ana moyo safi kama huna pesa anakutibia hata bure unampa ata buku 3 ukipona utarudi peke yako kumlipa deni lake .......KILICHONISTAJABISHA KWA HUYU anatoa kinga hii unameza moyo wa mnyama anachinjwa kisha moyo wake unachanganywa na dawa unapewa unameza moyo ukiwa bado unapumia ....sijui nisemeje apo nieleweke kirahisi.....moyo inategemeana unaweza kuwa moyo wa paka, sungura, kuku ni wewe na chaguo lako.....


Kilichonostajabisha zaidi kuna mganga anapatikana wilaya ya magu mkoa wa mwanza yaani huyu mtaalamu anafanya kazi na watu zaidi ya 10 ambao ni wasaidizi wake katika utafiti wangu kuna kitu cha kustajabisha sana nilikiona wanachukua viatu, ndala na sandals za watu nazani huziokota mitaani zilizochakaa kisha zinachemshwa na kuchanganywa na Dawa......
ushauri wangu hapa kama unama viatu yaliyochakaa na huvivai usitupe kwenye taka bora uvitie moto kwani WAGANGA ni watu wa.ajabu sana. pia kuna uwezekano mkubwa akawa na uhusiano wa karibu na wakina nanii...... hapa sina uhakika sana.........🤫🤫.
Tukio jingine ni mkoa wa morogoro wakazi wa wilaya ya Ulanga vijiji vya lupiro, kichangani, ikunguwa nazani mnawajua watalaamu wenu wa mvua mnaowaita MBUYU....kweli tembea uone mengi.
kuna mtaalamu mwingine sijui mganga huyu mambo yake nmeyasahau ni zamani sana anapatikana nane nane morogoro mjini huyo alikuwa ni kama.tapeli fulani kwani huwa anawatisha wateja wake mfano anamwambia kuwa hii dawa natakiwa nikaitafute baharini sijui natakiwa nikamkamate nyoka aina ya Black mamba kisha anakutajia bei kubwa ata laki 8 au millions kadha asee kuna siri nyingi sana huku duniani




.Tukio jingine kuna mganga yupo wilaya ya longido njia ya kwenda Namanga mkoa wa Arusha huyu ana masharti ya ajabu kweli kwanza anafanya kazi siku 3 tu kwa wiki na nje ya boma lake amezungusha mawe na kuyapaka chokaa ikitokea mtu akakanyaga mawe hayo siku hiyo hafanyi kazi mpaka kesho yake usiombe ikatokea umeenda kwake alafu wewe ndio ukakanyaga wenzio watatamani kukumeza huyu mzee ni tajiri sana ana ngombe zaidi ya 200 nyumba yake ni za asili lakini amezijenga eneo kubwa sana pia kuna gari spesho yani kazi yake ni kupeleka watu kwake ni hiace inasemekana kuwa utajiri wake mwingi unatokana na asante kutoka kwa wateja wake baada ya kufanikiwa ........ nyuma ya pazia kuna mengi sana.
Nimalze kwa kusema Dawa watoazo waganga wengi za kuoga, kujipaka sijui kufukiza na mambo kama hayo nyingi ni home remedies mfano hutumia mkaa na kuusaga unakuwa kama unga ndio unapewa ukaogee
wakati mwingine hutumia chumvi hii pia husagwa na unaweza kuambiwa uogee na pia uweke kwa chai
.MUNGU yupo pia shetani yupo na UCHAWI upo pia waganga wapo utofauti wa mganga na mchawi ni kuwa kuna wakati waganga wanaondoa na kuharibu mipango ya kichawi pia wanafanya mambo ya kichawi kama kufifisha nyota na kuuwa watu lakini kiuhalisia mganga hana tofauti sana na mchawi.
