Wafugaji Tanzania waende wapi..?

Wafugaji Tanzania waende wapi..?

olee

Member
Joined
Nov 24, 2011
Posts
97
Reaction score
23
Kufuga mifugo mbalimbali ilianza toka zamani za kale. Binadamu alipewa uwezo wa kuwamiliki wanyama na kuwatumia anatakavyo kulingana na mahitaji yake. Mfano kulima, kupata nyama, maziwa, ngozi kwa matumizi mambalimbali, huongeza pato la taifa, ajira. Imezoeleka kwamba binadamu hasa wa kitanzania hufuga au humiliki wanyama kama mbuzi, ng'ombe, kondoo, punda na wengine wengi.


Tanzania inasifika dunia kwamba ni ya tatu afrika kwa kuwa na mifugo mengi. Tanzania kama nchi isingepata hii sifa kimataifa ingekua sio raia wake ndo wanaofuga. Serikali kama serikali isingeweza kufuga kiwango ambayo wafugaji binafi wanafanya. Vile sidhani hata kama serikali inayo mradi inayoiendesha kama serikali. Pamoja na hayo nchi yetu imekua ikifaidi yatokanayo kwa mifugo ndani na nje ya nchi kwa sababu raia wake wanafuga.


Pamoja na faida mfugaji anayoyapata kwa kufuga pia jamii nzima hufaidi kutoka kwa mifugo yake. Mfano katika jamii ya kitanzania hakuna mji unaweza ukaenda usikute bucher maana wanakula nyama kutoka kwa wafugaji wanaofuga kijijini, pia mijini kuna maziwa madukani iwe ya unga au ya packit au ya kupima inapatikana kutoka kwa mifugo husika, Vile vile watu wanafaa viatu na mavazi mengine yatokanayo na ngozi ya mifugo na faida nyingine ambayo jamii kwa ujumula inapata moja kwamoja kutoka kwa mifugo ambayo wao hawafugi.


Hata hivo serikali inafaidi mambo mengi kutoka kwa mifugo ikiwemo kupatikana kwa ajira kwa vijana aidha kwa kuwa wachungi wa mifugo au kufanya biashara ya mifugo au kwa kufanya biashara ya vitu yatokanayo kwa mifugo. Mfano biashara ya bucher, kuuza maziwa, ngozi n.k.


Pato la taifa huuongezeka kulingana na mapato yatokanayo na mifugo. Serikali inapata fedha za kigeni kutoka kwa mifgo mfano, kila siku mifugo aina ya mbuzi na kondoo wanapakiwa kwenye meli na kuwasafirisha nje ya nchi. Bila shaka serikali inafaidi mambo mengi kupitia kwa mifugo ikiwemo kukusanya kodi.

Lakini hawa wafugaji wanaotaabika kuifaidisha jamii ya kitanzania kwa kutoa huduma nzuri kwa watanzania kulingana na faida ya mifugo niliyotaja hapo juu hawajapewa kipau mbele ya maeneo ya kuwekeza. Wao wameoneka wanaharibu mazingira na kuoneka wanyang'anyi wa maeneo.


Hii imejidhihirisha wazi kwani kila siku kwenye vyombo vya habari ukisikia mapigano. Ni lazima iwe ni baina ya wafugaji na wakulima. Wafugaji mara nyingi ndo wanaonekana wakorofi, wameingilia maeneo ya wakulima, wameingilia sehemu ya mwekezaji, wameingiliea sehemu ya hifadhi.


Mfano mapigano iliyotokea huko INVOMERO, KITETO, LOLIONDO, NGORONGORO na sehumu zingine ilikua ni baina ya wafugaji wa jamii ya kimasai na wakulima au na mwekezaji. Watu wengi walipoteza maisha wakiwemo watoto na wakinamama, Watu walipoteza mali na hata makazi kwani kuna mengine yaliteketezwa kwa moto.


Hawa watu wameshindwa kupata sehemu za kudumu za kufuga. Hawa watu wamekua wakimbizi kila uchao katika nchi yao huru, kila siku kuna mapigano baina wafugaji na jamii inayo wazunguka. Wafugaji wanashindwa sasa kukaa na kufaidi mifugo yao na kuwasomesha watoto wao. Wafugaji wamekua ni kuhamahama kwani hawana sehemu maalum zilizotengwa kwa ajili ya ufugaji wao.


Uwekezaji wa wafugaji ni wa manufaa sana katika nchi yoyote ile. Wafugaji hunufaisha watu wengi hata wale ambao hawafugi pamoja na serikali yao.


Sasa kwa kizazi kinachokuja ya wafugaji vile wanaona kizazi iliyowatangulia wasulubiwa kila uchao wao watakua na hamu ya kufuga? Na kama hapana maanayake kama taifa tutakosa yatokanayo kwa mifugo. Badala ya kuimarisha uchumu wa taifa itakua inaporomoka kwani itatulazimu tuwe tunawaleta mifugo kutoka nje ya nchi kwa ajili ya matumizi ya kawaida mfano nyama na mengine mengi.


Serikali yetu haina budi kuangalia kwa upya namna ya kuboresha ufugaji. Hii itawezeka kwa kutengeneza sera nzuri na kutenga maeneo maalumu kwa ajili ya ufugaji. Serikali haina budi kuboresha miundo mindu ya wafugaji kama mabwawa, majosho n.k.

karibuni kwa mjadala!!!!
 
mkuu hili jambo huwa linanitatiza sana, kila mahali wafugaji wanapopaita makazi lazima wageuke wavamizi, hii dhana ya kuwanyima haki ya kuishi ya kikatiba sijui ni kwa faida ya nani
 
mkuu hili jambo huwa linanitatiza sana, kila mahali wafugaji wanapopaita makazi lazima wageuke wavamizi, hii dhana ya kuwanyima haki ya kuishi ya kikatiba sijui ni kwa faida ya nani

siku tukikosa watakao amua kufuga ndo tutajua umuhumu wao.... kuna vitu unajua umuhu wake pale inapokua hamna
 
wafugaji wanatumia uwezo wao wa kifedha kuhonga mamlaka mbalimbali za kiserikali hivyo kuwaonea wakulima.
 
wafugaji wanatumia uwezo wao wa kifedha kuhonga mamlaka mbalimbali za kiserikali hivyo kuwaonea wakulima.


mapigano yanayotokea ni kutokana kuhonga?... ingekua ni kuhonga ingekua wanahalalishiwa kumiliki maeneo husika. je kwenye hifadhi nayo wanaonga au
 
Haya ni matokeo mabaya ya sera mbovu katika umilikiji wa ardhi. Ikumbukwe kuwa hawa watu ni pastoralist, walikuwa na maeneo yao hayo ya kuchungia tangu zama hizo. Ongezeko la watu na makazi/mashamba yamewasogelea hawa jamaa na kuzuia mzunguko wao wa kulisha na kunywesha wanyama. Sababu hawajaandikishwa kama kijiji basi wanaonekana wao ni wavamizi. Natumaini serikali inajua kiini cha tatizo, ila sababu hawana majibu, basi itakuwa ngumu zaidi kupata ufumbuzi. Tutegemee ongezeko la kutofautiana na hata vita kati ya wakulima na wafigaji maana ni zaidi ya miaka ishirini sasa serikali imelifumbia macho (Morogor-Kilosa, Arusha, bonde la Usangu nk).
 
Haya ni matokeo mabaya ya sera mbovu katika umilikiji wa ardhi. Ikumbukwe kuwa hawa watu ni pastoralist, walikuwa na maeneo yao hayo ya kuchungia tangu zama hizo. Ongezeko la watu na makazi/mashamba yamewasogelea hawa jamaa na kuzuia mzunguko wao wa kulisha na kunywesha wanyama. Sababu hawajaandikishwa kama kijiji basi wanaonekana wao ni wavamizi. Natumaini serikali inajua kiini cha tatizo, ila sababu hawana majibu, basi itakuwa ngumu zaidi kupata ufumbuzi. Tutegemee ongezeko la kutofautiana na hata vita kati ya wakulima na wafigaji maana ni zaidi ya miaka ishirini sasa serikali imelifumbia macho (Morogor-Kilosa, Arusha, bonde la Usangu nk).



umenena kamanda.. That is all!! sijui hukuo tunakonda itakuaje asee...
 
Wadau hapa swala la msingi ni mabadiliko ya hali ya hewa inayowafanya wahame kuelekea maeneo mengine, mfano Jamii ya wasukuma inaongoza kwa kuwa na eneo kubwa Tanzania lakini bado wanahama, Longido hakulimiki, ni wafugaji tu lakini bado wanahama, Ngorongoro hawaruhusiwi kulima, ni kufuga tu lakini bado wanahama, kwa ujumla hali ya hewa ni changamoto, wanatakiwa wafuge kisasa na si vinginevyo. Lakini pia tujiulize kwanini pia wafugaji wa Burundi na Rwanda wanahamia Tanzania kufuga, utawaona Kigoma na Kagera
 
Tatizo ni kuwa idadi ya mifugo na wafugaji imekuwa kubwa mno kwa miaka ya karibuni baada ya jamii sa wafugaji hasa Wasukuma na Wamaasai walipo amua "kutanua" kutoka kwenye maeneo yao ya asili na kwenda sehemu zingine za nchi. Hii imeifanya mifugo kuzaliana sana hasa baada ya kuepuka kianganzi kwa kupata malisho mazuri na maji kule Ihefu, Kilombero, Kilosa n.k. Vilevile watu wazito serikalini wamewekeza sanakwenye mifugo nyuma ya mgongo wa wafugaji asili na kuwapa nguvu ya kiuchumi na mamlaka.
 
ni wakati wa kubadilika mambo ya kufuga kizamani makundi makubwa ya mifugo wakati ardhi haiongezeki . watu walime kisasa na kufuga kisasa baas


kisasa gani wewe unayosemea... kufuga ngombe wawali ndani ndo kisasa, mbona wanaolima wanalima mahekta na mahekita.. mi nahisi issue ni priority katika sera ya nchi yetu. mfano tukiwa tunafuga ng'ombe wachache vile tunashauriwa utawauza wangapi ili upate mahitaji mengine madhalan kusomesha na kuweka akiba na mambo mengine.

kufuga kundi kubwa ndo faida nayo inaoneka na kufanya mambo makubwa kama vile biashara kubwa ndo yenye return kubwa.
 
mkuu hili jambo huwa linanitatiza sana, kila mahali wafugaji wanapopaita makazi lazima wageuke wavamizi, hii dhana ya kuwanyima haki ya kuishi ya kikatiba sijui ni kwa faida ya nani
Wewe, Tanzania kuna wachungaji na sio wafugaji!
 
Serikali imepora maeneo ya wafugaji, wameyafanya kuwa hifadhi za taifa na kuwapa wawekezaji, wafugaji hawatambuliki na serikali ya Kikwete, cha msingi waunge mkono harakati za mabadiliko yanayoongozwa na Chadema, tuing'oe madarakani ccm, kisha tuweke utaratibu, kila mtu awe na maeneo ya kuendeshea shughuli zake, iwe kilimo, ufugaji, machinga nk, wakizingua tu na kuendelea kuishabikia ccm, hawatapata ufumbuzi, hii serikali ni corupt, tuungane watanzania wote kuisapoti Chadema, tuache kupoteza muda kuangalia vyama visivyo na nguvu kwa sasa, ambavyo ni mamruki wa ccm, watu kama kina Zitto wamejaa usaliti mwili mzima, hakuna tofauti kati ya zitto na mwigulu, kinyume na hapo hakuna ufumbuzi, Chadema ndio jibu pekee kwa kwa sasa, ndio maana ccm hawalali wakitafuta njia ya kuibomoa Chadema, kama tukishikamana, hawataweza, tutawang'oa tu, tumeanza na Mungu, tutamaliza na Mungu.
 
Wewe, Tanzania kuna wachungaji na sio wafugaji!


pamoja na kwabwa unafaidi mifugo unadiriki kusema wachungaji ndo wapo..., labda wewe haujui tofauti kati ya mchungi na mfugaji... au haujatembea katika maeneo yenye wafugaji ndo maana unaongea hivo...
 
pamoja na kwabwa unafaidi mifugo unadiriki kusema wachungaji ndo wapo..., labda wewe haujui tofauti kati ya mchungi na mfugaji... au haujatembea katika maeneo yenye wafugaji ndo maana unaongea hivo...
Tangu lini wafugaji wakatangatanga nchi nzima? hao ni wachungaji tu kwani wanyama wao hawana manufaa kwao wao wenyewe wala kwa jamii. Hivi mtu mwenye ng'ombe 3000 halafu hana nyumba zaidi ya manyata na wala hapeleki watoto shule, analalia ngozi badala ya godoro, anatibiwa kwa mitishamba, hana maji safi, josho wala matibabu ya wanyama wake unaweza kumuita mfugaji?
 
Haaaa unauliza waende wapi?, warudi na wabaki huko huko walikotoka. Yaani wameharibu mazingira yao halafu wahamie kwa wengine. Swala la kuwa ni Pastoralism halina mshiko. Kwani wanatakiwa kuzunguka huko huko, Mmasai kwenda Mtwara au Msukuma kuhamia Morogoro wapi na wapi. Mikoa hiyo ni ya wakulima na mikoa yao ni ya wafugaji. Swala la Utanzani sio sababu hata kama katiba inaruhusu, hivi wanataka Tanzania nzima wajae wao?

Nawasapoti wote waliopinga wazo la mtoa mada.
1. Nchi haiongezeki bali mifugo inaongezeka, ni wakati muafaka hawa mnaowaita wafugaji lakini ni wachungaji wapunguze mifugo yao na kutumia njia bora za ufugaji kulingana na ardhi zao za asili. Kimsingi hawa wachungaji wanaona ufahari kuwa na ng'ombe wengi ambao hawapati maendeleo yo yote kiuchumi matokeo yake ni maeneo yao ya kuchungia yanakuwa madogo na kuhamia maeneo mengine ambapo wanafanya uharibifu mkubwa.
2. Wakati wachungaji wanaongezeka pamoja na ng'ombe wao wananchi wakulima nao wanaongezeka. Wakulima hawawezi kuhama hama maana maeneo yao ni ya kudumu, hawa wachungaji hakuna mwenye eneo. Ikiwa kila mchungaji atagawiwa eneo lake na kupewa hati miliki hakuna atakayethubutu kuongeza mifugo wala kuhamahama, na hapo amani itapatikana.
3. Ni kweli Tanzania inaongoza kwa kuwa na idadi kubwa ya mifugo katika bara la Afrika, je mchango wao katika uchumi ni kiasi gani? ilitakiwa tuwe tunaongoza katika mauzo ya nyama na maziwa nchi za nje. Ufugaji wate hauna tija wafugaji wabadilike.
 
pamoja na kwabwa unafaidi mifugo unadiriki kusema wachungaji ndo wapo..., labda wewe haujui tofauti kati ya mchungi na mfugaji... au haujatembea katika maeneo yenye wafugaji ndo maana unaongea hivo...

Hata ukukataa hao ni wachungaji tu. Wafugaji wana ranchi au maeneo maalum ya kufugia sio kuhamahama..
 
Tuachane na hii culture ya kufuga ng'ombe kwa kuchunga kwa kuwa inasababisha mamilioni ya watoto Tanzania wasiende shule kwa mwaka, ukienda usukumani na umasaini utaona watoto wenye umri wa kwenda shule wanachunga mwaka mzima badala ya kwenda shule , ndiyo maana jamii za kifugaji zinaongoza kwa ujinga
 
Haya ni matokeo mabaya ya sera mbovu katika umilikiji wa ardhi. Ikumbukwe kuwa hawa watu ni pastoralist, walikuwa na maeneo yao hayo ya kuchungia tangu zama hizo. Ongezeko la watu na makazi/mashamba yamewasogelea hawa jamaa na kuzuia mzunguko wao wa kulisha na kunywesha wanyama. Sababu hawajaandikishwa kama kijiji basi wanaonekana wao ni wavamizi. Natumaini serikali inajua kiini cha tatizo, ila sababu hawana majibu, basi itakuwa ngumu zaidi kupata ufumbuzi. Tutegemee ongezeko la kutofautiana na hata vita kati ya wakulima na wafigaji maana ni zaidi ya miaka ishirini sasa serikali imelifumbia macho (Morogor-Kilosa, Arusha, bonde la Usangu nk).
Hibi unaongea kwa data au unajaribu kujifurahisha. Wagugaji ndiyo kundi linalozaliana kwa wingi na hovyo tembelea makabila ya wafugaji uone walivyozaliana unakuta mwanaume 1 anawawake 2 hadi 4 au 5 na hao wanawake wanazaa watoto kati ya 4hdi 8 haya fikiria kama mwanaume 1 akiwa na watoto kianzia 18 hadi Hata 30 hafu awagawie ng'ombe nao wajitegemee unadhani baada ya miaka 10 na kuendelea huoni wafugaji watakuwa mara2 ya wale wa awali? maeneo watayatoa wapi? wakati nakua kuna mikoa haikuwa hata na ng'ombe nchii kutokana na ndorobo lakini leo ng'ombe wamejaa hadi mikoa ya Mtwara na Lindi, Mbeya, Rukwa na Katavi hakukuwa na wagugaji leo wamejaa kutoka mikoa ya shinyanga, Arusha na Manyara na Dodoma.
Angalia hata ktk sensa zote mikoa ile ya wafugaji ndiyo inaidadi kubwa ya watu, na ng'ombe nao wameongezeka zaidi ili kuendana na idadi ya wafugaji
Wakulima hawazaliani hovyo kama wafugaji. Nadhani umenielewa.
 
Olee, nadhani kwa jina lako wewe ni mmasai, ebu niambie ni wa jinsi gani watoto wa kimasai wanashindwa kwenda shule kwa sababu ya kuchunga?
 
Back
Top Bottom