1-Kuwapa maeneo ya kudumu maana yake unaunga mkono hoja watoto wasiende shule, mimi ninavyojua kila nyumba ya Kimaasai angalau watoto 4 hawaendi shule kabisa wanachunga tu hasa wa kiume, ndiyo maana wasichana wa kimasaai angalau wamesoma kuliko wavulana kwa kuwa wao hawachungi sana
2. Pia swala la kuwawekea Ranchi kila familia haitekelezeki, usukumani kwa mfano wana maeneo ya kuchungia lakini bado wanahama, mfano Meatu wana eneo kubwa lisilolimika, pia mbona Longido wameachiwa wachunge lakini bado wamehama?, Ngorongoro pia mbona bado kuna shida?. Najua kuwaamasisha watu wafuge ni kudumaza elimu lakini kama ikiwezekana watengewe maeneo yao tuone wanaishia wapi.
Mr Olee, hapa swala la msingi tupambane kila jamii ielimike ili watu waweze kufuga mifugo michache yenye tija, vinginevyo hii ishu ni ngumu kwa kuwa wanaofuga ndiyo haohao wanapenda kulima mfano wasukuma.