Wafuasi CHADEMA wampopoa mawe OCD wa MUSOMA MJINI

Magesi

JF-Expert Member
Jul 10, 2012
2,587
573
Katika kile kinachoonekana ni kuchoshwa na uonevu wa jeshi la polisi dhidi ya CHADEMA, wafuasi wa CHADEMA wamempiga mawe OCD wa MUSOMA MJINI baada ya kutaka kuwakamata.

Nitawaletea taarifa zaidi.

Nawasilisha.Mwenyekiti wa jumuiya ya wazazi ccm taifa ndg Abdala Bulembo alikua na mkutano wa hadhara leo ndio ukafika wakati wa maswali na majibu mwananchi mmoja alitaka ufafanuzi juu ya fedha zilizofichwa uswis yeye akaanza kumkashifu Mh.ZITO kuwa alikuwa anatafuta umaarufu wa kisiasa wala hamna fedha zilizofichwa uswiss pamoja na kumkashifu Mbunge wa Musoma Mjini Mh. Nyerere ndipo watu walianza kuzomea hali iliyofanya Asikari kuanza kufyatua risasi ovyo na kuwakamata baadh ya wananchi hali iliyopelekea fujo kubwa kuzuka ndipo OCD alipoingilia kati na aliyekuwa mbunge wa zamani ndg Mathayo ndipo waliposhambuliwa kwa mawe na wananchi na mkutano kuvunjika nawengine wamepelekwa kituo cha polisi.
 
Back
Top Bottom