Wafanyakazi wa Dar Serena, NMB na Montage na siku ya mtoto wa Afrika Dogodogo Centre Bunju

Mtambuzi

Platinum Member
Oct 29, 2008
8,809
15,419
13445412_1009811035739939_3978690068052616944_n.jpg


13445685_1009861565734886_223426465920485181_n.jpg


View attachment 357161

13466219_1009862269068149_4890474392327128488_n.jpg


Wafanyakazi wa Dar Serena Hoteli, NMB na Montage kwa pamoja walisherehekea siku ya mtoto wa Afrika leo tarehe 16/6/2016 kwa kutembelea kituo cha Dogodogo Centre Bunju ambacho hutoa elimu ya ufundi kwa watoto wanaoishi katika mazingira magumu au hatarishi.

Katika hafla hiyo walitoa misaada mbalimbali kwa watoto hao pamoja na kushiriki zoezi la kupaka rangi sehemu ya kulia chakula ya kituo hicho.

Wakizungumza karika Hafla hiyo wawakilishi wa kampuni hizo yaani Dar Serena Hotel ikiwakilishwa na Mkurugenzi wa Masoko ndugu Seraphin Lusala na Meneja wa mafunzo Bi Rhoda Kitila, NMB ikiwakilishwa na Madam Elizabeth na Elice Wangwe na Montage ikiwakilishwa na Madam Tedi Mapunda waliitaka jamii na taasisi mbalimbali kusaidia kituo hicho ambacho kinakabiliwa na ukata wa fedha za kuendeshea mafunzo ya ufundi kwa kutoa tenda za samani na ushonaji wa sare ili kukijengea uwezo kijiendeshe kibiashara kwani wana fani za ushonaji na ufundi seremala pamoja na fani nyingine mbalimbali.
 
Iko sawa,watoto raha yao ni kupiga msosi mzuri sio unawaletea tu stori ndeeeefu za soweto.
 
Hvi hiki kituo ni cha mtu binafsi shirika au taasisi? maana vile walivyojenga hayo majengo na vifaa vya nafunzo walivyo navyo hata chuo cha veta kinachohudumiwa na serikali hakifikii kituo hiki
 
Back
Top Bottom