Wafanyakazi TRA wanahujumu mapato

Wafanyakazi TRA wanahujumu mapato

Noti mpya tz

JF-Expert Member
Joined
Mar 23, 2011
Posts
974
Reaction score
247
Imenitokea mwenyewe live leo kwenye ofisi za TRA makao makuu ya mkoa wa Arusha.

Ni hivi, mwaka juzi nilijiandikisha kama mlipa kodi mkoani mwanza na lengo langu kuu ilikuwa ni kupata TIN namba ili nikate leseni ya kuendesha magari, bahati mbaya nikapata safari nje ya nchi kabla sijapata tin namba ikabidi niahirishe zoezi la leseni niwahi mbele.

Niliporudi mwaka jana makao yangu kwa muda yakawa Singida na ikabidi nikatie huko leseni yangu. Walitafuta jina kwenye system yao wakalipata hivyo nikafanya process nikapata leseni.

Miezi miwili iliyopita nilianzisha kibiashara changu hapa Arusha, kimeendelea baadae nikajiambia mwenyewe kuwa ni vizuri kukata leseni ya biashara kwani sipendi vitu bubu, leo nimeamka nikaenda tra nikakutana na dada mmoja akanielekeza nipande ghorofani nikamuone mama mmoja anaitwa mama KESSY.

Ngodongodo huyo kwa mama kessy, nikajieleza kila kitu na nikauliza uwezekano wa kutumia TIN namba yangu niliyoikata mwanza ili nikate leseni ya biashara na mambo mengine.

La haula, Mama kessy akaniambia ni lazima niende mwanza kwanza kwenye ofisi za TRA halafu ndiyo nije kukata leseni. Nikauliza namba yangu si iko kwenye system kwanini nisifanyiwe process nikalipa hapa arusha? Mama akasema nisimfundishe kazi ni lazima niende mwanza.Nini kunanipeleka mwanza?

Ni kwamba, Nilipokata tin namba sikupewa certificate ya TIN namba so ni lazima niende mwanza wakaniprintie ile certificate ndipo nije arusha kulipa kodi.

Mimi si mtaalam wa tra, inawezekana taratibu ndivyo zilivyo. Shwaki langu ni hiki.Kwani hakujipa muda kunipa maelezo ya kutosha ni kwanini napaswa kwenda mwanza?

Je, ni kweli kwamba tin namba certificate haiwezi kuprintiwa sehemu nyingie? Na je, siwezi kulipa leseni kwa kutumia tin namba yangu inayoonekana kwenye system ya tra kama nilivyofanya singida wakati wa kukata leseni?

Swali la mwisho, Ni wananchi wangapi wenye moyo wa kulipa ushuru wamekatishwa tamaa na wafanyakazi wa TRA?

Nisaidieni
 
Umeongea jambo la muhimu sana, ila baada ya kukukatalia ungeomba kukutana na TRA Regional mangaer au ungeuliza reception nani yuko top ya mama Kessy kimadaraka uonane naye na umuelezee suala lako kama iliwezekana Singida kwanini hapo ishindikane na TRA system wanayotumia ni ileile!
 
Hongera kwa kuwa raia mwema anaeipenda nchi yake, usiwe kama hao wanaoiibia serikal huku wakiubiri uzalendo. Well, nadhani bado swala lako laweza tatuliwa hapo hapo arusha onana na senior officers kabla ya kupoteza muda kwenda mwanza
 
pole sana mkuu. wahujumu uchumi wako wengi. huyo mama ashitakiwe kwa kutaka kuinyima serikali mapato

Watumishi wa Tra wanajisahau na kujiona kama miungu mtu hapa Tanzania.
 
Hongera kwa kuwa raia mwema anaeipenda nchi yake, usiwe kama hao wanaoiibia serikal huku wakiubiri uzalendo. Well, nadhani bado swala lako laweza tatuliwa hapo hapo arusha onana na senior officers kabla ya kupoteza muda kwenda mwanza

Hiyo yote ni kuandaa mazingira ya kukubana utoe rushwa,pole sana
 
Kama wamekataa, rudi kafanye biashara zako.
 
..... Mama kessy akaniambia ni lazima niende mwanza kwanza kwenye ofisi za TRA halafu ndiyo nije kukata leseni. Nikauliza namba yangu si iko kwenye system kwanini nisifanyiwe process nikalipa hapa arusha? Mama akasema nisimfundishe kazi ni lazima niende mwanza.Nini kunanipeleka mwanza????Ni kwamba..... Nilipokata tin namba sikupewa certificate ya tin namba so ni lazima niende mwanza wakaniprintie ile certificate ndipo nije arusha kulipa kodi.

Pole ndugu yangu,
pia yamekuta, Nipo MKOA X nilinunu gari la biashara nikalipeleka Mkoa Y na TIN yangu ni ya MKOA X, sasa basi wakati umefika natakiwa nilipie kodi ya mapato, nimeshindwa kulipia kule Y na sasa certificate inatakiwa irudi X na ndio nilipie Mapato.

Hakika nchii hii ni majanga.
 
Hawa akina mama kessy hawa nanatugharimu sana kama taifa.
 
Sasa kila kitu kama kiko kwenye system za TRA tatizo ni nini!? Jaribu kuwaona wa juu yake huyo Mama Kessy ili wakusaidie.
 
Imenitokea mwenyewe live leo kwenye ofisi za TRA makao makuu ya mkoa wa Arusha.Ni hivi, mwaka juzi nilijiandikisha kama mlipa kodi mkoani mwanza na lengo langu kuu ilikuwa ni kupata TIN namba ili nikate leseni ya kuendesha magari, bahati mbaya nikapata safari nje ya nchi kabla sijapata tin namba ikabidi niahirishe zoezi la leseni niwahi mbele. Niliporudi mwaka jana makao yangu kwa muda yakawa Singida na ikabidi nikatie huko leseni yangu. Walitafuta jina kwenye system yao wakalipata hivyo nikafanya process nikapata leseni.Miezi miwili iliyopita nilianzisha kibiashara changu hapa Arusha, kimeendelea baadae nikajiambia mwenyewe kuwa ni vizuri kukata leseni ya biashara kwani sipendi vitu bubu, leo nimeamka nikaenda tra nikakutana na dada mmoja akanielekeza nipande ghorofani nikamuone mama mmoja anaitwa mama KESSY. Ngodongodo huyo kwa mama kessy, nikajieleza kila kitu na nikauliza uwezekano wa kutumia TIN namba yangu niliyoikata mwanza ili nikate leseni ya biashara na mambo mengine.La haula,..... Mama kessy akaniambia ni lazima niende mwanza kwanza kwenye ofisi za TRA halafu ndiyo nije kukata leseni. Nikauliza namba yangu si iko kwenye system kwanini nisifanyiwe process nikalipa hapa arusha? Mama akasema nisimfundishe kazi ni lazima niende mwanza.Nini kunanipeleka mwanza????Ni kwamba..... Nilipokata tin namba sikupewa certificate ya tin namba so ni lazima niende mwanza wakaniprintie ile certificate ndipo nije arusha kulipa kodi.Mimi si mtaalam wa tra, inawezekana taratibu ndivyo zilivyo. Shwaki langu ni hiki.... Kwani hakujipa muda kunipa maelezo ya kutosha ni kwanini napaswa kwenda mwanza? Je, ni kweli kwamba tin namba certificate haiwezi kuprintiwa sehemu nyingie? Na je, siwezi kulipa leseni kwa kutumia tin namba yangu inayoonekana kwenye system ya tra kama nilivyofanya singida wakati wa kukata leseni?Swali la mwisho..... Ni wananchi wangapi wenye moyo wa kulipa ushuru wamekatishwa tamaa na wafanya kazi wa tra?Nisaidieni Noti

unajua mkuu nchi ishauzwa hii sema tu hatumjui mnunuzi wetu ni nani,so tunajitahidi tuchukue marupurupu mapema kabla ya mwenye mali hajaja ku claim chake.

usilaumu sana kaka hata ungekuwa wewe ndo umepata hiyo nafasi ungechukua miposho yako mapema kabla ya muda.ngoja nimpigie swahiba wangu mama kessy,coz cwez kukosa chupa mbili tatu coz ofisi hii nilipo haichanganyii kivile
 
viongozi wote wangemuiga jk kujiunga jamii forum wangesoma hizi comment na kuzifanyia kazi haraka. JK umetisha!!!
 
Pole ndugu yangu,
pia yamekuta, Nipo MKOA X nilinunu gari la biashara nikalipeleka Mkoa Y na TIN yangu ni ya MKOA X, sasa basi wakati umefika natakiwa nilipie kodi ya mapato, nimeshindwa kulipia kule Y na sasa certificate inatakiwa irudi X na ndio nilipie Mapato.
Hakika nchii hii ni majanga.

Unalipa popote Mkuu mradi waoneshe hiyo namba ya TIN
km ni Road Licence au Leseni ya udreva wape Namba za TIN zaidi ya hapo ni ngumu kutafuta kwa majina au manual kwa sababu majina hayajakaa Kimkoa au Wilaya yapo kitaifa kwa Walipa Kodi wote
 
Kama wamekataa, rudi kafanye biashara zako.
kweli kabisa kwanini Noti mpya tz usirudi ukaendelee na kazi / biashara zako
kwani km upo makini utembee na hizo Tax Identification Number
Kwani wana mpango wa kuziingiza kweny simu za mitandao yetu na hapo sisi wakwepaji mtatuponza tutaanza kukatwa hadi Vocha
 
kweli kabisa kwanini Noti mpya tz usirudi ukaendelee na kazi / biashara zako
kwani km upo makini utembee na hizo Tax Identification Number
Kwani wana mpango wa kuziingiza kweny simu za mitandao yetu na hapo sisi wakwepaji mtatuponza tutaanza kukatwa hadi Vocha

Hao tra wahuni. Wakikukamata barabarani hujalipa kodi watakuachia msiba mkubwa.
 
Umeongea jambo la muhimu sana, ila baada ya kukukatalia ungeomba kukutana na TRA Regional mangaer au ungeuliza reception nani yuko top ya mama Kessy kimadaraka uonane naye na umuelezee suala lako kama iliwezekana Singida kwanini hapo ishindikane na TRA system wanayotumia ni ileile!

Napinga 100% huu utamaduni wakukimbiza hata vitu vidogo kama hivi kwa managers.

Lazima mashirika na serikali iweke mikakati ya kuwa adabisha hawa watumishi wanaoleta usumbufu usio na maana, hapo kwa kifupi huyo Mama angeweza kumsaidia kama asingekuwa na nia ya kutaka rushwa. Ingekuwa mimi ningeenda mbali na kumshtaki kwa kuomba rushwa.
 
Umeongea jambo la muhimu sana, ila baada ya kukukatalia ungeomba kukutana na TRA Regional mangaer au ungeuliza reception nani yuko top ya mama Kessy kimadaraka uonane naye na umuelezee suala lako kama iliwezekana Singida kwanini hapo ishindikane na TRA system wanayotumia ni ileile!
Ushauri mzuri... Ahsante sana.
 
Back
Top Bottom