Wafanyabiashara kuweni na utu

bakundande jr

JF-Expert Member
Oct 22, 2021
507
670
Moja kwa moja kwenye mada.

Kutokana na sababu tofauti kumekuwa na panda shuka ya bei ya bidhaa tofauti kuanzia vinywaji hata vyakula.

Kitu cha kushangaza ni kuwa wafanyabiashara wanakuwa wepesi kubadilisha bei ya bidhaa pale wanaposikia bidhaa hiyo imepanda bei hata kama ndio ametoka kununua bidhaa hiyo kwa bei chee jana yake ila imekuwa tofauti pale ambapo bidhaa hushuka bei.

Kwa mfano upande wa vinywaji hususani soda imepita kama wiki naona matangazo na mabango ya kampuni flani kushusha bei ya vinywaji vyake ila kila nikienda kununua bidhaa hizo nakuta bei ni ile ile. Kitu cha kushangaza zaidi ni kuwa kwenye duka hilo hilo unaweza kuta bango ambalo lina onesha kushuka kwa bei ya bidhaa husika.

Sasa kama bado mnakuwa na mzigo mkubwa kwanini msikatae kuweka hayo matangazo?
 
Fungua biashara ili uwe unapunguza bei
Moja kwa moja kwenye mada.

Kutokana na sababu tofauti kumekuwa na panda shuka ya bei ya bidhaa tofauti kuanzia vinywaji hata vyakula.

Kitu cha kushangaza ni kuwa wafanyabiashara wanakuwa wepesi kubadilisha bei ya bidhaa pale wanaposikia bidhaa hiyo imepanda bei hata kama ndio ametoka kununua bidhaa hiyo kwa bei chee jana yake ila imekuwa tofauti pale ambapo bidhaa hushuka bei.

Kwa mfano upande wa vinywaji hususani soda imepita kama wiki naona matangazo na mabango ya kampuni flani kushusha bei ya vinywaji vyake ila kila nikienda kununua bidhaa hizo nakuta bei ni ile ile. Kitu cha kushangaza zaidi ni kuwa kwenye duka hilo hilo unaweza kuta bango ambalo lina onesha kushuka kwa bei ya bidhaa husika.

Sasa kama bado mnakuwa na mzigo mkubwa kwanini msikatae kuweka hayo matangazo?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Lengo la mtu kuweka pesa yake kwenye fremu ni kupata hela ndugu
Tatizo la wateja wengine wanataka wafanye mahesabu ya faida yako wakupangie eti faida ya mia moja inatosha nyingine yote ya nini..
Hajui kwamba kufuata mzigo ni gharama pia Kodi inahitajika tofauti na kwamba pia unakuza biashara yako
 
Siku ukifanya nawe biashara utapata jibu sahihi kwanini wanafanya hivyo
 
Lengo la mtu kuweka pesa yake kwenye fremu ni kupata hela ndugu
Tatizo la wateja wengine wanataka wafanye mahesabu ya faida yako wakupangie eti faida ya mia moja inatosha nyingine yote ya nini..
Hajui kwamba kufuata mzigo ni gharama pia Kodi inahitajika tofauti na kwamba pia unakuza biashara yako
Mkuu hapo kwenye suala la faida sipongi ila ni kwanini uweke tangazo lenye bei tofauti na bei unayouza???

If unauza 1000 acha ikae hivo sio kusema unauza 500 wakati unauza 800
 
Back
Top Bottom