Wafahamu Marais wa Afrika wasio na shahada za Vyuo Vikuu

MUGASHA THE HERO

JF-Expert Member
Mar 22, 2016
327
205
  1. Muhammadu Buhari wa Nigeria
Alisoma Shule ya msingi Daura na Mai’adua huko Katsina State, Nigeria Kaskazini. Na kisha kujiunga na shule ya Katsina Model mwaka 1953, na badae sekondani ya kitongoji cha Katsina ambayo kwa sasa ni chuo cha serikali mwaka 1956 – 1961.

muhammadu1.jpg


2. Dennis Sassou Nguesso wa Jamhuri ya Congo

Alipokea mafunzo yake katika chuo cha Ualimu, Dolisie Nairi. ameendesha nchi kuanzia enzi za Brazzaville mwezi oktoba 1997.

Denis-Sassou-NGuesso.png


3. Isaias Afwerki wa Eritrea
Licha ya kwamba hakumaliza masomo yake ya Sekondari, Rais wa Eritrea Isaias Afwerki anaongoza vizuri tu nchi yake. Japo katika rekodi nyingi inaonekana alitunukiwa cheti kutoka shule ya Prince Makonnen lakini hakuweza kusoma masomo ya Chuo kwasababu hakupata alama za kutosha na baadae akajiunga na kuwa mwanaharakati wa kuikomboa Eritrea

President-Isaias-Afwerki-interview-2.jpg


4. Paul Kagame wa Rwanda.
Rais Kagame alianza shule ya msingi karibu kabisa na kambi ya wakimbizi alipofunzwa Kiingereza na utamaduni wa Kiganda. Na alipofiwa na Baba yake miaka ya 70, maendeleo yake shuleni yakadhoofika. Na katika harakati za yeye kupenda siasa aliishia kuahirishiwa masomo yake na kumaliza tofauti na wenzie katika shule ya sekondari ya zamani ya Kampla.

president-paul-kagame-7.jpg
 
Naona haya ni maandalizi ya kumuandaa Freeman Mbowe kuwa Mgombea Urais wa CHADEMA. Ila mkumbuke kuwa Katiba ya nchi inataka Mgombea Urais sharti awe na Angalau Shahada ya kwanza
 
Back
Top Bottom