MO11
JF-Expert Member
- Mar 23, 2014
- 19,553
- 41,467
House girl alitandika kitanda cha
bosi wake Kama Sehemu ya
jukumu lake la kila siku.
Alipomaliza akakitazama sana kile
kitanda cha bosi wake akasema
naweza kufa bure bila ya kulalia
kitanda kama hiki. Akasema ngoja
nijaribu kulala angalau kidogo.
Akavua nguo zote akaziweka chini,
akabaki na gagulo tu akawasha AC
akajifunika brangeti gubigubi
akalala. Kwa bahati mbaya usingizi
ukampitia kweli akalala fofofo.
Ghafla Mume wa bosi akarudi na
haikuwa kawaida yake kurudi Muda
huo. Alipoingia chumbani, akajua
hakika huyu ni mke wangu na kwa
kuwa jana tulikwaruzana atakuwa
amekasirika tu. Akaogopa
kumwamsha. Mwanamme
akasaula, akabaki na msuli naye
akajifunika hilo hilo blanketi kwa
taratibu sana kwa hofu ya
kumwamsha mke wake. Kwa
bahati mbaya naye usingizi
ukampitia, akalala fofofo .
Mkewe aliporudi, akaingia
chumbani, akakuta watu wawili
wamelala fofofo. Akafunua
blanketi kwa nguvu, akawakuta
wote wawili; yaani yule mfanyakazi
na mume wake wamelala pamoja.
Walipoulizwa kila mtu akaeleza
ukweli wake.
1. Je, kama wewe ungekuwa ndiyo
yule mke wa bosi ungewaelewa?
2. Je, kama wewe ungekuwa ndiyo
yule mfanyakazi ungejitetea vipi?
3. Je, Wewe ungekuwa ndiyo yule
bosi ungejitetea vipi?
4. Je hapo ugomvi utakuwa
umesababishwa na nani? Mke,
mume au mfanyakazi?
bosi wake Kama Sehemu ya
jukumu lake la kila siku.
Alipomaliza akakitazama sana kile
kitanda cha bosi wake akasema
naweza kufa bure bila ya kulalia
kitanda kama hiki. Akasema ngoja
nijaribu kulala angalau kidogo.
Akavua nguo zote akaziweka chini,
akabaki na gagulo tu akawasha AC
akajifunika brangeti gubigubi
akalala. Kwa bahati mbaya usingizi
ukampitia kweli akalala fofofo.
Ghafla Mume wa bosi akarudi na
haikuwa kawaida yake kurudi Muda
huo. Alipoingia chumbani, akajua
hakika huyu ni mke wangu na kwa
kuwa jana tulikwaruzana atakuwa
amekasirika tu. Akaogopa
kumwamsha. Mwanamme
akasaula, akabaki na msuli naye
akajifunika hilo hilo blanketi kwa
taratibu sana kwa hofu ya
kumwamsha mke wake. Kwa
bahati mbaya naye usingizi
ukampitia, akalala fofofo .
Mkewe aliporudi, akaingia
chumbani, akakuta watu wawili
wamelala fofofo. Akafunua
blanketi kwa nguvu, akawakuta
wote wawili; yaani yule mfanyakazi
na mume wake wamelala pamoja.
Walipoulizwa kila mtu akaeleza
ukweli wake.
1. Je, kama wewe ungekuwa ndiyo
yule mke wa bosi ungewaelewa?
2. Je, kama wewe ungekuwa ndiyo
yule mfanyakazi ungejitetea vipi?
3. Je, Wewe ungekuwa ndiyo yule
bosi ungejitetea vipi?
4. Je hapo ugomvi utakuwa
umesababishwa na nani? Mke,
mume au mfanyakazi?