Wadau naombeni maelezo kuhusu eggs incubater

Wadau naombeni maelezo kuhusu eggs incubater

FORCE NAMBA

JF-Expert Member
Joined
Aug 19, 2014
Posts
937
Reaction score
328
Wadau wenye uelewa tafadhari naomba kujua bei ya eggs incubator na jinsi ya kuitumia.Nahitaji kuanza ufugaji kuku.Mashine iwe na uwezo wa kutotolesha Mayai 50-100
.Picha ni muhimu
 
Watakuja wenye nazo maana humu hawakosekani. Usikae mbali Na jukwaa hili
 
Nafikiri andiko lako linakosa nguvu,ungejitahidi kuwa specific juu ya kile unachohitaji kufahamishwa.Kwa mfano labda bei,brand gani ni zuri zaidi kwenye ufanisi,lakini pia ninavyofahamu mimi hizi mashine zipo tunazotengeneza wenyewe hapa nyumbani lakini pia tuna ambazo tunaagiza kutoka nje.

Pia zipo ambazo ni automatic na nyingine ni mannual na hasa kwa hizi ambazo tunazitengeneza wenyewe.Nafikiri hapa kwa upande wa mashine nitakua nime cover kwa baadhi ya maeneo.

Baada ya hapo utahitaji kufahamishwa namna ya uendeshaji wake.Mfano mayai yakuwekwa kwenye mashine yanatakiwa yawe yametagwa ndani ya wiki moja,Lakini pia uhifadhi wa haya mayai huwa yananamna yake yakuhifadhi ile ncha ya yai inatizama juu kwa kawaida.Lakini pia ni vema ukawa na standby generator kwani umeme wetu haina uhakika.

Kwa anayefahamu vizuri basi atakufahamisha vizuri hasa kwenye nyanja hizo.
 
Nauza vifaranga chotara,pm kwa kuweka oda yako,bei 1500 kwa kifaranga wa siku moja.
 
Back
Top Bottom