benteke
JF-Expert Member
- Apr 3, 2014
- 1,305
- 1,066
Kha..! yaani nadamka mpaka najishtukia...najikuta nimeshavaa kila kitu nikitaka kutoka naona giza nje..nakumbuka kuangalia saa..eti ndo saa kumi na moja kasorobo. Inabidi nirudi nikae nizuge kidogo angalau nitoke saa kumi na moja na robo hivi.Nafika ofisini nafikiri nimewai naangalia parking nakuta kuna wenzangu wanne washafika, nachoka kabisa. Yaani haya mateso yoote ya kudamka alfajiri na kuwai ofisini ni kwa sababu ya kuflirt kidogo na hawa warembo kabla mda wa kazi...tuko wengi hata wazee wapo pia .....ni raha sana. Wadada wazuri hasanteni sana mnatuliwaza na kututoa stress kabla ya kazi...Sizungumzii uzuri wa umbo na sura tu, hata wa moyoni pia... unaweza kuwa mzuri wa umbo ukawa na roho mbaya, ni mwiba ofisini. Tunawapenda wadada endeleni na moyo huo, maana mnatufanya tunaipenda kazi hata kama mshara ni mdogo.