Kula'ela,yaani kutumia pesa kwa ajili ya kujiburudisha,ni lazima uwe na mwanamke. Kula pesa bila mwanamke ni sawa na kula ugali bila mboga.
Hivi! Inaingia akilini kweli uende bar uanze kuagiza mipombe, uyanywe mwenyewe,mwanzo mwisho bila kuwa na mwanamke! Hitimisho la furaha yako ni usingizi yaani ukalale umwene?
Maradhi ya msongo wa mawazo unayakaribisha wewe kwa sababu ya ubinafsi.
Ukimhonga mwanamke,linapokuja suala la mapenzi,utafanya kwa kujiamini sana,kwa sababu una dhamana ya fedha zako. Utajituma hadi utajiogopa! Lakini ingia kichwa kichwa hauna hata chapa uone!
Ukiambiwa 'kaka nisaidie nauli ya daladala' utatachechetuka adi utajidharau. Maana kutunga uongo napo ni kazi'ujue!
Nani alikuambia kuhonga mwanamke kwa ajili ya kulainisha penzi kunaubaya? Ee bw eeh tusipotoshane, me nikipata mlupo nahonga.