Kwanza tukubaliane kitu kimoja, kuwa kifo kwa mwanadamu hakiepukiki. Kila nafsi itaonja mauti, maandiko yanasema. Hata hivyo kwa muda mrefu mwanadamu amekuwa akijibiidisha kukwepa kifo, ndio maana tunaenda hospitali au tunakunywa dawa.
kwa post yko hapo juu, ni kweli kifo kinaweza kucheleweshwa lakini ipo siku tu mtu lazima afe. Hata hivyo kuna watu wamejitokeza kuwadanganya wengine kuwa wanaweza kuzuia kufa kwa maombi peke yake. Kweli wapo wanamaombi wenye uwezo huo lakini wengi ni waongo. wanafanya kila wanalofanya kwa malengo yao binafsi na si kwa ajili ya utukufu wa Mungu.Kila jambo linalofanywa kwa maslai binafsi na si kwa ajili ya utukufu wa Mungu ni sawa na ushetani.
Mungu analengo kwa kila jambo, tuwe tayari kukabiliana na malengo ya Mungu ambayo hayatupendezi katika nafsi zetu ikiwemo kifo.