KAKA A TAIFA
JF-Expert Member
- Apr 27, 2011
- 566
- 80
Mimi hainiingii akilini kwanini hatulindi pesa zetu za kigeni.najiuliza iweje rahisi mtu yeyote kununua pesa za kigeni kwenye maduka husika bila kuwepo na chombo cha udhibiti.tunawezaje kujua mtu fulani kanunua pesa za kigeni kiasi gani?na atazitumiaje/anzipeleka wapi?mkulima anlima mazao yake kwa tabu kubwa iwe pamba ,kahawa,chai,karafuu, vyanzo vingine kama mifugo,mazao ya misitu,bahari nk.tunauza tunapata hela za kigeni.sasa matumizi mfanya biashara ananunua pesa za kigeni anakwenda china kununua mapambo ya plastic,viatu ambavyo ukivivaa asubuhi ,jioni tu tayari vimeshachanika.jamani haya si matumizi mabaya ambayo hayana udhibiti kabisaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaaa.nisaidieni na nyie kama hii ni sawa?