KAMPUNI ya China Railway Constraction Engeering Group kwa kushirikiana na Kampuni ya China Bridge imeshinda zabuni ya ujenzi wa daraja la Kigamboni ambapo ujenzi huo utachukua miaka mitatu kukamilika.
Mkataba wa ujenzi wa daraja hilo ulisainiwa jana na mwakilishi wa kampuni ya hiyo, Shi Yiqian, na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jami (NSSF), Dk. Ramadhan Dau.
Akizungumzia ujenzi huo, Dau alisema kuwa ndoto imetimia ambapo kazi iliyobaki ni utekelezaji kwa kampuni hiyo kuanza kujenga.
Alisema kuwa shirika limehangaika sana katika kufanya kazi kutafuta mkandarasi mshauri wa mradi huo ambapo limechukua kipindi kirefu hadi kufikia kumpata.
Dau alisema katika ujenzi huo NSSF inatoa asilimia 60 ya mradi mzima na serikali itatoa asilimia 40 ambapo mradi mzima utagharimu sh 214, 630,40,000. Naye, Waziri wa Ujenzi, Dk. John Magufuli, alimtaka mkandarasi kufanya kazi kwa nguvu ili ujenzi wa daraja hilo uwe umekamilika ndani ya miezi 36.
Dk. Magufuli alisema katika ujenzi huo hakuhitajiki siasa kutokana na Watanzania kuchoshwa na mambo hayo badala yake watu wanataka daraja kwa ajili ya shughuli zao za maendeleo.
Alisema kuwa kuendekeza siasa kutawafikisha pabaya Watanzania na kukosekana kwa maendeleo na kuacha kutumia fursa zilizopo.
Watu wamechoka na siasa zisizo za vitendo na badala yake watu wafanye kazi kwa masilahi ya taifa ili kuweza kufanikiwa kwa miradi ambayo serikali imedhamiria kuifanya, alisema Dk. Magufuli. Aliwataka Watanzania kujitokeza kuomba kazi pindi ujenzi huo utakapoanza bila kujali itikadi zao za vyama lengo ni kuweza kujikwamua na umaskini.
source Tanzania daima
Hapo kwenye bolded ndo majibu ya magufuli kwa wabunge wa dar kama hajuwi
Mkataba wa ujenzi wa daraja hilo ulisainiwa jana na mwakilishi wa kampuni ya hiyo, Shi Yiqian, na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jami (NSSF), Dk. Ramadhan Dau.
Akizungumzia ujenzi huo, Dau alisema kuwa ndoto imetimia ambapo kazi iliyobaki ni utekelezaji kwa kampuni hiyo kuanza kujenga.
Alisema kuwa shirika limehangaika sana katika kufanya kazi kutafuta mkandarasi mshauri wa mradi huo ambapo limechukua kipindi kirefu hadi kufikia kumpata.
Dau alisema katika ujenzi huo NSSF inatoa asilimia 60 ya mradi mzima na serikali itatoa asilimia 40 ambapo mradi mzima utagharimu sh 214, 630,40,000. Naye, Waziri wa Ujenzi, Dk. John Magufuli, alimtaka mkandarasi kufanya kazi kwa nguvu ili ujenzi wa daraja hilo uwe umekamilika ndani ya miezi 36.
Dk. Magufuli alisema katika ujenzi huo hakuhitajiki siasa kutokana na Watanzania kuchoshwa na mambo hayo badala yake watu wanataka daraja kwa ajili ya shughuli zao za maendeleo.
Alisema kuwa kuendekeza siasa kutawafikisha pabaya Watanzania na kukosekana kwa maendeleo na kuacha kutumia fursa zilizopo.
Watu wamechoka na siasa zisizo za vitendo na badala yake watu wafanye kazi kwa masilahi ya taifa ili kuweza kufanikiwa kwa miradi ambayo serikali imedhamiria kuifanya, alisema Dk. Magufuli. Aliwataka Watanzania kujitokeza kuomba kazi pindi ujenzi huo utakapoanza bila kujali itikadi zao za vyama lengo ni kuweza kujikwamua na umaskini.
source Tanzania daima
Hapo kwenye bolded ndo majibu ya magufuli kwa wabunge wa dar kama hajuwi