Wachawi bado wananiandama

Wachawi bado wananiandama

Joined
Aug 13, 2015
Posts
94
Reaction score
75
Baada ya kufiwa na mwanangu mwenye umri wa siku mbili katika mazingira ya utata, takribani wiki 3 zilizopita,niliamua kukaa karibu na Mungu ili nisije kuanza kuwatwanga risasi watu wote ninao wahisi kuwa wachawi ktk eneo hili la Maswa, maombi ya nguvu nikishirikisha watumishi mbali mbali wa Mungu yalianza.

Wiki moja baadae asubuhi nikakuta nyayo kubwa kama ngumi ya mtu mzima za fisi ama simba zikiwa zimeizunguka nyumba yangu na katika dirisha la chumba changu nje palikuwa pamekwaruzwa kwa nyayo zile sambamba na alama za raba za mtu aliyekuwa kasimama dirishani.

Kabla ya kufiwa na mwanangu wakati mke wangu akiwa mjamzito nilikuta alfajiri saa 12 kinyesi cha binadamu mlangoni kwangu,Leo hii alfajiri saa 11 nimeshtuka na kujikuta nikiwa uchi kitandani wakati nililala na nguo,nilianza kusali na kuzizingira nguo hizo kwa damu ya Yesu,dk 5 baada ya kumaliza maombi paka akaanza kulia nje ya dirisha la chumba changu kwa sauti hafifu sana,nikamkea na kisha akatoweka ghafla.

Ole wenu wachawi nitawashinda ktk ulimwengu wa roho.
 
haya Mambo magumu sana, yote hayo uliyosema nayaona ya kawaida sana na sioni ajabu. Cha ajabu ni hicho cha kujikuta uchi wakati hukuvua nguo. Sio kwamba ulivua lakini ukasahau kweli boss?

Hebu niambie, Huwa unakunywa pombe?
 
Endeleza maombi Mungu atakufunulia mbaya wako kwa namna ya ajabu... suichoke kufunga na kuomba Mungu atasema nao
 
haya Mambo magumu sana, yote hayo uliyosema nayaona ya kawaida sana na sioni ajabu. Cha ajabu ni hicho cha kujikuta uchi wakati hukuvua nguo. Sio kwamba ulivua lakini ukasahau kweli boss?

Hebu niambie, Huwa unakunywa pombe?

Kutokana na mawazo, kuna muda unaweza ukaota alafu unasahau kuwa uliota. Sasa ikitokea kumbukumbu za ile ndoto zikikujia baada ya masaa au siku utadhani ndio tukio lilitokea kweli na ndio mwanzo wa kuandika hivi.

Mimi kuna mtu alinilipa deni langu ndotoni bila kujua mimi ninadhani alinilipa kawaida.

Ngoja sasa siku niliyotafakari vizuri ndio nilicharuka
 
pole ndugu. zidi kusimama katika uwepo wa Mungu, naye atakutetea. Upo wakati wa Mungu kukutetea.
 
sasa nyie wachawi , mlimvua nguo bwana the Counseller,,,, ili iweje?... Dah! Pole sana!.... walikuacha salama kweli hawa?....Naomba Ukimbie haraka kacheki afya Mkuu!
 
Last edited by a moderator:
Pastor Illovo kuna mtumishi atahitaji huduma ya kiroho uku pasipo kuwasahau wazee wa miti shamba MziziMkavu na mshanajr
 
Last edited by a moderator:
mshanajr na MziziMkavu ebu njooni kama mnalo suluhisho la huyu ndugu

Baada ya kufiwa na mwanangu mwenye umri wa siku mbili katika mazingira ya utata, takribani wiki 3 zilizopita,niliamua kukaa karibu na Mungu ili nisije kuanza kuwatwanga risasi watu wote ninao wahisi kuwa wachawi ktk eneo hili la Maswa, maombi ya nguvu nikishirikisha watumishi mbali mbali wa Mungu yalianza.

Wiki moja baadae asubuhi nikakuta nyayo kubwa kama ngumi ya mtu mzima za fisi ama simba zikiwa zimeizunguka nyumba yangu na katika dirisha la chumba changu nje palikuwa pamekwaruzwa kwa nyayo zile sambamba na alama za raba za mtu aliyekuwa kasimama dirishani.

Kabla ya kufiwa na mwanangu wakati mke wangu akiwa mjamzito nilikuta alfajiri saa 12 kinyesi cha binadamu mlangoni kwangu,Leo hii alfajiri saa 11 nimeshtuka na kujikuta nikiwa uchi kitandani wakati nililala na nguo,nilianza kusali na kuzizingira nguo hizo kwa damu ya Yesu,dk 5 baada ya kumaliza maombi paka akaanza kulia nje ya dirisha la chumba changu kwa sauti hafifu sana,nikamkea na kisha akatoweka ghafla.

Ole wenu wachawi nitawashinda ktk ulimwengu wa roho.
Pole bibie kwa kuandamwa na kuchezewa mchezo na hao wachawi na nyumba yako ipo nyepesi ndio maana hao wachawi wanaweza kuingia mpaka ndani wamemla mwanao sasa wanataka kukumaliza na wewe pia. Mimi nitakusaidia dawa ndogo ya kuwakomesha kisha ukitaka dawa kubwa

utanitafuta kwa wakati wako Dawa yenyewe hivi: Katafute kwa mafundi majiko au mafundi wa vyuma Madini ya shaba kipande kidogo tu unapokwenda kukinunuwa kwa aho mafundi usiwaambieni unakwenda kukifanyia nini madini ya shaba

wafiche iwe siri yako kishaukichukuwe hicho kipande cha madini ya shaba ukiweke chini ya Mto mchawi akija kwako kwa uwezı wa hicho kipande cha madini ya shaba kitamuunguza na atatoka mbio hatorudi tena kwako .na kila usiku

soma hii dua kabla hujalala mara 3 au mara 7 kisha lala. dua yenyewe hii hapa
(Kwa ajili ya ulinzi kutokana na hatari Soma, Zaburi 18 au 91) Kipande cha madini ya shaba angalia hapo chini picha yake.

copper.jpg
 
Baada ya kufiwa na mwanangu mwenye umri wa siku mbili katika mazingira ya utata, takribani wiki 3 zilizopita,niliamua kukaa karibu na Mungu ili nisije kuanza kuwatwanga risasi watu wote ninao wahisi kuwa wachawi ktk eneo hili la Maswa, maombi ya nguvu nikishirikisha watumishi mbali mbali wa Mungu yalianza.

Wiki moja baadae asubuhi nikakuta nyayo kubwa kama ngumi ya mtu mzima za fisi ama simba zikiwa zimeizunguka nyumba yangu na katika dirisha la chumba changu nje palikuwa pamekwaruzwa kwa nyayo zile sambamba na alama za raba za mtu aliyekuwa kasimama dirishani.

Kabla ya kufiwa na mwanangu wakati mke wangu akiwa mjamzito nilikuta alfajiri saa 12 kinyesi cha binadamu mlangoni kwangu,Leo hii alfajiri saa 11 nimeshtuka na kujikuta nikiwa uchi kitandani wakati nililala na nguo,nilianza kusali na kuzizingira nguo hizo kwa damu ya Yesu,dk 5 baada ya kumaliza maombi paka akaanza kulia nje ya dirisha la chumba changu kwa sauti hafifu sana,nikamkea na kisha akatoweka ghafla.

Ole wenu wachawi nitawashinda ktk ulimwengu wa roho.

Ondoa hofu Mungu wetu ni mkuu kuliko kitu chochote katika ulimwengu huu...ukiwa na hofu watakudhuru...
 
washamuulia Mtoto action 1
action 2,on the way....
shika imani ya Dini kisawasawa ""acha makandokando""
...endapo kama unaona imani yako NI haba sana... nawe ukajilazimisha!!!
 
haya Mambo magumu sana, yote hayo uliyosema nayaona ya kawaida sana na sioni ajabu. Cha ajabu ni hicho cha kujikuta uchi wakati hukuvua nguo. Sio kwamba ulivua lakini ukasahau kweli boss?

Hebu niambie, Huwa unakunywa pombe?


haha haha kwa ugonjwa wa kusahau.


swissme
 
Endelea kuomba na kuamini katika ulinzi wa Mungu! Ni Mlinzi asiyesinzia...some Biblia ili umjue Mungu zaidi. Hakika Hatakuacha...Atakupigania Hakika kama Utamtegemea na Kumwamini! Blessings!
 
Baada ya kufiwa na mwanangu mwenye umri wa siku mbili katika mazingira ya utata, takribani wiki 3 zilizopita,niliamua kukaa karibu na Mungu ili nisije kuanza kuwatwanga risasi watu wote ninao wahisi kuwa wachawi ktk eneo hili la Maswa, maombi ya nguvu nikishirikisha watumishi mbali mbali wa Mungu yalianza.

Wiki moja baadae asubuhi nikakuta nyayo kubwa kama ngumi ya mtu mzima za fisi ama simba zikiwa zimeizunguka nyumba yangu na katika dirisha la chumba changu nje palikuwa pamekwaruzwa kwa nyayo zile sambamba na alama za raba za mtu aliyekuwa kasimama dirishani.

Kabla ya kufiwa na mwanangu wakati mke wangu akiwa mjamzito nilikuta alfajiri saa 12 kinyesi cha binadamu mlangoni kwangu,Leo hii alfajiri saa 11 nimeshtuka na kujikuta nikiwa uchi kitandani wakati nililala na nguo,nilianza kusali na kuzizingira nguo hizo kwa damu ya Yesu,dk 5 baada ya kumaliza maombi paka akaanza kulia nje ya dirisha la chumba changu kwa sauti hafifu sana,nikamkea na kisha akatoweka ghafla.

Ole wenu wachawi nitawashinda ktk ulimwengu wa roho.

mkuu pole sana , kama vipi ngoja nikuunganishe na mkuu john shibuda
ili walau akupe link ya kukuwezesha kukaa kwa amani huko Maswa
kwani anafahamika vema sana.
 
Last edited by a moderator:
Haya mambo ya kichwawi mengine yana records ndani ya familia zetu.
Na wapo watu Baba zao na Mamazao ni wachawi ila wao wakiambiwa wanasubiria ushahidi.
Kwanza jitathmini mwenyewe,either unamali ya Dhulma,au kwenye mahusiano yenu ya ndoa wazazi wa upande mmoja au mmoja wapo hakupenda muoane.Hii hupelekea kuuwa kila kizazi.
 
Ungekuwa Muislam ningekupa dua usome,wiki tu ungezika mtu,hata kama mama yako.

Na ndio maan watu wa tiba au waganga,wakiona ni mzazi basi wanakufisha,ila kuna jamaa yangu yeye alikuwa anaambiwa kabisa kwa ni baba yako.Maana hata kaka yake alikufa kiutata.
Basi ilisomwa dua ya nguvu,wiki tu wakazika Baba yake,aisee jamaa anaroho ngum kweli akasema safi sana.Watu walibakia midomo wazi,ila hapo ndio baadhi ya watu wakamuweka wazi juu ya Baba yake.Na kabla ya baba yake kufa,wakati anahangaika na umauti alisema yoote
 
Back
Top Bottom