Wabunge wa Tanzania Vs Spika Ndugai Vs Wananchi

Kambaku

JF-Expert Member
Nov 12, 2011
7,184
26,848
Hivi wabunge wa Tanzania mkataba wao ukoje. Hawa ni wawakilishi wa wananchi na wananchi ndio huwatuma bungeni sasa kuna dhambi gani wananchi kuwatumia au kuwaandikia maswali wawakilishi wao ili wakaulize bungeni kwa niaba yao? Kwanini Spika alimkataza mbunge Devotha kuuliza swali kwa sababu kaandikiwa au katumwa na watu wengine?

Mwenye uelewa jamani naomba msaada wa tafsiri hapa.

Na hivi ni dhambi mbunge kujiandaa kwa kuandika swali lake ili ikifika zamu yake aliulize kwa unadhifu zaidi au ni lazima saa ya kuuliza swali litoke kichwani straight?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…