Wabunge wa Chadema watahudhuria hotuba ya Rais Kikwete?

Wameshakubali mbona na wameshaunda Kambi ya upinzani bungeni baadae wataweka mawaziri vimvuli? usicheze na kitu kinaitwa cheo au uheshimiwa mpango ulikuwa kumbwaga Slaa apotee in next 5 years na umetimia we unadhani CCM tu walitaka kumpoteza sita? na vyama vingine wana watu wao kaka..

Acha kuongea upumbavu kama huna hoja sio lazima kudandia kila topic.
 
Hakuna sababu ya kumsikiliza rais wa kundi la watu wachache kati ya wengi pamoja na kuchakachua waende zao wakafanye shughuli zao zingine kama alivyofanya Dk. Silaa tangu awali wabunge wamuunge mkono na siyo kujipendekeza kama kwa jk. Kama cuf

Mkuu najua una hasira ila hapa kidogo tutmie uumgwana, hatupo bungeni kwa ajili ya chama bali kwa ajili ya watanzania waliotuchagua. Tufanye mambo kwa hekima, haya mambo yatakaa sawa maana mpaka sasa wakombozi wa kweli wa Tanzania wameshajulikana.
 
yes, ni jambo la busara na hekima kuhudhuria hotuba ya rais, hata kama mna mambo yenu rohoni ila huyu ni rais na katiba yetu inataka kumheshimu rais. itakua ni utoto tu na akili za kuku kuzira, hopeful they gonna attend. thanks

sidhani kama ni sahihi kuhudhuria hotuba hiyo.nilazima yawepo matendo yatakayomfumbua Raisi Kilaza macho kuwa hakubaliki,watanzania tusiwe wanafiki,tanzania itabadilishwa na watu wachache wenye uchungu na watanzania wote,hivi kweli utamueleza mtu mwenye akili timamu kwa amani ya rohoni kuwa Tanzania tuna Raisi hata watoto wadogo wanalijua hili sasa,nilazima tupambane kuhakikisha haya yanatoweka Tanzania ni nchi yetu hatuwezi kuiacha iteketezwe na watu wachache wenye masilai yao binafsi na ushabiki usio na msingi,hatuna mda wa kufanya ushabiki sasa kiila mwenye akili anatakiwa kujiuliza nini cha kufanya kwa michango ya kuikomboa nchi hii inatakiwa sasa,watu wanaishi bila kuwa na uhuru wao binafsi tutaishi hivi mpaka lini?wafanyabihashara na wasomi ,wataalamu wazuri wote wanatafuta jinsi ya kuihama nchi yao hii mpaka lini??????????????

open your eyes men ,this is the hour for all things to happen.

NO PRESIDENT IN TANZANIA NO MATTER AMEAPISHWA NA WATU WAKE WA CCM BUT WATANZANIA NO OOOOOOOOOOOOOOOO,Na safari hii watakoma maana raisi mwenyewe hafuati sheria sijui nani ataniambia nifuate sheria.


sidhani
 
Hivi hujui Zitto na Mbowe wote wanataka kuwa wenyekiti wa chama na kiti kipo kimoja? unajua godfather EM alimkataa Zitto kuwa mwenyekiti eti kwakua hawamjui sawaswa na akaamua kumpa mkwe wake? nawapenda wapiganani wa Chadema no doubt ila mfumo wa chama siupendi ngoja nitafautiane na nyie.....

Kuna jamaa alisema kuwa
ukitaka kujua tabia za mume, angalia matendo yaa mkewe
hii nmeikubali kwani ina uhusiano no hii
ukitaka kujua tabia na msimamo wa mwanaJF basi angalia AVATAR yake
 
Wameshakubali mbona na wameshaunda Kambi ya upinzani bungeni baadae wataweka mawaziri vimvuli? usicheze na kitu kinaitwa cheo au uheshimiwa mpango ulikuwa kumbwaga Slaa apotee in next 5 years na umetimia we unadhani CCM tu walitaka kumpoteza sita? na vyama vingine wana watu wao kaka..

mawazo mengine bwana as if mtu unaandika huku unakimbizwa
 
Ifike mahali chadema ichague moja; ama ikumbali ya kuwa JK alichaguliwa kihalali na umma wa watanzania na hivyo kinamtambua kama rais, vinginevyo kama chama hicho kinaendelea na msimamo wa kudai kwamba hakuchaguliwa kihalali sioni namna chama hicho kinavyoweza kutambua urais wake; na kama chama hicho hakimtambui kama rais itakuwa ni kichekesho kama wabunge wake watahudhuria hotuba ya ufunguzi wake wa bunge.
 
wasiikimbie hotuba ya rais.wamsikilize then waichuje waweze kupata hata hoja humo! wakisepa haina maana na itakuwa picha mbaya sana na kukiaribia chama cha chadema sifa kubwa ambayo tayari wanayo
 
Back
Top Bottom