Nakuunga mkono zaid ya 100%,lowasa kuingia CDM nikukiua chama kwa haraka na uhakika mkubwa,mtu ambaye mlisema ni fisadi na ccm wakawasaidia zaid kusema ni kwel ni fisadi,leo kusema mumkaribishe nikujiua kwa uhakika mkubwa sana,
Hakuna taasisi yoyote ambayo imewahi kumsafisha na wala yeye mwenyewe hajawahi sema ni nani alihusika kama siyo yeye zaidi yakusema anauchukia umaskini(ambayo ni porojo)...
Leo bashe amemnyanyua mkono magufuli,ambapo bashe alikuwa ni mtu muhimu katika team ya lowasa,ila leo kamtosa,wale madiwan wa monduli ni kizungumkuti,leo wanasema wapo CDM kesho wamechukua form zakugombea udiwani ccm,kwa hiyo utaona kuwa lowasa hana wafuasi wala watu ambao utasema ni wapo nae popote pale,zaid ya wao kuangalia fursa(na lowasa wakat ule alitumia fedha sana)na hata hawa wanaoshadadia ahamie CDM ni kuwa bado anawapa fedha.
Kitendo cha lowasa kujiunga CDM iwe awe mwanachama wa kawaida au vyovyote ujue CDM itapoteza wanachama wengi ambao ni wafia chama na hata ule uaminifu katika macho ya watu utakuwa umekufa na hiko ndio kifo chake...
Ccm imevua gamba CDM inajifanya inajua kuaminisha watu nyeusi ni nyeupe,katika kosa kubwa lakiufundi watalofanya CDM nikumpokea lowasa,huku kwenye mitandao watu wanapiga kelele kuwa anafaa ila huko field hali ni tofauti...ujumbe huu uwafikie,wasiposikia wataona kwa vitendo...CDM inajitosheleza haihitaji mtu wa namna yake