Wabunge wa CHADEMA wamkaribisha Lowassa

Wabunge wa CHADEMA wamkaribisha Lowassa

Baadhi ya wabunge wa CHADEMA wamezungumzia taarifa zinazosambaa zikieleza kuwapo mkakati wa Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa kuhamia katika chama hicho, wengi wao wakimkaribisha.

Wakati wabunge hao wakikubali kumpokea, Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk Willibrod Slaa amesema wananchi wasubiri mambo yatakapokuwa tayari badala ya kutegemea mitandao ya kijamii.

“Nitazungumza pale mambo yatakapokuwa sawa, siwezi kuzungumza sasa, subirini… sasa hivi mambo mengi yanazungumzwa kwenye mitandao,” alisema Dk Slaa ambaye pia anatajwa kuwa mgombea wa chama hicho ndani ya Ukawa.

Msemaji wa Lowassa, Aboubakary Liongo alipoulizwa kuhusu kuwapo kwa mpango huo alisema hawezi kulizungumzia hilo kwa kuwa ni suala la mtu binafsi. Hata hivyo, jitihada za kumpata Lowassa jana hazikufanikiwa kwani simu yake iliita pasi na kupokewa.

Hivi karibuni, idadi kubwa ya madiwani wa CCM walirudisha kadi zao na kujiunga na Chadema wakisema sababu ni kutoridhishwa na kukatwa kwa jina Lowassa kati ya wagombea urais wa CCM.

Kadhalika, mtandao wa kijamii uliokuwa ukimuunga mkono mbunge huyo wa Monduli unajulikana kwa jina la 4U Movement ulitangaza kuhamia CHADEMA hali inayoashiria kuwa kuna dalili ya Lowassa pia kujiunga nao.

Wakiandika katika akaunti ya Twitter ya 4U Movement, wafuasi hao walisema: “Ukimya ni hekima na ukimya ni busara. Ukimya wa Edward Lowassa ni kutafakari Safari ya Matumaini... Tuungane kuyapata mabadiliko nje CCM.”

CHADEMA ni kanisa la wokovu

Akizungumzia taarifa hizo, Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa alikifananisha chama hicho na kanisa ambalo kwa kawaida halikatai mtu, bali linawapokea wenye dhambi na kuwaongoza kufanya toba.

“CHADEMA ni kama kanisa, hakataliwi mtu, tunahubiri habari njema ya wokovu, ukija hapa unatubu unaendelea kufanya kazi,” alisema.

Kuhusu viongozi wa CCM kuhamia CHADEMA, Msigwa alisema inawezekana kasi hiyo inachagizwa na Lowassa kukosa nafasi aliyoitaka ndani ya chama hicho.

“Unapokuwa mwanasiasa unakuwa na wafuasi, inawezekana wengine wanaohamia CHADEMA ni watu wake ambao wameona mtu wao amekosa nafasi aliyoitaka ndiyo maana wanakihama chama,” alisema.

Msigwa alisema CHADEMA ilikuwa inakusanya wanachama wapya kwa muda mrefu hata kabla ya vuguvugu la Lowassa na chama chake kuibuka na ushindi na wanaohamia wanafanya hivyo kwa sababu wanakipenda chama na wameichoka CCM.

Huenda akatimiza safari ya matumaini

Akizungumzia ujio wa Lowassa kwenye chama hicho, Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema alisema iwapo Lowassa atahamia CHADEMA anakaribishwa na huenda akaitimiza safari yake ya matumaini.

“Namkaribisha Lowassa CHADEMA, huenda safari yake ya matumaini ikaishia huku, akawa mwanachama au hata kiongozi,” alisema.

Alisema hakuna shaka kuwa mbunge huyo wa Monduli ana nguvu ndani ya CCM ndiyo maana viongozi wengi wa chama hicho wanakihama wakati huu.

“Hiyo ilijionyesha kuanzia kwenye Kamati Kuu ya CCM, Halmashauri Kuu, Lowasa amekamata wajumbe kwa asilimia 80 na hiyo ni ishara kuwa ameishika CCM,” alisema.

Lema aliongeza kuwa wanaoihama CCM hawaihami kwa bahati mbaya, bali wameona mtu wao waliyemtarajia ameondoka.

“Ni wengi wanaohamia CHADEMA, kwa sasa kadi zimetuishia na hiyo ni ishara kuwa CCM inakufa, ripoti za mikoa yote tunazo,” alisema.

Mbunge wa Viti Maalumu, Lucy Owenya alisema wanaoihama CCM kwa sasa wamegundua kuwa chama pekee kinachoweza kutetea wananchi ni CHADEMA.

“Sisi tunawakaribisha kwa mikono miwili, waje tuchape kazi, ilimradi wanafuata kanuni na taratibu za chama, basi. Wamejionea wenyewe kuwa CCM hakuna chochote,” alisema.

Alisema CCM waliamua kupitisha katiba bila kuwapo kwa Ukawa, lakini sasa wameona kuwa walichokifanya ni makosa na wameanza kurudi CHADEMA ambako wanaamini kuna demokrasia ya kweli.

Mbunge wa Viti Maalumu, Cecilia Paresso alisema: “Tunamkaribisha kwa mikono miwili. Tumekinyooshea CCM vidole kwa muda mrefu kuwa kuna rushwa na makundi na hilo linajidhihirisha sasa. Lakini wale wote wanaokuja CHADEMA, tunawakaribisha ili mradi wafuate kanuni na taratibu zetu.”

Paresso alisema hana tathmini ya kina kuhusu wafuasi wa Lowassa wanaoihama CCM, bali wanaokihama chama hicho wameona kina matatizo.

Atakiwa akidhi vigezo na masharti

Licha ya kuonyesha kumkaribisha, katika chama hicho, baadhi ya wabunge walimtaka Lowassa afuate kanuni ili awe mwanachama mwenye sifa.

Mbunge wa Mbozi Magharibi, David Silinde alisema anakaribishwa lakini hana budi kufuata sheria na kanuni za chama... “Anatakiwa afuate taratibu za chama, milango ipo huru, lakini afuate kanuni… asije akafikiri ataleta taratibu zake hapa, sitakubali.”

Silinde alisema wanaohamia CHADEMA hawajapendezwa na mwenendo mzima wa uteuzi wa mgombea wa urais na hivyo wameifuata demokrasia ya kweli ndani ya chama hicho.

Mbunge wa Kawe, Halima Mdee hakutaka kuzungumzia kwa undani suala hilo lakini alisema endapo atajiunga, chama hicho kitampokea kulingana na vigezo na taratibu.

“Akihamia CHADEMA nitatoa maoni yangu lakini ninachoweza kusema ni kuwa kila mtu ana haki ya kwenda chama chochote ili mradi ana tija,” alisema.

Mdee alisema wanaCCM wanaohamia CHADEMA wamesoma alama za nyakati na kuona kuwa CCM haiendani na ahadi zake.

Mbunge wa Viti Maalumu, Susan Lyimo alisema, Lowassa ni binadamu wa kawaida kwa hiyo kuhamia kwake CHADEMA si kitu cha ajabu ilimradi afuate kanuni... “Cha muhimu afuate masharti ya chama, kanuni na taratibu, kama watu wanahama vyama vingine yeye ni nani asihame CCM?”

Lyimo alisema wanaCCM wengine wanakaribishwa kujiunga kwa sababu kwenye siasa hakuna rafiki wa kudumu wala adui wa kudumu.

Mbunge wa Viti Maalumu, Pauline Gekul, aliwataka wana CCM na Lowasa kuhamia zaidi Chadema ili kuunganisha nguvu na kuichukua nchi.

“Mfikishie salamu Lowassa mwambie karibu kwenye jeshi la ukombozi,” alisema.

Chanzo: Mwananchi

Kuna kitu cha ajaabu kidogo. Wabunge wote wa Kaskazini wako radhi kumpokea fisadi aliyenyimwa uingozi kwao. Amebaki Silinde pekee ndiye kaongea kama Mtanzania, wengine wire ukabika. Ama kweli tutaona mengi safari hii. Makamanda wako tayari kumtisa Kamanda Slaa mradi tu wawe na "mwenzai". Matata kwelikweli. WM.
 
Mkuu, ...Suala muhimu siyo kubadili chama au jina la chama, suala muhimu ni kubadili mfumo wa fikra na mitazamo.
Unachosahau Ng'wamapalala ni kwamba tupo humu ambao tunachukua muda kusoma mtiririko wa thread kabla ya ku comment na wapo ambao wata comment tu post moja bila kuangalia mjadala ulipoanzia, ulipo na unakoelekea. Ndio maana pamoja na kujiunga JF zaidi ya miaka minane iliyopita michango yangu haijafika 6,000 sawa na wastani wa post 2 kila siku tofauti na wengi.

Comment
uliyoitoa hapo juu yathibitisha kabisa ninalolisema kila siku, tuna watu wamejiaminisha kimakosa kwamba wanachosema ni sahihi. Tatizo la mfumo wa fikra na mtizamo hauwezi kupatiwa ufumbuzi na watu wale wale wenye fikra na mawazo yale yale yaliyosababisha fikra hizo hizo na mtizamo huo huo. Kuamini hivyo ni ama kujidanganya katika nafsi zetu au ni matokeo ya fikra zisizo huru zinazosukumwa na unafiki.

Duniani kote panafika pahala ili kuweza kufanikiwa kuleta mabadiliko lazima kutokee mapinduzi na kama nchi imeweza kuongozwa na watu wale wale kwa mfumo ule ule kwa miaka hamsini, mabadiliko hayawezi tena kuwa ya hiari. Binadamu ana tatizo la mazoea na mazoea yanapata nguvu zaidi kadiri siku zinavyosogea na ndio maana ni vigumu kuwatoa madarakani waliokaa muda mrefu kama CCM kwani kumejengeka kiburi cha hatimiliki mioyoni mwao.

Kukaa tukisubiri mabadiliko yaletwe na CCM ni zaidi ya ujuha kwani mtu anatakiwa tu ajiulize ni kitu gani kimezuia hayo mabadiliko yasifanikiwe kwa mihula hiyo yote. Alikuja Mwinyi na ufagio akatuahidi Tanzania mpya na safi, miaka kumi baadaye akaja Mkapa na uwajibikaji akiahidi uwazi na uwajibikaji, miaka ishirini baadaye akaja Kikwete na nguvu mpya, ari mpya na kasi mpya! Wote tu mashahidi kwa matatizo tuliyoyapata.
Siyo wote walioko CCM ni mafisadi na siyo mafisadi wote ni CCM.
Hii ndio hasa ninaiita lugha ya kilaghai ambayo inaweza kutamkwa na mtu anayedanganyika kirahisi, tabia ambayo imekuzwa na mazoea badala hali halisi. Kama kuna fisadi nchi hii, kikatiba ni nani anatakiwa kumshughulikia? Kama kuna wahalifu ndani ya nchi hii ni nani kapewa mamlaka na katiba ya nchi kumwajibisha? Kama tuna utawala unaofuata sheria ni kwa nini kila siku ni kilio kile kile cha wananchi kuhusu kutopata haki na usawa mbele ya sheria?

Mwaka 2010 kuna watu walitajwa kwamba ni mafisadi lakini pamoja na kelele zote, watu hao hao eti walichaguliwa kwa kura nyingi na kupewa uongozi wa nchi! Utawala uliokuwapo ulitumia kila mbinu kuhakikisha unabaki madarakani ikiwa ni pamoja na kuvitumia vyombo vya dola usalama kusimamia uchaguzi usio huru. Nani yuko CCM amewahi kukemea matumizi ya vyombo vya dola kupambana na wananchi wanaodai haki zao? Sana sana tumeshuhudia wale wanaowajeruhi na hata kuwaua wananchi wasio na hatia wakipandishwa vyeo!

Hapana Ng'wamapalala, wewe ni katika watu wanaokesha humu wakitetea hali hii kwa madai ya kijinga kama ulivyoanza hapo juu..eti Siyo wote walioko CCM ni mafisadi na siyo mafisadi wote ni CCM. Wote tumeshuhudia mafisadi ndani ya CCM wakilindwa na hata kuogopwa, je hao mafisadi walio nje ya CCM nao wako juu ya sheria? Mathalani ikithibitika kwa Mh. Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema kaiba, vyombo vya dola vinasubiri nini kumshughulikia au na yeye anaogopwa na serikali kama alivyowahi kutamka Waziri Mkuu Mizengo Pinda?

Mbona ni jambo la kawaida tu kuwakamata viongozi wa upinzani, kuwapiga wabunge wa upinzani na hata kuwasweka ndani kwa mambo ya kipuuzi? Kwa nini kama ni wezi wasikamatwe wakafunguliwa mashtaka? @Ng'wamapala, nachukia sana unafiki lakini nachukia zaidi matapeli wa kisiasa popote walipo. Hebu soma tena mada zote unazozianzisha pole pole na taratibu halafu ujiulize kama kweli una nia njema katika kuzianzisha. Hao wasafi ndani ya CCM wameweza vipi kuishi pamoja na kuwa na mshikamano na mafisadi?
 
Last edited by a moderator:
Asanteni wabunge wa chadema kwa kukiri kumpokea mzee weyu low as a, watanzania baadhi wanaanza kutuonyesha ukabila hasa kwenye kupeana ajira na Leo wanaleta usoni, jeshi no wasukuma wamejaa kisa wakubwa ndio wao, tunawataka viongozi was kutujali site,
 
HABARINI ZA JIONI

MAKAMANDA NAOMBA UFAFANUZI KUHUSU HILI

1. inakuwaje lowasa akiwa nje ya chadema anakuwa fisadi ..ila akiwa ndani ya chadema anakuwa msafi..nasema ivi kutokana na chadema kujiandaa kumpokea lowasa ushahidi ninao na picha ninazo..kuwa soon lowasa anaenda chadema..kama niivyo hata magufuli aki amia chadema nahizi kashfa mnazo mpa atakuwa msafi tena

2.ina kuwaje kwenye pesa ambazo na watu wa chadema zina wahusu huwa hawa ongei chochote..inamaana nanyi pia mna jali maslahi yenu..nasema hivi nikiwa na maanisha pesa za kampeni zilitolewa nyingi sana zaidi ya milion 200 kwa kila mbunge lakini hakuna hata moja alie lalamika kuwa serikali ina ingia hasara na wananchi wana umia..posho za bunge nikubwa sana but hakuna wabunge wanao fight with..

Niliwaza kuconlude kuwa chadema huwa wanakuwa wapole sehemu ambayo na wenyew wana husika...

NAOMBA NIELEWEKE KUWA SIKO UPANDE WA CHAMA CHOCHOTE ILA NAOMBA MAJIBU TOKA KWENU MAKAMANDA..
 
Mapato na matumizi ya chama hazina ipo tengelu, na hapo hakuna anaehoji.
 
Mmeingia woga sana, lakini hamna namna...

Leo mtasema yote, endeleeni kuropokwa...

Teh teh
 
Ametubu, kwani mtu akikosa basi ataendelea kuwa mkosaji mpaka afe??? Fikiria hata wewe dhambi ngapi umefanya hivyo msikitini/kanisani wakufukuze. Ukiona umeenda kanisani/msikitini ina maana umekubaliana na sera za huko. Karibu na wewe tukutubishe, uwe msafi
 
Hakuna jibu, maana unacho uliza ni wazo lako, au hisia zako, sasa unatakka kujibiwa hisia zako? Lowassa yupo CCM si Chadema, kama umeota yuko Chadema pole yako, Elewa hiyo ni ndoto tu kama ndoto zingine
 
HABARINI ZA JIONI

MAKAMANDA NAOMBA UFAFANUZI KUHUSU HILI

1. inakuwaje lowasa akiwa nje ya chadema anakuwa fisadi ..ila akiwa ndani ya chadema anakuwa msafi..nasema ivi kutokana na chadema kujiandaa kumpokea lowasa ushahidi ninao na picha ninazo..kuwa soon lowasa anaenda chadema..kama niivyo hata magufuli aki amia chadema nahizi kashfa mnazo mpa atakuwa msafi tena

2.ina kuwaje kwenye pesa ambazo na watu wa chadema zina wahusu huwa hawa ongei chochote..inamaana nanyi pia mna jali maslahi yenu..nasema hivi nikiwa na maanisha pesa za kampeni zilitolewa nyingi sana zaidi ya milion 200 kwa kila mbunge lakini hakuna hata moja alie lalamika kuwa serikali ina ingia hasara na wananchi wana umia..posho za bunge nikubwa sana but hakuna wabunge wanao fight with..

Niliwaza kuconlude kuwa chadema huwa wanakuwa wapole sehemu ambayo na wenyew wana husika...

NAOMBA NIELEWEKE KUWA SIKO UPANDE WA CHAMA CHOCHOTE ILA NAOMBA MAJIBU TOKA KWENU MAKAMANDA..
Nani ksema Lowsa anatfutwa na CDM? Un ushhidi?
 
petro faustine,

..hivi hujawahi kusikia mhalifu akisaidia polisi ktk upelelezi?

..wakati mwingine mhalifu anaweza hata kusamehewa makosa yake au kupewa kifungo kifupi ikiwa atatoa ushirikiano utakaopelekea kukamatwa wahalifu wengi zaidi.
 
Last edited by a moderator:
Kila chama kinayo misingi yake ambayo ukitaka kwenda huko yakupasa uielewe Na uwe radhi kuifuata. Yy Na wenzie ukiona hivyo ujue wametubu Na kuiamini injili ya cdm. Hongereni cdm kwa usajili, Mimi sina chama ila nitawapigia kura yangu kwa ngazi zooooote.
 
Gamba Ng'wamapalala

Kila Siku lazima uanzishe thread inayomhusu Lowassa na CHADEMA.
Acha wivu wa Kike Mkuu,muacheni Mzee wa watu afanye analoona linamfaa,huku kutapata kwenu Ma agents wa Magamba ni indication kuwa huyo Mzee Mnamgwaya sana.
Mkuu;
Gamba Bramo

Kuanzisha thread ni utashi wa kila mwanaJF.

Huu wivu wa kike ndiyo upi? Wa kiume ndiyo upi?

Kuansisha thread zinazomhusu Lowassa haina maana nina muogopa au simuogopi.

Kitu gani kunafanya udhani ninatapatapa na pia ni ajent wa magamba.

Mimi na Lowassa wapi na wapi.

Nashangaa unaumizwa na thread zinazomhusu Lowassa. Kwani wewe pia ni ajent wa Lowassa?
 
HABARINI ZA JIONI

MAKAMANDA NAOMBA UFAFANUZI KUHUSU HILI

1. inakuwaje lowasa akiwa nje ya chadema anakuwa fisadi ..ila akiwa ndani ya chadema anakuwa msafi..nasema ivi kutokana na chadema kujiandaa kumpokea lowasa ushahidi ninao na picha ninazo..kuwa soon lowasa anaenda chadema..kama niivyo hata magufuli aki amia chadema nahizi kashfa mnazo mpa atakuwa msafi tena

2.ina kuwaje kwenye pesa ambazo na watu wa chadema zina wahusu huwa hawa ongei chochote..inamaana nanyi pia mna jali maslahi yenu..nasema hivi nikiwa na maanisha pesa za kampeni zilitolewa nyingi sana zaidi ya milion 200 kwa kila mbunge lakini hakuna hata moja alie lalamika kuwa serikali ina ingia hasara na wananchi wana umia..posho za bunge nikubwa sana but hakuna wabunge wanao fight with..

Niliwaza kuconlude kuwa chadema huwa wanakuwa wapole sehemu ambayo na wenyew wana husika...

NAOMBA NIELEWEKE KUWA SIKO UPANDE WA CHAMA CHOCHOTE ILA NAOMBA MAJIBU TOKA KWENU MAKAMANDA..
kama ungekuwa na akili ungewauliza ccm ni kwa nini waohawamfukuzi wakati wanasema na mchafu?

vile vile kama ungekuwa na akili ungeiuliza serikali ya ccm kwa nini hawakumpeleka mahakamani kwa sababu bunge lilisema alihusika na richmondi na moja ya mapendekezo ya kamati ya bunge lilikuwa kuwafikisha mahakamani wote waliohusika?

au na wewe wamekubandikia tikiti maji kichwani?
 
Mkuu;
Gamba Bramo

Kuanzisha thread ni utashi wa kila mwanaJF.

Huu wivu wa kike ndiyo upi? Wa kiume ndiyo upi?

Kuansisha thread zinazomhusu Lowassa haina maana nina muogopa au simuogopi.

Kitu gani kunafanya udhani ninatapatapa na pia ni ajent wa magamba.

Mimi na Lowassa wapi na wapi.

Nashangaa unaumizwa na thread zinazomhusu Lowassa. Kwani wewe pia ni ajent wa Lowassa?

Mkuu Gamba Ng'wamapalala


Kwnaini tu usifanye uka Complie thread zako zote zinazmhusu Lowassa na CHADEMA ukaja na uzi Mmoja.
Kila Siku Kuanzisha uzi unaomhusu Mtu ni Kushusha hadhi ya Jukwaa Letu Mkuu.
 
Last edited by a moderator:
HABARINI ZA JIONI

MAKAMANDA NAOMBA UFAFANUZI KUHUSU HILI

1. inakuwaje lowasa akiwa nje ya chadema anakuwa fisadi ..ila akiwa ndani ya chadema anakuwa msafi..nasema ivi kutokana na chadema kujiandaa kumpokea lowasa ushahidi ninao na picha ninazo..kuwa soon lowasa anaenda chadema..kama niivyo hata magufuli aki amia chadema nahizi kashfa mnazo mpa atakuwa msafi tena

2.ina kuwaje kwenye pesa ambazo na watu wa chadema zina wahusu huwa hawa ongei chochote..inamaana nanyi pia mna jali maslahi yenu..nasema hivi nikiwa na maanisha pesa za kampeni zilitolewa nyingi sana zaidi ya milion 200 kwa kila mbunge lakini hakuna hata moja alie lalamika kuwa serikali ina ingia hasara na wananchi wana umia..posho za bunge nikubwa sana but hakuna wabunge wanao fight with..

Niliwaza kuconlude kuwa chadema huwa wanakuwa wapole sehemu ambayo na wenyew wana husika...

NAOMBA NIELEWEKE KUWA SIKO UPANDE WA CHAMA CHOCHOTE ILA NAOMBA MAJIBU TOKA KWENU MAKAMANDA..
Mbona unajihami sana kuwa huna chama! Najua hofu yako ni kuwa utajulikana kuwa mwana CCM maana ni wana CCM tu wanaouliza maswali ya hovyo na wivu kiasi hiki. Basi kama huna chama chochote, umetumwa na mwana ccm uulize hili swali yaani unatumika, tena vibaya.
 
Wapumbavu kama wewe hawafundishiki, mmeona kuchukua watu wa mfumo ule ule, tena wanaotuhumiwa ufisadi ndio kuleta mabadiliko? au mmeshakuwa wachumia tumbo? Baada ya Lowasa kugawa fedha CCM na kuwagawa watu mnataka aje kugawa CDM na kutugawa? wewe na Mwenyekiti ni vibaraka, mnatakka hela za Lowasa , washenzi kabisa!!! na mkimpokea mtatukoma!!!! Shenzz!
Mkuu,
Acha jazba na matusi!

Kila mwananchi ana fikra na mtazamo wake, cha muhimu ni kujenga hoja na kupambana katika hoja.
 
Umesomeka mkuu,,,hata kama yeye lowasa hatakubali kujiunga na CDM hizo kauli na tetesi za viongoz wa cdm kumtaka lowasa ajiunge nao zimekishushia hadhi cdm..mi najiondoa rasmi CDM

Subiri Lowasa akiingia CHADEMA mnabadilishana kadi anakupa ya makufuli unampa ya funguo, kisha unaacha chama.
 
Wakuu,
Mtanisamehe kwa kutokuunga mkono ujio wa Edo CDM. Kiukweli kabisa chadema haikutakiwa imsubiri mtu ili imfanye kuwa mgombea wao. Chama kimekomaa kisiasa, hao watu wa ccm wanaojiunga na CDM na wanapokelewa kwa shamra shamra kubwa ni udhaifu uliopitiliza kwa chama changu. Wapo wenye uwezo wa kuongoza chama na wenye uwezo wa kuwa raisi wa jamhuri.

Nachelea kusema kuwa upinzani bado hatujajua lengo letu ni kitu gani na tunataka kufanya nini. Ninachokiona wazi ni maamuzi magumu ya kula matapishi yetu wenyewe. Tulihubiri na kuwasihi watu kwamba mafisadi hawatakiwi tena kwenda ikulu. Dr Slaa kwa kinywa chake akiwa na akili timamu aliwataja akina Edo kwamba ni vinara wa ufisadi Tanzania, kumbukeni "list of shame", leo tumeshau?! Hainingii akilini hata kidogo eti leo Lowassa anaonekana kuwa msafi pale tu atakapokuja CDM, ila akiwa CCM ni msafi, narudia huu ni upungufu wa akili mkubwa na kutokuwa na kumbukumbu.

Nawaomba CDM, chonde chonde, kuweni na maamuzi yenye tija, acheni kukumbatia maslahi yenu binafsi. Na endapo Edo ataenda CDM, huu ni ushindi kwa CCM, maana watatumia nafasi hii kwamba wao waliwakataa mafisadi ila wapinzani wakawapokea. kwa namna moja au nyingine watu watarudisha imani kwa CCM. Tufanye jitihada za dhati kuongeza wabunge wa upinzani, raisi tuangalie mtu huko huko UKAWA na sio kumsubiri Edward eti atakuja na watu kutoka CCM.

Watanzania tumekuwa na akili fupi kiasi kikubwa na hatuna dira kabisa, hii ni ishara kwamba hata upinzani utafanya yale yale yanayofanywa na CCM, na hawatakuwa na jipya kamwe!!!!!

C.C
Ben Saanane,
Tumaini Makene,
Kurugenzi ya Habari. et al.

Nakuunga mkono zaid ya 100%,lowasa kuingia CDM nikukiua chama kwa haraka na uhakika mkubwa,mtu ambaye mlisema ni fisadi na ccm wakawasaidia zaid kusema ni kwel ni fisadi,leo kusema mumkaribishe nikujiua kwa uhakika mkubwa sana,
Hakuna taasisi yoyote ambayo imewahi kumsafisha na wala yeye mwenyewe hajawahi sema ni nani alihusika kama siyo yeye zaidi yakusema anauchukia umaskini(ambayo ni porojo)...
Leo bashe amemnyanyua mkono magufuli,ambapo bashe alikuwa ni mtu muhimu katika team ya lowasa,ila leo kamtosa,wale madiwan wa monduli ni kizungumkuti,leo wanasema wapo CDM kesho wamechukua form zakugombea udiwani ccm,kwa hiyo utaona kuwa lowasa hana wafuasi wala watu ambao utasema ni wapo nae popote pale,zaid ya wao kuangalia fursa(na lowasa wakat ule alitumia fedha sana)na hata hawa wanaoshadadia ahamie CDM ni kuwa bado anawapa fedha.
Kitendo cha lowasa kujiunga CDM iwe awe mwanachama wa kawaida au vyovyote ujue CDM itapoteza wanachama wengi ambao ni wafia chama na hata ule uaminifu katika macho ya watu utakuwa umekufa na hiko ndio kifo chake...
Ccm imevua gamba CDM inajifanya inajua kuaminisha watu nyeusi ni nyeupe,katika kosa kubwa lakiufundi watalofanya CDM nikumpokea lowasa,huku kwenye mitandao watu wanapiga kelele kuwa anafaa ila huko field hali ni tofauti...ujumbe huu uwafikie,wasiposikia wataona kwa vitendo...CDM inajitosheleza haihitaji mtu wa namna yake
 
Umesomeka mkuu,,,hata kama yeye lowasa hatakubali kujiunga na CDM hizo kauli na tetesi za viongoz wa cdm kumtaka lowasa ajiunge nao zimekishushia hadhi cdm..mi najiondoa rasmi CDM

Subiri Lowasa akiingia CHADEMA mnabadilishana kadi anakupa ya makufuli unampa ya funguo, kisha unaacha chama.
 
Back
Top Bottom