Wabunge wa CCM wasioiunga mkono Bajeti ya Serikali wakwepa kupiga kura!

Haya Mnyika alishayasema, kuwa wabunge wa ccm kwa upuuzi wao wataipitisha tu hii bajeti. Ila watakapopatikana kina Mpina na Filikunjombe 20 ndani ya ccm basi kazi watakuwa nayo hao waliobakia
 
Hao wabunge wamejitahidi kuwaonyesha msimamo wao hilo tunawaunga mkono, hao wajinga wengine wao ni ndiooo.Majimbo waliowachagua ndio wehu.
 
Hata Kangi Lugola naye alitangaza kuipinga bajeti lakini jana hakwepo bungeni kupiga kura ya hapa, woga mbaya sana
 
Hata hivyo ni haki yake, na kuwepo kwake kusingebadili lolote. Bado tunawapongeza japo kwa kuonyesha misimamo yao juu ya hili[/QUOTE]

Mkuu, nakushauri usiwasifie. hiyo siyo misimamo ya kishujaa, ni misimamo ya kinafiki.
Mpamabanaji wa kweli hupigana hadi hatua ya mwisho, na siyo kutafuta visingizio vya kuondoka ulingoni ili hali mapambano uliyoyaanzisha bado yanaendelea.

Hatua ya mwisho ni ipi hiyo?
Si amesema na kila mwenye sikio amemsikia?
Kimtokacho mtu mdomoni ndicho kilicho Rohoni Mkuu!
 
Wote walio kimbia kupiga kura ni dhaifu tuuu! Waoga sana,wanaiogaopa almashauri ya ccm kuzidi wananchi wao!

Huu ni unafiki wa waziwazi maana kama kweli walikuwa wanapinga budget wasinge sepaa, mbona wenzao walirudi na kupiga kura?

Wote hao ni dhaifu,kwani hawana misimamo binafsi.
 
Hivi nyie mlidhani hawa waheshimiwa ni serious? Hawa ni wachumia tumbo tu. To them matumbo yao na maslahi binafsi ndiyo dira yao ya kwanza na ndiyo kipaumbele chao. Hili linafuatiwa na "mapenzi yao ya muda kwa chama chao" ambacho huwa kinawateua wakati wa chaguzi mbalimbali na mwisho kabisa ni wapiga kura wao - wale ambao huwa wanawanunua kwa fulana na kofia kutoka ughaibuni wakati wa msimu wa uchaguzi.

Watu hawa hawako kwa faida yetu ndio maana wamepitisha hii bajeti kwani machungu yawafikayo na yatakayowafika wananchi kutokana na hii bajeti si tatizo wala kero yao. Kwao cha muhimu ni kuendelea kuwa mjengoni na kupokea poshooooooozi?
 
Acha uongo wewe waliosema ndiyo ni magamba wenyewe tbc1 walionesha kiti chake kikiwa wazi. Hata kama hupendi usimzushie uongo

kama hakuwepo, basi katibu wa bunge alifanya kosa sana kutorudia kuita jina la shibuda, maana sauti ya 'ndiyo' ilisikika, ila niligundua kuwa shibuda hana sauti dhaifu vile
 
John Shibuda alisema ndiyo,ila sikumshangaa sababu yupo chma tawala kwa kupitia chama pinzani.Huyu ni wakumtema mwaka 2015 hatufai kama mbunge sina chama lakini napenda upinzani wa kujenga nchi yetu.
 
Woga umewafanya wakafika hapo walipofika. Wameogopa kusulibiwa na chama chao, kama wasaliti. Ninavyoona, ni bora wangekubali kusulibiwa kwa kusimamia ukweli. Tungewaona wa maana kama wangekisimamia walichokisema kwa vitendo. Woga ni udhaifu mbubwa sana, na hauwezi ukamfanya mwanadamu akafanikiwa kwa lolote. kwa hiyo kuogopa kwao ndio kufeli kwao!
 
Back
Top Bottom