Wabunge wa CCM wacharuka kuhusu serikali kutaka kukata mafao yao

Emma.

JF-Expert Member
Jun 25, 2012
19,935
5,558


Heshima kwenu Wana JF.

Wabunge wa CCM leo bungeni wameicharukia serikali kuhusu mpango wa serikali wa kutaka kukata mafao yao

Wabunge wa chama cha mapinduzi CCM wamezungumza kwa hisia kali walipokuwa wakipinga hatua ya serikali kutaka kuwakata kodi kwenye yao watapokamaliza kazi ya ubunge mwaka 2020.

Wabunge hao wamesema hawatakubali kuona wanakatwa kodi ya mafao yao na serikali walipokuwa wakichangia mjadala bungeni wa kupitisha Bajeti kuu ya serikali kwa mwaka wa fedha 2016-2017 ,mjini dodoma .

Mbunge wa Mwibara Kangi anasema -Kila mwenzi tunakatwa kodi ya mapato alafu mafao yetu na yenywe yakakatwe kodi?mnataka turudi mtaani alafu muanze tena kutucheka .Lazima wabunge tulinde maslahi yetu hatuwezi kukubali .

Hawa ndo wabunge wamechaguliwa na wananchi wanakwenda bungeni kutetea maslahi yao?
 

Attachments

  • Screenshot_2016-06-10-18-11-45.png
    Screenshot_2016-06-10-18-11-45.png
    250.8 KB · Views: 103
Sasa mbona na wao walipitisha wafanyakazi wasichukue mafao yao pindi wakiacha kazi mpaka wafikishe 55yrs? wabunge waliopitisha ni wanafiki mbona wao kukatwa tu wanatoa povu inabidi na wao wasichukue mpaka wafikishe 55yrs kwa wasiofika na kwale waliofika ikatwe kodi tu.
 
Mungu wangu, wanasahau kuwa ni wao walipitisha wastaafu wakatwe kodi kutoka kwenye mafao toka mifuko ya hifadhi ya jamii.
Waone aibu jamani, kwanini wanajipigania wao tu na sio wapiga kura wao?
Mstaafu anakatwa kodi kwenye mafao na sheria hii wakati inaletwa wafanyakazi walilalamika kweli lakini hakuna aliyewatetea na Leo linakuja kwao linakuws chungu - Magufuli kaza kamba.
 
Uyo Kangi haaminiki kama Kanga(ndege) mjamzito anashati la kijani huku moyo wake unatamani gwanda RIP filikunjombe
 
Heshima kwenu Wana JF.

Wabunge wa CCM leo bungeni wameicharukia serikali kuhusu mpango wa serikali wa kutaka kukata mafao yao
Wabunge wa chama cha mapinduzi CCM wamezungumza kwa hisia kali walipokuwa wakipinga hatua ya serikali kutaka kuwakata kodi kwenye yao watapokamaliza kazi ya ubunge mwaka 2020.
Wabunge hao wamesema hawatakubali kuona wanakatwa kodi ya mafao yao na serikali walipokuwa wakichangia mjadala bungeni wa kupitisha Bajeti kuu ya serikali kwa mwaka wa fedha 2016-2017 ,mjini dodoma .
Mbunge wa Mwibara Kangi anasema -Kila mwenzi tunakatwa kodi ya mapato alafu mafao yetu na yenywe yakakatwe kodi?mnataka turudi mtaani alafu muanze tena kutucheka .Lazima wabunge tulinde maslahi yetu hatuwezi kukubali .
Hawa ndo wabunge wamechaguliwa na wananchi wanakwenda bungeni kutetea maslahi yao?
Ila wabunge wa upinzani wameunga mkono hoja kwa Moyo wa dhati.
 
Uyo Kangi haaminiki kama Kanga(ndege) mjamzito anashati la kijani huku moyo wake unatamani gwanda RIP filikunjombe
Duh wabunge wa CCM kwenye kutozwa kodi ya mafao hapo wamesema hawatokubali ngoja tuone kama serikali wataitoa kwa kuogopa wabunge wa CCM
 
Back
Top Bottom