Toosweet
JF-Expert Member
- May 27, 2012
- 2,141
- 1,982
Heshima Kwenu,
Baadhi ya wabunge wa CCM wameonekana kumpigia kampeni za chinichini aliyekuwa mgombea ubunge kstika jimbo la Longido (CCM),Dr. Steven Kiruswa kwenye Uchaguzi Mkuu wa 2015 mbele ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa aliyekwenda kuweka jiwe la msingi kwenye mradi wa maji wa Longido.
Junk 29,2016 Mahakama Kuu Kanda ya Arusha ilitengua ushindi wa mbunge wa Longido, Onesmo Ole Nangole (CHADEMA) na sasa Tume ya Taifa ya Uchaguzi(NEC) inasubiriwa kutangaza kuwa jimbo liko wazi na tarehe ya uchaguzi.
Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Arusha (CCM),Catherine Magige alitumia nafasi ya kusalimia wananchi aliyopewa na mkuu wa mkoa huo, Mrisho Gambo kumtambulisha Dr. Kiruswa na kusema amekuwa akimtuma Bungeni kuzungumzia matatizo ya Longido.
"Yale ambayo nimekuwa nikiyazungumza bungeni kuiomba serikali, huyu hapa (akimwonyesha) Dr. Kiruswa ndiyo alikuwa ananiambia, kila siku ananisumbua kwenye simu. Yeye hakushinda ubunge lakini anatekeleza ilani ya Chama Cha Mapinduzi kupitia mimi, " alisema Magige.
Mwananchi.
Hoja:Kulikuwa na ulazima wa Mkuu wa Mkoa kualika mbunge asalimie wananchi kikampeni kwenye shughuli ya Serikali?
Kwani Longido haikuwa na mbunge mpaka Magige atumwe bungeni na Kiruswa?
Kiruswa hana mamlaka ya kutuma mtu wa kumwakilisha bungeni wakati yeye si mbunge.
NEC fuatilieni hii habari.
Baadhi ya wabunge wa CCM wameonekana kumpigia kampeni za chinichini aliyekuwa mgombea ubunge kstika jimbo la Longido (CCM),Dr. Steven Kiruswa kwenye Uchaguzi Mkuu wa 2015 mbele ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa aliyekwenda kuweka jiwe la msingi kwenye mradi wa maji wa Longido.
Junk 29,2016 Mahakama Kuu Kanda ya Arusha ilitengua ushindi wa mbunge wa Longido, Onesmo Ole Nangole (CHADEMA) na sasa Tume ya Taifa ya Uchaguzi(NEC) inasubiriwa kutangaza kuwa jimbo liko wazi na tarehe ya uchaguzi.
Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Arusha (CCM),Catherine Magige alitumia nafasi ya kusalimia wananchi aliyopewa na mkuu wa mkoa huo, Mrisho Gambo kumtambulisha Dr. Kiruswa na kusema amekuwa akimtuma Bungeni kuzungumzia matatizo ya Longido.
"Yale ambayo nimekuwa nikiyazungumza bungeni kuiomba serikali, huyu hapa (akimwonyesha) Dr. Kiruswa ndiyo alikuwa ananiambia, kila siku ananisumbua kwenye simu. Yeye hakushinda ubunge lakini anatekeleza ilani ya Chama Cha Mapinduzi kupitia mimi, " alisema Magige.
Mwananchi.
Hoja:Kulikuwa na ulazima wa Mkuu wa Mkoa kualika mbunge asalimie wananchi kikampeni kwenye shughuli ya Serikali?
Kwani Longido haikuwa na mbunge mpaka Magige atumwe bungeni na Kiruswa?
Kiruswa hana mamlaka ya kutuma mtu wa kumwakilisha bungeni wakati yeye si mbunge.
NEC fuatilieni hii habari.