Sooth
JF-Expert Member
- Apr 27, 2009
- 3,928
- 5,615
Ktk picha hii (kwa hisani ya Mjengwa), wabunge wa bunge la JMT wakipata kifungua kinywa leo asubuhi, uwanja wa ndege JKNIA DSM baada ya kutoka Malaysia kuichunguza na kubaini uwezo wa kampuni iliyopewa dhamana ya kutengeneza vitambulisho ya nchini malaysia-IRIS. Wanadai kampuni ina uwezo mzuri na imefanya kazi nchi mbalimbali, kwa hiyo tusiwe na wasiwasi.
Mimi najiuliza maswali mawili: Kwanin ubalozi wetu huko malaysia haukutumika kwa hili mpaka ikalazimu wabunge waende(hapa lengo ni kupunguza gharama)? Pili, kweli wabunge wetu wana 'utaalamu' wa kuchunguza uwezo wa kampuni kwa siku kadhaa na sio 'waambata' waliopo ubalozini? Msingi wa hoja yangu ni kujaribu kupunguza gharama kwa upande wa serikali, ili sekta zenye uhitaji zaidi ziweze kupata fedha za kutosha.