Wabunge CCM wamsafisha Lowassa.

Wabunge CCM wamsafisha Lowassa.

Msafisheni tu kwenye vikao vyenu, lakini kwa wananchi huku sisi bado ni mchafu sana, hata akioga kwa jiki hatakati katu katu!
 
jaman msipoteze muda wenu! ni simple! lowassa kasafishwa na wabunge wa ccm, bungeni! lakini si kwa wananchi! sasa mwacheni atapigiwa kura na wabunge hao wa ccm! na si wananchi! ss tuangalieni olimpic kwa raha wala wasitupe presha.
 
Richmond ilikuwa mradi wa mapacha watatu (Kikwete, Lowasa,Rostam) km kifuta jasho baada ya kutumia pesa nyingi kuingia ikulu. Kuna watu wanasema hawa mapacha walikuwa na mpango mbaya sn na nchi hii eti walikuwa wanafidia pale mwalimu nyerere alipowabania.

Nasikia walipiga hesabu kiasi walichokuwa wamepoteza baada ya nyerere kuwabania kuwa viongozi wakuu kwa hiyo walikuwa wamejidhatiti kuikamua nchi na kwa kuanzia ndiyo waanzisha kampuni feki ya richmond na kujichotea Tsh.155,000,000 kila siku iendayo kwa mungu.

Haya hayatakuja kuisha vichwani mwa watz.
 
Watamsafisha wao lakini kwetu sisi wananchi wa Tanzania Lowasa ni Mchafu Mchafu Mchafu X 1000
 
Sakata hilo, lilibuka juzi usiku, katika kikao cha Wabunge wa CCM, ambacho kilikuwa kinajadili tatizo la umeme, hali iliyomfanya Mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka (CCM), kuibuka na na hoja ya kutaka viongozi wa wizara hiyo wawajibishwe.
Hoja ya Sendeka, ilimlenga Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo na Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Eliakim Maswi, wawajibishwe kwa kukiuka Sheria ya Manunuzi ya Umma....

Kama wamegundua 2008 walimtosa EL kwa makosa basi wawe na courage waandae hoja waipeleke bungeni rasmi kumsafisha EL, umma mpaka leo unajua EL alitenda makosa kwa nini wasimsafishe hadharani!?
 
Sakata hilo, lilibuka juzi usiku, katika kikao cha Wabunge wa CCM, ambacho kilikuwa kinajadili tatizo la umeme, hali iliyomfanya Mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole Sendeka (CCM), kuibuka na na hoja ya kutaka viongozi wa wizara hiyo wawajibishwe.
Hoja ya Sendeka, ilimlenga Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo na Katibu Mkuu wa wizara hiyo, Eliakim Maswi, wawajibishwe kwa kukiuka Sheria ya Manunuzi ya Umma.....

Hizi ndo siasa za bongo bana!. Kutoka fisadi hadi mtu safi, tulifanya makosa, na baada ya muda si mwingi tutasikia "UTUSAMEHE MZEE HIZI NDO SIASA MBOFUMBOFU ZA KIBONGO"
 
lowasaa ANAWEZA but lowassa siyo msafi kama ambavyo wewe pia siyo msafi.....

Lakini anaweza kufanya kazi vizuri sana akadeliver......kwangu mimi bora uniibie lakini unazalisha, pengine hata kwa ziada. Yanifaa nini kama wewe ni mwaminifu asilimia mia but uwezo wako wa uzalishaji na mdogo au haupo?

The worse scenario ni pale mtu au kiongozi anapokuwa haweza kuzalisha kabisa lakini vile vile ni fisadi.......damn

lowassa come on board.....unaweza unaweza sana kuongoza hata kama wewe si msafi!
 
ni kazi ngumu lakini mungu awatangulie, kila la heri
 
Back
Top Bottom