Huu ni utumbo mtupu kwani hawa wabunge wote wapo kwa maslahi yao wenyewe na si ya wananchi, hii ni janja yao tu ya kutaka kupata umaarufu katika kipindi hiki cha uchaguzi.....tutaona na kusikia mengi
Imani ya hawa jamaa kukitema chama chao cha majambazi ilinitoka pale Mr Six aliposhindwa kuwatupia kadi yao aliposulubiwa na kina Makamba.
Awali niliamini na kutamani sana Sitta kuwarudishia kadi yao mara baada ya kumjadili na kumtishia kumvua uanachama, kisha tungeshuhudia wabunge wengine toka chama hicho wakimfuata kwa kurudisha kadi zao, ni hatua ambayo ingesisimua na kuwavutia zaidi wananchi, wangeamini kile wanachokihubiri Bungeni, lakini hilo halikutokea, wataweza sasa kujiengua
kuundwa kwa chama kingine si suluhisho la matatizo ya watanzania. kuna tatizo sugu ambalo sisi kama watanzania linatuzunguka ambalo ni haki zetu za kimsingi, wengi watapiga kelele lakini ifikapo mda wa kwenda kupiga kura wanaingia mitini. Tuache bla bla jamani.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.