Wabunge 128 wanafaida gani kwa nchi?

Wabunge 128 wanafaida gani kwa nchi?

HIMARS

JF-Expert Member
Joined
Jan 23, 2012
Posts
73,250
Reaction score
103,369
Kwenye Bunge la Tanzania kuna wabunge 393 ambapo wabunge 264 ni wa kuchaguliwa, yaani wana majimbo, wabunge 113 hawa ni kundi maalumu kwa wanawake tu, kuna wabunge 5 kutoka Zanzibar, kuna wabunge 10 wanaoteuliwa na Rais na kuna Mwanasheria Mkuu wa Serikali, swala langu ni kwa hawa wabunge 128.

Hivi Tanzania tulilogwa na nani? Kwanini tuwe na kundi kubwa lisilowakirisha jimbo lolote?

Wabunge 128 wanakula pesa za Watanzania ambazo zingetumika katika kufanya mambo ya msingi. Kwanini wabunge kutoka Zanzibar waingie bunge letu wakati sisi hatuko kwao?

Kwanini Rais ateue wabunge 10 wasio na majimbo? Je, hatuoni kuwa hawa kwa sehemu kubwa wanasababisha gharama za uendeshaji?

Wabunge hao 128 kwa asilimi 90 hawana mchango wa maana bungeni, mf. Salma Kikwete, yule mama Mwenyekiti wa Bunge na wengine wengi.

Hebu tufikirie tulikosea wapi na tuondoe haya mambo, au tuvumilie?
 
Sina mengi ya kusema zaidi ya kusema aliyeturoga kafa.
 
Sioni tija ya bunge zaidi ya kukamilisha vifungu vya katiba tu.
 
Tulikofikia hii nchi sasa tugawane mbao Ili kila mtu achukue chake.

Tunapotezeana Muda sasa.
 
Genge la kupeana ulaji tu hakuna kingine, yaani mwenye nchi akimkumbuka mshkaji wake walisoma wote Tabora Boys anampa nafasi akapige meza na kupata mshiko.

Kifupi katiba inampa raisi nafasi kubwa ya kuweka watu wake kuanzia wabunge, wakuu wa mikoa, wilaya, wakurugenzi...the list I endless!
 
Futa hao viti maalum wote
 
hata hao waliopo 393hawana faida zaidi ya kupanda v8 na kupiga sarakasi bungeni na kupitishi tozo za hovyo kwa wananchi
 
Na bado wanataka kuongeza majimbo kama huko Mbeya ili iwe mzigo kwa Wananchi badala ya kupunguza gharama wao wanataka kuongeza tuu wanatamani wawepo wabunge 1000 kwa sababu ya uvivu wa kufanya kazi ili walipwe pesa za bure tuu na posho za Vikao...wakiwa huko utawasikia vijana wanaomaliza vyuo wajiajiri...
 
Kwenye Bunge la Tanzania kuna wabunge 393
Ambapo
Wabunge 264 ni wa kuchaguliwa, yaani wana majimbo

Wabunge 113 hawa ni kundi maalumu kwa wanawake tu

Kuna wabunge 5 kutoka Zanzibar

Kuna wabunge 10 wanaoteuliwa na Rais

Kuna Mwanasheria Mkuu wa Serikali

Swala langu ni kwa hawa wabunge 128

Hivi Tanzania tulilogwa na nani?

Kwanini tuwe na kundi kubwa lisilowakirisha jimbo lolote?

Wabunge 128 wanakula pesa za Watanzania ambazo zingetumika katika kufanya mambo ya msingi.

Kwanini wabunge kutoka Zanzibar waingie bunge letu wakati sisi hatuko kwao?

Kwanini Rais ateue wabunge 10 wasio na majimbo

Je hatuoni kuwa hawa kwa sehemu kubwa wanasababisha gharama za uendeshaji?

Wabunge hao 128 kwa asilimi 90 hawana mchango wa maana bungeni mf Salma Kikwete, yule Mama mwenyekiti wa Bunge na wengine wengi

Hebu tufikirie tulikosea wapi na tuondoe haya mambo

Au tuvumilie?
Mama Salma Kikwete ni mbunge wa Jimbo la Mchinga-Lindi.......acha husda.
 
Suluhisho la haya ni Mungu tu..(daniel 2:44)
 
Back
Top Bottom