Wabeba lawama tukutane hapa!

Wabeba lawama tukutane hapa!

Wakuu bila shaka ni wazima, bila shaka wote tunaelewa maisha yalivyojaa changamoto za kila aina.
Kuna watu ni wepesi kueleza yale yanayowasibu, ila kuna akina sisi ambao huwa tunakufa na tai shingoni!

Kifupi kwa upande wangu sina maisha hayo ambayo ndugu na jamaa wanayafikiria, lakini lawama zimekuwa haziishi kwamba sina msaada wowote kwao ihali mwanzo nilikuwa nawapiga tafu pale inapowezekana.

Hapa karibuni kuna hali imenishtua unakuta mtu mzima tena mwanaume, mkizoena kidogo tu anataka umpe hela, mi huwa najiuliza mbona mimi huwa napambana na ya kwangu mwenyewe, hawa wanaahindwa vipi, na sio kwamba mtu anataka kukopa hapana anataka apewe bure bure tu.

Ukimwambia pengine na wewe una hali mbaya basi urafiki unaishia hapo, ananuna na hautamuona tena. Vipi nyie mnakabiliana vipi na hawa watoa lawama, maana kuna muda huwa nakuta wananivuruga kabisa, tena kipindi hicho unakuta na mimi mambo yangu mengi hayaendi kabisa.
Bora lawama mkuu kuliko kusaidia watu ambao hawana msaada na wewe maana ukijifanya mwema sana kwa kuwasaidia mwisho wa siku ni ngumu kumridhisha binadamu akaridhika na utaishi maisha yasiokuwa na furaha milele
 
Back
Top Bottom