Mrembo wee msikilize anataka nini then wewe ni mtu mzima utaamua cha kufanya.
Nililetewa the same case juzi eti kuna libaba liliita nikakimbia,mwhy ukimbie simama msikilize shida yake kama hauko tayari kumsadia achana nae.
Ushauri wangu ni kwamba sidhani kama mume anapaswa kufahamu hayo mambo maana sisi wanaume tunajijua wenyewe kugombana huwa hatuchelewi kabisa sasa wewe muangalie mwenendo wake utapata jibu
Maana mnafukua fukua tu hizi mada za zamani enzi JF ikiwa sehemu ya uhakika wa kupata habari motomoto toka jikoni, enzi Le Mutuz akiwa mzee wa Sauti Ya Umeme kabla ya wabebz kumchanganya, enzi mzee Kyoma akiwa active member (nayamisi sana mawe yake huyu jamaa), enzi Yo Yo akiwa anataka umaarufu kupitia mgongo wa wenu mtiifu (NN).....
Those were the platinum days that I miss something fierce.
we unafikiri kwanini anasema anasita kunipigia simu? na kama ni maswala mengine, sisi ni majirani na yupo free kunitembelea nyumbani kama ilivyo kawaida.
kama kamuona mumeo ni mchepukaji sasa anakuonea huruma anataka kukuambia ila pia anasita kwakuhofia matokeo baada ya taarifa?usiwaze sana kutongozwa kubali wito kataa maneno
dalili ya mvua hiyo .. mjibu tu .. kumbe hii ni namba yako basi nashukuru kwani umempunguzia mume wangu kazi kwani jana tu alizungumzia kukufuata ili akuombe namba yako .. basi nitampatia hii message aisome kabisa .. ubarikiwe
'hujambo xxx. ninayo simu yako mda mrefu lakini kila nikitaka kipiga nasita. mimi ni YYYY' hii message imetoka kwa mme wa jirani yangu ambaye familia yangu na yake zinaheshimiana sana na ni marafiki wakubwa. Sasa hii message aliyonitumia imenichanganya. najiuliza maswali mengi, je ana nia gani?? mimi bado sijaijibu lakini nawaza je inawezekana hana nia mbaya?
Wana JF naomba msaada wa mawazo.