Yawezekana ama kweli wameanguka kisiasa au ni mchezo wa kuigiza. Vyovyote ilivyo, kuna mabadiliko katika maisha yao ya kisiasa na kiuchumi na uwezo wao wa kuwezesha mawakala wao wa kisiasa na kiuchumi.
Ni wazi, kuna wapambe wao wengi ndani ya chama tawala, upinzani na serikalini. Baadhi yao naamini walikuwa kipato chao pekee kinatokana na ukuwadi wao, uvuvuzela, kunusa taarifa na pengine kushulikia adui.
Baada ya mabadiliko yaliyofanywa ngazi ya juu ya ccm, naamini kwamba maisha na kipato cha hawa wapambe vitafifia. Baadhi wanaweza kuwa jobless (mfano, kuna watu tayari wameaga hapa janvini na wengine wanaonekana kubadili falsafa zao)
Je tunaweza kukisia ni watu wangapi wameathirika na mabadiliko haya na ni kwa kiwango gani? Je sasa nchi itatawalika?