Vyuo Vikuu visiwe chini ya Wizara ya Elimu

Vyuo Vikuu visiwe chini ya Wizara ya Elimu

Wakusoma 12

JF-Expert Member
Joined
Jul 3, 2017
Posts
5,151
Reaction score
14,490
Kwanza wizara ya elimu inapaswa ijishughulishe na maswala ya elimu ya msingi, secondary na taaluma za kielimu kama vyuo vya elimu na vyuo vya kati.

Elimu ya juu inapaswa kusimamiwa na taasisi ya maswala ya elimu ya juu pekee. Kipindi cha rais Mkapa pamoja na JK tulikuwa na wizara ya elimu ya juu. Elimu ya juu kuendeshwa sawa na shule za msingi ni tusi kwa wanataaluma na watafiti nchni.

Leo wizara ya elimu inajiamulia tu kufuta udahili kwa baadhi ya programu kwa sababu wao hawaitakii ama hawazijui zinahusu nini. Elimu haina programu isiyo na maana hata siku moja, programu zote zimefanyiwa tafiti na kukubaliwa ziwepo.

Kuna programu na associate programu sasa hawa watu wa wizara ya elimu wanajiamulia tu kusema programu hizi na ile mwaka huu usidahili, jambo ambalo linaweza kupelekea wanafunzi wanaoendelea kwenye programu husika waone kama wamepotea kumbe ni mawazo ya afisa mmoja tu ambaye alisoma kuanzia grade A akaunga unga mpaka akawa daktari wa soshiolojia.
 
Hayo madude ya yaliyofutwa hayana tija ,hii ni akili simple kabisa hata sheria ni masomo ya kufutwa hayana maana ..Sheria ni zetu .
 
Elimu haina programu isiyo na maana hata siku moja, programu zote zimefanyiwa tafiti na kukubaliwa ziwepo.
Naona yale ya Commerce & Book Keeping kuwekwa somo moja na Biology & Chemistry kuwekwa somo moja yanaanza kujirudia, kurahisisha rahisisha mambo
 
Hayo madude ya yaliyofutwa hayana tija ,hii ni akili simple kabisa hata sheria ni masomo ya kufutwa hayana maana ..Sheria ni zetu .
Hayana tiba kivipi kwa utafiti upi? Inazuia udahili wa kozi kama sheria, saikolojia na elimu kisa hayana tija kwako
 
Hayana tiba kivipi kwa utafiti upi? Inazuia udahili wa kozi kama sheria, saikolojia na elimu kisa hayana tija kwako
Sheria na saikolojia ,elimu hazina future ukweli usemwe ..Wako sahihi ,sheria inasaidia nn zaidi ya kuzalishwa wakariri vifungu .
 
Technically vyuo vikuu vinatakiwa kuwa independent kwa kila kitu ili viweze kuwa na mchango sahihi tazama dunia nzima! Hivi vyetu vinavyopangiwa mtaala na masisiemu lazima vitengeneze kizazi cha chawa watukuka!
Ukishakuwa CHADEMA unakuwa mwehu
Taja nchi moja tu duniani ambayo vyuo vikuu huwa independent havina usimamizi wa taasisi nyingine
 
Sheria na saikolojia ,elimu hazina future ukweli usemwe ..Wako sahihi ,sheria inasaidia nn zaidi ya kuzalishwa wakariri vifungu .
Dah kijana unajianika hovyo kabisa, na kuonyesha utupu 😀
Najitolea kukujibu katika ufinyu huo huo wa mifano yako. Sheria ni somo pana, linasaidia katika mambo ya utaratibu, haki, uhuru na usalama.

Bila sheria we mTanga tutakuwekea mafuta ya nguruwe katika mafuta ya kupikia na unaweza kujua na usifanye chochote. Biashara zinalindwa na sheria, umesema wanakariri vifungu... ndio nikweli lakini pia wanasaidia kutoa ufafanuzi, mafano wewe Feisal Salum Myanga unajua kusoma na kuandika lakini mktaba tu uliosukwavizuri unaweza kukuingiza Matatizoni, kisha ukaanza kulia vilio visivyo na mantiki kama kulishwa ugali na chumvi,

Saikolojia ni somo kubwa na muhimu sana hitaji lake mojawapo haraka haraka ni pamoja na kusaidia kujua tabia za binadamu na mienendo ya kiakili/ufikiriaji. Wataalamu wa saikolojia wanahitajika sehemu nyingi sana hospitali na mpaka katika biashara.

Wakati mwingine google kwanza kabla haujaponda kazi au fani ambazo zimefanyiwa utafiti wa kina na wataalamu mkuu.
 
Dah kijana unajianika hovyo kabisa, na kuonyesha utupu 😀
Najitolea kukujibu katika ufinyu huo huo wa mifano yako. Sheria ni somo pana, linasaidia katika mambo ya utaratibu, haki, uhuru na usalama.

Bila sheria we mTanga tutakuwekea mafuta ya nguruwe katika mafuta ya kupikia na unaweza kujua na usifanye chochote. Biashara zinalindwa na sheria, umesema wanakariri vifungu... ndio nikweli lakini pia wanasaidia kutoa ufafanuzi, mafano wewe Feisal Salum Myanga unajua kusoma na kuandika lakini mktaba tu uliosukwavizuri unaweza kukuingiza Matatizoni, kisha ukaanza kulia vilio visivyo na mantiki kama kulishwa ugali na chumvi,

Saikolojia ni somo kubwa na muhimu sana hitaji lake mojawapo haraka haraka ni pamoja na kusaidia kujua tabia za binadamu na mienendo ya kiakili/ufikiriaji. Wataalamu wa saikolojia wanahitajika sehemu nyingi sana hospitali na mpaka katika biashara.

Wakati mwingine google kwanza kabla haujaponda kazi au fani ambazo zimefanyiwa utafiti wa kina na wataalamu mkuu.
Kama ulichoandika hapa ,basi ni matokeo ya ujinga ...Eti biashara zinalindwa na sheria ,nyokooo!

Watu walipokuwa wanafanya barter trade hizo sheria zenu za wazungu zilikuwa wapi ?.Weka mafuta ya Nguruwe uyalete Tanga uone balaa lake ..

Biashara zote za sasa ni utapeli ,mifumo ya bank, mambo ya bima ,yote ni utapeli...Sheria na saikolojia zinazalisha wanaokariri tu basi kama wewe.
 
Back
Top Bottom