Vyuo Vikuu Nchini kudahili Wanafunzi sawa na walioshinda Mtihani wa Kidato cha IV: Nani aliuharibu Mfumo wa Elimu?

Mgambilwa ni mntu

JF-Expert Member
May 30, 2017
2,869
3,188
Kwa muda sasa, kumekuwepo kelele nyingi za Wadau wa Elimu nchini juu ya kuzorota kwa Mfumo wa Elimu wa Tanzania lakini kelele hizi zimesikika sana hasa katika Awamu ya V ya Rais John Pombe Magufuli. Kwa haraka haraka, unaweza ukaingia kwenye mkumbo wa kudhani, Sera za sasa za Serikali ya Awamu ya Tano, ndizo zimeifikisha hapa elimu ya Tanzania. Wengi wamekuwa wakiinyoshea Sera ya Elimu Msingi Bila Malipo kuwa, ndio chanzo cha kuporomoka kwa elimu ya Tanzania.
Hata hivyo, mi naona kelele zimekuwa nyingi baada ya Serikali kuboresha kwa kiwango kikubwa shule zake, ikiwemo kuondoa karo na hivyo kuvutia wazazi wengi kuhamishia watoto wao katika shule za umma kutoka shule binafsi na hivyo kuathiri sana sekta binafsi hasa katika kipindi hiki cha kupaka vyuma grisi. Je, kushuka kwa elimu kuhusishwe na Rais John Pombe Magufuli, ama a Magufuli ndiye anayeitoa shimoni na hivyo kuwawafumbua macho Watanzania, juu ya jinsi elimu yetu ilikuwa imeshadharaulika?
Jibu: Kwa kawaida, Mfumo wa Elimu kwa dunia nzima, umetengenezwa katika umbo la Pyramid kuanzia chini hadi juu Killeen, ambapo wanafunzi huanza wakiwa wengi na kadri madarasa yanavyopanda ndivyo pia idadi ya wanafunzi hushuka. Hivyo, wanafunzi wa shule za msingi huwa wengi kuliko wale wa shule za sekondari, kama ambavyo nao ni wengi kuliko wa vyuo vikuu.

Hata hivyo, kwa Tanzania, kuna sehemu kama Nchi tuliamua kujichanganya wenyewe na kuiacha hiyo kanuni kwa kuendekeza kupanua magoli na hivyo kuruhusu wenye ufaulu mdogo kuchaguliwa kwenda chuo kikuu. Tumeruhusu kuwepo kwa utitiri wa Vyuo Vikuu vya Private vinavyodahili wanafunzi waliopata hadi Principals za D. Hao watu wakimaliza Vyuo, ndio huwa wa kwanza kupata kazi kwani huwa tayari kuhonga wakijua hawakuwa na sifa kama za wenzao. Hali hiyo huwaacha vipanga wakirandaranda mitaani bila ajira.
Mfano: Kwa mwaka 2018, Tanzania ina wanafunzi wanaotarajiwa kufanya Mtihani wa STD IV - 1,609,000; Mtihani wa Std. VII - 965,000; Mtihani wa Kidato II - 547,000; Form IV - 440,000; na Form VI - 80,000 (wameshafanya).
Ajabu ni kuwa, mwaka 2014, jumla ya Watahiniwa 196,805 (68%) walifaulu Mtihani wa Kidato cha IV, kati ya Watahiniwa 235,227 waliofanya Mtihani huo. Hata hivyo, ni Watahiniwa 73,832 pekee, sawa na asilimia 30% ndio waliopata madaraja ya: distinction, merit na credit.
Wanafunzi hao 73,800 ni miongoni mwa Wahitimu 75,116 waliofanya Mtihani wa Kidato cha VI mwaka 2017, ambapo wanafunzi 58,556 sawa na asilimia 93%, walifaulu Mtihani huo.
Kama asilimia 93% wanafaulu Mtihani, kuna haja gani ya Mtihani huo? Na in fact, hao ni waliopata I - III lakini ukijumlisha na wale waliopata ushindi wa Division IV (huwa wanaenda vyuo vya diploma), utakuta possibly asilimia 99% ya Watahiniwa wa Mtihani wa Kidato cha VI, hufaulu.
So, huo ni Mtihani? Je, hatujicheleweshi tu sisi wenyewe bila kujua? Chanzo cha kupunguza point za kujiunga na chuo ni nini? Mlitaka wote waende Chuo Kikuu?
Mchawi amejificha hapo. Vyuo vikuu vilitaka hela za mikopo na zikawa tayari kudahili wanafunzi wenye makisi za chini. Haiwezekani wanafunzi wanaotoka stage moja ya kielimu kwenda nyingine wawe wengi (40,000 wa Mwaka wa Kwanza watakaopata mkopo - 2018) kuliko ambao hawakuchaguliwa kwenda Vyuo vikuu (58,000 - 40,000 = 18,000) Chukua tena hao 18,000 utoe wanachuo ambao hawakuomba/Hawatapata mkopo, utapata ambao hawakwenda Chuo Kikuu.
Hiyo inamaanisha wanaoingia kusoma kazi za utaalamu wa kati (diploma) ni around 10,000 pekee. Hapa ndipo kuna tatizo.

IMG_4098.jpg IMG_4099.jpg IMG_4100.jpg
 
Naamini tupo na wadau wa elimu humu, Mlinga mzee wa Wazir wa masifuri,eatatuambia kama elimu imeahuka au imepanda ....
 
Kwa muda sasa, kumekuwepo kelele nyingi za Wadau wa Elimu nchini juu ya kuzorota kwa Mfumo wa Elimu wa Tanzania lakini kelele hizi zimesikika sana hasa katika Awamu ya V ya Rais John Pombe Magufuli. Kwa haraka haraka, unaweza ukaingia kwenye mkumbo wa kudhani, Sera za sasa za Serikali ya Awamu ya Tano, ndizo zimeifikisha hapa elimu ya Tanzania. Wengi wamekuwa wakiinyoshea Sera ya Elimu Msingi Bila Malipo kuwa, ndio chanzo cha kuporomoka kwa elimu ya Tanzania.
Hata hivyo, mi naona kelele zimekuwa nyingi baada ya Serikali kuboresha kwa kiwango kikubwa shule zake, ikiwemo kuondoa karo na hivyo kuvutia wazazi wengi kuhamishia watoto wao katika shule za umma kutoka shule binafsi na hivyo kuathiri sana sekta binafsi hasa katika kipindi hiki cha kupaka vyuma grisi. Je, kushuka kwa elimu kuhusishwe na Rais John Pombe Magufuli, ama a Magufuli ndiye anayeitoa shimoni na hivyo kuwawafumbua macho Watanzania, juu ya jinsi elimu yetu ilikuwa imeshadharaulika?
Jibu: Kwa kawaida, Mfumo wa Elimu kwa dunia nzima, umetengenezwa katika umbo la Pyramid kuanzia chini hadi juu Killeen, ambapo wanafunzi huanza wakiwa wengi na kadri madarasa yanavyopanda ndivyo pia idadi ya wanafunzi hushuka. Hivyo, wanafunzi wa shule za msingi huwa wengi kuliko wale wa shule za sekondari, kama ambavyo nao ni wengi kuliko wa vyuo vikuu.

Hata hivyo, kwa Tanzania, kuna sehemu kama Nchi tuliamua kujichanganya wenyewe na kuiacha hiyo kanuni kwa kuendekeza kupanua magoli na hivyo kuruhusu wenye ufaulu mdogo kuchaguliwa kwenda chuo kikuu. Tumeruhusu kuwepo kwa utitiri wa Vyuo Vikuu vya Private vinavyodahili wanafunzi waliopata hadi Principals za D. Hao watu wakimaliza Vyuo, ndio huwa wa kwanza kupata kazi kwani huwa tayari kuhonga wakijua hawakuwa na sifa kama za wenzao. Hali hiyo huwaacha vipanga wakirandaranda mitaani bila ajira.
Mfano: Kwa mwaka 2018, Tanzania ina wanafunzi wanaotarajiwa kufanya Mtihani wa STD IV - 1,609,000; Mtihani wa Std. VII - 965,000; Mtihani wa Kidato II - 547,000; Form IV - 440,000; na Form VI - 80,000 (wameshafanya).
Ajabu ni kuwa, mwaka 2014, jumla ya Watahiniwa 196,805 (68%) walifaulu Mtihani wa Kidato cha IV, kati ya Watahiniwa 235,227 waliofanya Mtihani huo. Hata hivyo, ni Watahiniwa 73,832 pekee, sawa na asilimia 30% ndio waliopata madaraja ya: distinction, merit na credit.
Wanafunzi hao 73,800 ni miongoni mwa Wahitimu 75,116 waliofanya Mtihani wa Kidato cha VI mwaka 2017, ambapo wanafunzi 58,556 sawa na asilimia 93%, walifaulu Mtihani huo.
Kama asilimia 93% wanafaulu Mtihani, kuna haja gani ya Mtihani huo? Na in fact, hao ni waliopata I - III lakini ukijumlisha na wale waliopata ushindi wa Division IV (huwa wanaenda vyuo vya diploma), utakuta possibly asilimia 99% ya Watahiniwa wa Mtihani wa Kidato cha VI, hufaulu.
So, huo ni Mtihani? Je, hatujicheleweshi tu sisi wenyewe bila kujua? Chanzo cha kupunguza point za kujiunga na chuo ni nini? Mlitaka wote waende Chuo Kikuu?
Mchawi amejificha hapo. Vyuo vikuu vilitaka hela za mikopo na zikawa tayari kudahili wanafunzi wenye makisi za chini. Haiwezekani wanafunzi wanaotoka stage moja ya kielimu kwenda nyingine wawe wengi (40,000 wa Mwaka wa Kwanza watakaopata mkopo - 2018) kuliko ambao hawakuchaguliwa kwenda Vyuo vikuu (58,000 - 40,000 = 18,000) Chukua tena hao 18,000 utoe wanachuo ambao hawakuomba/Hawakupata mkopo, utapata ambao hawakwenda Chuo Kikuu.
Hiyo inamaanisha wanaoingia kusoma kazi za utaalamu wa kati (diploma) ni around 10,000 pekee. Hapa ndipo kuna tatizo.

View attachment 799537 View attachment 799538 View attachment 799540
nimekupata bro. mi nadhani tusilazimishe wanafunzi waende chuo kikuu,

tuwe na mfumo mzuri wa elimu ambao utawachukua na kuwaendeleza wale ambao hawajafikia alama za ufaulu kwenda sekondari,

tuwekeze kwenye vocation training, tuwe na vocation centers nyingi, labda moja kila kata

ukiweza kuanzisha vocation trainining utawapa ujuzi vijana wa kupambana na mazingira yao mfano. uvuvi, kilimo, ufugaji,ufundi, nk

kwa hivyo utabakiwa na cream ya wachache waliobahatika kupata alama za kwenda sekondari, ambao nao watachujwa,
watakaochujwa wataenda kupata elimu ya kati (diploma)

watakao baki wachache zaidi ndo wataenda chuo kikuuu kufundishwa kufikiri( critical thinking)

kwa mtiririko huo tutatengeneza pyramid ambayo itamudu changamoto mbalimbali za mahitaji ya nchi.

ni ujinga kufikiri kuwa kila mtu lazima afike chuo kikuu.
 
nimekupata bro. mi nadhani tusilazimishe wanafunzi waende chuo kikuu,

tuwe na mfumo mzuri wa elimu ambao utawachukua na kuwaendeleza wale ambao hawajafikia alama za ufaulu kwenda sekondari,

tuwekeze kwenye vocation training, tuwe na vocation centers nyingi, labda moja kila kata

ukiweza kuanzisha vocation trainining utawapa ujuzi vijana wa kupambana na mazingira yao mfano. uvuvi, kilimo, ufugaji,ufundi, nk

kwa hivyo utabakiwa na cream ya wachache waliobahatika kupata alama za kwenda sekondari, ambao nao watachujwa,
watakaochujwa wataenda kupata elimu ya kati (diploma)

watakao baki wachache zaidi ndo wataenda chuo kikuuu kufundishwa kufikiri( critical thinking)

kwa mtiririko huo tutatengeneza pyramid ambayo itamudu changamoto mbalimbali za mahitaji ya nchi.

ni ujinga kufikiri kuwa kila mtu lazima afike chuo kikuu.
Hayo ndiyo ninayomaanisha hasa. Inasikitisha sana kwamba, Tanzania kama Nchi, tuliamua kuwa na A-Level ili kupata cream ya kwenda Chou Kikuu lakini cha ajabu, leo hii mtu yeyote anayefaulu Form IV, Ana asilimia zaidi ya 90 ya kwenda Chuo Kikuu. Sasa, kuna haja gani ya kuwa na A-Level kama wote wanafaulu?
Tunakosa mafundi mchundo wa kutosha kutokana na mikopo ya elimu ya juu kwa Vyuo vya private. Cha ajabu, hao wa private licha ya kuwa wa kawaida kichwani, ndio wanapata ajira kwa urahisi na kuacha vipanga vikikosa kazi.
Lazima tupunguze vyuo vikuu tu kama tunataka tutoke hapa.
 
Pamoja na kujaza maelezo mengi binafsi nimejaribu kukuelewa;
1. Elimu yetu imejikita katika Ufaulu wa mitihani na si kupata ujuzi wa ngazi husika.
2. Siasa zimetawala na kushabikia wingi wa vyuo vikuu/wahitimu badala ya Ubora unaotolewa.
***Enzi za Mungai wizarani ndo zilileta maafa kwa kupendelea wafanyabiashara wenzie (wana Vigango) kuanzisha vyuo holela kupata hela ya bure toka Loans Board....awamu hii ya Ngosha+ kupitia askari Joy tegemea TEKU, TUDARCO, MUM kufungwa kwa kukosa sifa na wanafunzi.
 
Pamoja na kujaza maelezo mengi binafsi nimejaribu kukuelewa;
1. Elimu yetu imejikita katika Ufaulu wa mitihani na si kupata ujuzi wa ngazi husika.
2. Siasa zimetawala na kushabikia wingi wa vyuo vikuu/wahitimu badala ya Ubora unaotolewa.
***Enzi za Mungai wizarani ndo zilileta maafa kwa kupendelea wafanyabiashara wenzie (wana Vigango) kuanzisha vyuo holela kupata hela ya bure toka Loans Board....awamu hii ya Ngosha+ kupitia askari Joy tegemea TEKU, TUDARCO, MUM kufungwa kwa kukosa sifa na wanafunzi.
unatoka nje ya mada, si busara kuvikomoa vyuo binanafsi, kwani vina mchango mkubwa

hoja ni kuwa vidahili wanafunzi kufuata viwango vya kimataifa.

kwa kuwa population yetu inaongezeka, vyuo vya umma haviwezi kukudhi idadi inayoongezeka, hivyo basi vyuo private bado vitahitajika.

pia kigezo kikuu cha kupewa mikopo ya wanafunzi kingekuwa
ni academic performance regardless mwanafunzi amedahiliwa chuo gani
 
Pamoja na kujaza maelezo mengi binafsi nimejaribu kukuelewa;
1. Elimu yetu imejikita katika Ufaulu wa mitihani na si kupata ujuzi wa ngazi husika.
2. Siasa zimetawala na kushabikia wingi wa vyuo vikuu/wahitimu badala ya Ubora unaotolewa.
***Enzi za Mungai wizarani ndo zilileta maafa kwa kupendelea wafanyabiashara wenzie (wana Vigango) kuanzisha vyuo holela kupata hela ya bure toka Loans Board....awamu hii ya Ngosha+ kupitia askari Joy tegemea TEKU, TUDARCO, MUM kufungwa kwa kukosa sifa na wanafunzi.
Umenisaidia sana kwani umenielewa 100%. Hii Loans Board ilianzishwa kwa nia nzuri sana but ni mojawapo ya vikwazo vikubwa kwa sasa kwenye elimu yetu kwani kila mtu anafikiria kwenda chuo kikuu tu basi, haijalishi uwezo wake.
 
unatoka nje ya mada, si busara kuvikomoa vyuo binanafsi, kwani vina mchango mkubwa

hoja ni kuwa vidahili wanafunzi kufuata viwango vya kimataifa.

kwa kuwa population yetu inaongezeka, vyuo vya umma haviwezi kukudhi idadi inayoongezeka, hivyo basi vyuo private bado vitahitajika.

pia kigezo kikuu cha kupewa mikopo ya wanafunzi kingekuwa
ni academic performance regardless mwanafunzi amedahiliwa chuo gani
Naunga mkono hoja. Hata hivyo changamoto itakuwa ni uwezo duni wa Taasisi zetu kuhimili vishindo vya rushwa. Nani wa kuvisimamia hivyo viwango? Leo Rais Magufuli anajitahidi sana kudhibiti wezi na wazembe serikalini lakini ameonekana mbaya hadi anatafutiwa majina ya ajabu ajabu. Je, Waziri ndiye ataweza? Atakataa hela?
Otherwise nakubaliana pia na ushauri wako, juu ya umuhimu wa kutobadilisha standard zetu.
 
unatoka nje ya mada, si busara kuvikomoa vyuo binanafsi, kwani vina mchango mkubwa

hoja ni kuwa vidahili wanafunzi kufuata viwango vya kimataifa.

kwa kuwa population yetu inaongezeka, vyuo vya umma haviwezi kukudhi idadi inayoongezeka, hivyo basi vyuo private bado vitahitajika.

pia kigezo kikuu cha kupewa mikopo ya wanafunzi kingekuwa
ni academic performance regardless mwanafunzi amedahiliwa chuo gani
Tofauti na Shule za sekondari binafsi (nyingi zikiwa za Mashirika ya dini ya kikristo hasa KATOLIKI) vyuo vikuu binafsi viko hoi kitaaluma (wahadhiri wenye sofa stability eg. PhD katika taaluma wanazofundisha/kufanya tafiti, miundombinu, na uwezo duni wa ki-pesa)
 
Nakumbuka in 2000s, nikiwa PS & PA, kwenye mitihani ya chuo, wanafunzi walikuwa mara kadhaa darasani unawasikia wanaomba kusaidiwa na Lecturer eneo la ku-concentrate na (sijui kwa kutuhurumia?), baadhi walikuwa wakitoa dondoo. Tangu hapo niliidharau sana elimu yetu kwani nilikuwa nawaza sana kuwa, kama darasa letu hilo, makisi za chini alizochaguliwa nazo mvulana kwenye Kozi hiyo (UDSM) ni One ya Point 7, huko wasichana ikiwa ya Point 8, sasa hali ikoje kwa madarasa mengine ya UDSM, achilia mbali Vyuo Vikuu vingine?
Cha kusikitisha pia ni kwamba, hadi mpaka Chuo Kikuu, ukijisomea sana Library, utataniwa kwa matusi tuliyozoea tangu shule za Msingi na Sekondari kuwa Unasomea Ukoo, Dah!! Lazima tuibadilishe elimu yetu, siyo kila mtu ana uwezo wa kwenda chuo kikuu (ni haki yako though).
 
Tatizo tumeingiza siasa kwny elimu, watu wanatak waonekane wanaofaulu wengi ili wajisifie wanatoa elimu bora, kisha mazuzu wakawapigie kure
 
Umenisaidia sana kwani umenielewa 100%. Hii Loans Board ilianzishwa kwa nia nzuri sana but ni mojawapo ya vikwazo vikubwa kwa sasa kwenye elimu yetu kwani kila mtu anafikiria kwenda chuo kikuu tu basi, haijalishi uwezo wake.
Kwakweli hili limekua jipu kubwa sana enzi hizo nipo sekondari mtu anakomaa na science hata kama haiwezi ili apate tu ka boom ka 100% mwisho wake wanaishia tu kuwa watu wakumeza na kukariri ili tu apite mitihani chuoni wakienda wanakua na mentality hizo hizo mwisho wa siku unatoa mwanasayansi kutoka chuo yupo ovyo tu yeye alichokua anakielewa ni kukariri tu kwa ajili ya mitihani baasi ku apply alichojifunza hawezi kabisa ..watu wa aina hio walitakiwa tu waende vyuo vya ufundi vyuo vikuu anaenda mtu ambae ana uwezo wa kufikiri zaidi badala ya kukariri ndo mana sa hv kuna mlipuko wa watu wasio na ajira na hata wanao ajiriwa wanalipwa mishahara midogo sana maana hawawezi kufikiria nje ya box kukamatia fursa nyingine za kuzalisha ajira wao wanachojua katoka chuo basi anatakiwa apate ajira ..........hio kwa upande wa science inakua ngumu sana
 
Back
Top Bottom