MANILABHONA
JF-Expert Member
- Apr 1, 2015
- 462
- 351
Naomba mnisamehe wahusika kwa mawazo yangu. Hii ni katika kujaribu kuisaidia serikali kukusanya mapato na kupeleka huduma kwa wananchi. Naishauri serikali kufikiria kuanza kukusanya kodi kwenye biashara hii ambayo inaingiza mapato mengi sana lakini ina msamaha wa kodi-Biashara katika makanisa na misikiti, biashara ya kuhubiri injili/hotuba/mawaidha na kukusanya sadaka/ zaka nk. Hii biashara inaingiza fedha nyingi sana lakini sijasikia serikali inapata gawio kiasi gaani la mapato. Wabunge ishaurini serikali kuona eneo hili nalo kuna fedha za kutosha Nawasilisha