Vurugu bungeni zasababisha Bunge kuahirishwa asubuhi hii

kwa mujibu ya katiba ya jamhuri ya muungano wa tanzania kuandamana ni haki ya kila mwananchi ili mradi afuate taratibu.miongoni mwa taratibu ni kutoa taarifa mapema polisi kwa ajili ya ulinzi na sio kuomba kibali kama wengi wanavyopotosha.

Kwa mfano unataka kuandamana kuelekea nyumba ya mtu kwa hiyo uachiwe tu ulindwe? Ni lazima mkubaliane unaandamana kwenda wapi na kupitia wapi.Mfano unataka kuandamana kupitia katikati ya soko la kariakoo ukubaliwe tu? Sababu katiba imeruhusu.?

Kuandamana barabarani ina maana kuna kuzuia magari yasitembee yapishe maandamano! Ambulance za kubeba wagonjwa zisitembee zipishe maandamano! Madaladala yasisafiri hivyo abiria kibao wakwamwe kisa kupisha maandamano.

Polisi kazi yake si kupokea taarifa tu lazima wafanye analyisis ya kutosha kabla ya kusema sawa.
 
Polisi wametekeleza amri halali kwa mujibu wa Katiba na Sheria, wanasiasa wamekuwa mifano mibaya kwa jamii, namna hii itarudisha usawa na haki.
Haiwezekani wakivunja sheria wanaachwa, sisi uraiani iwe nongwa.

Wapigwe tuu

unatimia nini kufikiri???
 
Wewe unae mwita Mungu mpumbavu huna akili huja soma.Hufai hata kuwepo duniani mwandawazimu kubwa jinga tumbo kubwa umekosa hata elimu

Akili ndogo kama hizi huwa sijibizani nazo. Endelea kutukana ukichoka kakojoe ulale
 
Wajerumani juzi wameadhimisha siku ya mauaji ya kimbari yaliyofanywa na Nazi miaka 70 iliyopita, na maadhimisho hayo yaliisha salama duniani kote. Kwanini hapa kwetu iwe haramu kwa CUF kuwakumbuka wanachama wao waliokufa miaka iliyopita? Mauaji ya Wayahudi hayakuwa halali sawa na mauaji ya wana CUF Zanzibar, lakini inawezekanaje ya Wayahudi kule Ujerumani ambayo ni mabaya zaidi yaweze kukumbukwa bila kusababisha fujo lakini yale ya Zanzibar yazuiwe eti yataamsha hamasa za wananchi?
 
Wajerumani juzi wameadhimisha siku ya mauaji ya kimbari yaliyofanywa na Nazi miaka 70 iliyopita, na maadhimisho hayo yaliisha salama duniani kote. Kwanini hapa kwetu iwe haramu kwa CUF kuwakumbuka wanachama wao waliokufa miaka iliyopita? Mauaji ya Wayahudi hayakuwa halali sawa na mauaji ya wana CUF Zanzibar, lakini inawezekanaje ya Wayahudi kule Ujerumani ambayo ni mabaya zaidi yaweze kukumbukwa bila kusababisha fujo lakini yale ya Zanzibar yazuiwe eti yataamsha hamasa za wananchi?

Zanzibar ni nchi. Yaliyotokea nchi ya Zanzibar yakafanyike nchi hiyo ya zanzibar, kama vile yale yaliyotokea UJERUMANI hapa kwetu hatukufanya maandamano kwa ajili ya yaliyotokea ujerumani.
 
uyu naibu waziri wa habari anatudanganya eti Kenya awaonyeshi bunge lao live pumbavu zake ufisadi+uongo=ccm
 


TUKIO LA KIPIGO CHA WAFUASI WA CHAMA CHA WANANCHI (CUF) NA MWENYEKITI WAO, PROFESA IBRAHIMU LIPUMBA LISICHUKULIWE KISIASA ZAIDI!!! NI KIASHIRIA KIBAYA KWA MSTAKABALI WA AMANI NA UTULIVU KATIKA NCHI YETU, WATANZANIA WA LEO SIYO WA JANA!!! WATAKAPOONA HAKI INAPINDISHWA KILA MARA WANAWEZA KUTUMIA NGUVU YA UMMA KUITAFUTA!!!

CHONDE!!! CHONDE SERIKALI ILIYOKO MADARAKANI!!! BUSARA ITUMIKE ZAIDI MUDA WOTE!!!

AMANI!! AMANI!!! AMANI!!! = UTULIVU!!!!:clap2:
 

Attachments

  • NGUVU YA UMMA.jpg
    NGUVU YA UMMA.jpg
    140.3 KB · Views: 518
Sawa lakini turuhusu jeshi la polisi lifanye unyama bila ya sheria kufuatwa??

Hao wananchi si waliambiwa waondoke? sasa waling'ang'ania nini kujaa barabarani? Barabara ni mali ya umma, wanatumia kuwahi kazini, kwenye kujitafutia kipato au hospitalini, iweje wanasiasa wakomae wakati walipewa zuio? kama tatizo ni sheria na kanuni za jeshi, bora wangepeleka mswada kuomba mabadiliko ya sheria.
 
Hili bunge lina matatizo kuanzia spika hadi wabunge wenyewe.Bunge lina agenda ambazo zilipangwa kujadiliwa.Sasa linatokea tukio mtaani wanaahirisha na kuacha ajenda kuhamia matukio ya barabarani.Waliokamatwa watapelekwa mbele ya vyombo vya sheria kutakakojulikana kama CUF walikosea au la.Bunge kiherehere chake cha nini? wanajadili nini wakati suala liko mikononi mwa vyombo vya sheria?

Bunge limekuwa linaanza kwenda na matukio badala ya ajenda zilizowapeleka pale.Hizi zote ni mbinu chafu za kutaka kuzidisha siku na kula posho zitokanazo na kodi za wananchi.

Hili bunge hovyo kabisa heri uchaguzi uje upesi wachaguliwe wabunge wengine wapya kuliko hawa wa sasa.LO.

Mbafu. Huna lolote.
 
Katika maigizo yanayoendelea Bungeni inasikitisha sana Bunge kutojari muhimili mwingine na kujiona wao ni wao na hakuna mwingine.

Hivi inaingia akilini kuanzisha fujo Bungeni kisha eti hoja aliyoleta Mbatia ahijadiliwi leo na kusababisha shughuli za Bunge kusitishwa?. Chukuliwa kila upande uwe na msimamo na tuone utakao shindwa, mimi nimesema hoja itajadiliwa kesho na wewe unasema ijadiliwe leo, wakati huo mimi ndo nimeshikilia rungu itawezekana kweli wewe kushinda bila kutumia busara?.

Kinachosababisha upinzani kupata misukosuko ni kutotii sheria na kujitungia za kwao "Nguvu ya umma" na kusahau kama watakimbilia kule wanakokutukana na kuomba msaada.

Rejea maneno ya kanga anayoyatoa Dr. Slaa akiwa jukwaani juu ya Jeshi la Polisi utafikiri anawashambulia watoto wake na kujiona ananguvu nyingi kuliko wao. Ilifikia wakati anataka kujifanananisha na Nyerere eti mbona nimefika hapa polisi walikuwa wapi?. Vivyo hivyo na Lipumba, ahaiwezekani mkubaliane maandamano yasiwepo kisha ukaandamana kwa kisingizio cha Nguvu ya umma. Kuvunja sheria hakuangali Nguvu ya umma wote kwa pamoja lazima tutii sheria ili tuishi kwa amani.

Sasa Serikali imechoka kuona inazalaurika kila wakati tumeamua kufanya kazi, haiwezekani Bunge kujiona eti wao ndio muhimili Bora kuliko yote kisa eti walishinikiza sakata la Escrow kupitishwa kihovyohovyo na kusababisha hasara kubwa kwa Serikali bila faida yeyote sasa basi na lolote na liwe.


Ushauri kwa Upinzaji kama inawezekana adui lazima uishi nae vizuri ili umshawishi kirahisi akuamini na kukupa madaraka ya kumtawara ama kumuongoza bila kutumia nguvu nyingi. Tumie ujuzi aliotumia Nyerere hadi Wakoloni wakamwamini bila kutumia nguvu, kama mambo yataendelea hivi Watanzania hawatawaamini kwani watahisi harufu ya vita mbeleni, hivyo lazima umimi uwatoke kurudi kwenye sheria na kuteka Jeshi kimawazo.

Na mwisho lazima kutambua kuwa kwenye migogoro hiyo Serikali ina watu wake ili kupunguza ukali wa hoja zilizopo vichwani mwa watu.

Haya ni mawazo yangu tu kama tata mura.

Tatizo sio kuvunja sheria,,, tatizo ni kudeal na huyu mkosaji ambaye hana silaha,,, kuna tatizo kwa askari wenu namna ya kudeal na watuhumiwa.. hapa ndio kwenye shida... Mvunja sheria anashughulikiwa vipi??? Ukivunja sheria kwa hiyo upigwe na hamna namna nyingine???
 
hapo mtuhumiwa ni serikali na serikali ndiyo inastahili kutoa majibu na majibu huenda yakawa hayapo hapohapo wanapotaka yatolewe. hivi kama sio kutaka shari na umaarufu bangi, kesho kuna umbali gani hadi lazima iwe leo na sasa hivi???
halafu mbona makinda katumia busara ya kupita kiasi katika hili..!!!
binafsi naunga mkono kipigo alichopata lipumba maana maandamano yalikuwa batili na sababu ya maandamano ndio ushenzi mtupu.
ningekuwa mimi ndio serikali, katika mwaka wa uchaguzi kama huu ningepiga marufuku maandamano maana kuna WAJINGA KAMA WEWE AMBAO MNAWASHWA NA KUKUNWA KWENU NI KUPIGWA VIRUNGU



kwa hayo maneno machafu sina cha kukujibu, mimi nimeme lelewa na binadamu, ukute wewe mlezi wako ni mbwa koko... hivyo siwezi kumvunjia heshima mzazi wangu kwa kibizana na mtoto wa mbwa koko...na kibaraka wa mafisadi,,,.....
 
Tatizo sio kuvunja sheria,,, tatizo ni kudeal na huyu mkosaji ambaye hana silaha,,, kuna tatizo kwa askari wenu namna ya kudeal na watuhumiwa.. hapa ndio kwenye shida... Mvunja sheria anashughulikiwa vipi??? Ukivunja sheria kwa hiyo upigwe na hamna namna nyingine???



Inategemeana na njia uliyotumia kuvunja sheria.
 
Back
Top Bottom