Vodacom Wanakaangwa Afrika ya Kusini

Vodacom Wanakaangwa Afrika ya Kusini

tutafikatu

JF-Expert Member
Joined
Dec 17, 2011
Posts
3,399
Reaction score
4,732
Mitandao ya simu nchini Afrika ya Kusini (Vodacom, MTN, Cellc n.k) imewekwa kitimoto na kamati ya Bunge ya SA baada ya kulalamikiwa vifurushi internet kuwa ni ghali sana. Malalamiko hayo yamepelekwa na mmiliki mmoja wa kituo cha Radio.

Mmoja wa Wabunge amesema kwamba ni bora ukawa mteja wa Vodacom Tanzania, kuliko kuwa mteja wa Vodacom Afrika ya Kusini. Maana Data Bundles zao nchini Tanzania ni rahisi sana. Pia Mbunge kalalamika kwamba vifurushi vyao Vodacom vinaisha haraka sana.

Ingawa mitandao yote ya simu inauza data bundles bei kubwa sana, Vodacom inalalamikiwa kwa kuwa na bei zaidi.

Kama una Dstv angalia eNCA tv au search live streaming yao.

Niliandika majuzi kuhusu bei ndogo za mitandao ya simu Tanzania: Bongo Vifurushi vya Simu Bei Bwerere!!!



1474513815888-jpg.404628

Tazama hapa tz ndiyo tunaongoza kwa kuuza data bei rahisi kuliko wote.
 
Huku kwetu TCRA inawaangalia tu hawa jamaa, wamepunguza kiasi cha MB unachopata to almost half
Halafu unavocompare vifurushi vya nchi mbalimbali mbona huangalii cost of living na purchasing power

e.g a bus ride in Canada costs 2.50 CAD dollars,which is almost 4000 tsh, lakini nauli ya daladala kwa Tz ni tsh 400 tu. Je daladala zikipandisha nauli, tusilalamike kisa tu nchi fulani wanalipa bei juu zaidi for the same service
 
Huku kwetu TCRA inawaangalia tu hawa jamaa, wamepunguza kiasi cha MB unachopata to almost half
Halafu unavocompare vifurushi vya nchi mbalimbali mbona huangalii cost of living na purchasing power

e.g a bus ride in Canada costs 2.50 CAD dollars,which is almost 4000 tsh, lakini nauli ya daldala kwa Tz ni tsh 400 tu. Je daladala zikipandisha nauli, tusilalamike kisa tu nchi fulani wanalipa bei juu zaidi for the same service
Nimeskia juzi mfanyakazi wa TCRA akitetea hizi kampuni,mi shida yangu ni huduma mbovu za makampuni ya simu hapa Tanzania,ukiwa mteja wao huna uhakika wa huduma bora na hili limekua kilio cha muda mrefu sana na linakera,unaweza usiwe hewan hata 3 hrs,ukija kuuliza kampun husika watakujibu kirahis sana kuwa kulikua na matatizo ya kiufundi tuwie radhi,ndo wamemaliza hapo,lawama nazipeleka KWA TCRA
 
Nimeskia juzi mfanyakazi wa TCRA akitetea hizi kampuni,mi shida yangu ni huduma mbovu za makampuni ya simu hapa Tanzania,ukiwa mteja wao huna uhakika wa huduma bora na hili limekua kilio cha muda mrefu sana na linakera,unaweza usiwe hewan hata 3 hrs,ukija kuuliza kampun husika watakujibu kirahis sana kuwa kulikua na matatizo ya kiufundi tuwie radhi,ndo wamemaliza hapo,lawama nazipeleka KWA TCRA
Yaani utafikiri hiki chombo hakifanyi kazi, wao kila siku kung'ang'ana na redio companies na kuzipiga fine
 
Huku kwetu TCRA inawaangalia tu hawa jamaa, wamepunguza kiasi cha MB unachopata to almost half
Halafu unavocompare vifurushi vya nchi mbalimbali mbona huangalii cost of living na purchasing power

e.g a bus ride in Canada costs 2.50 CAD dollars,which is almost 4000 tsh, lakini nauli ya daldala kwa Tz ni tsh 400 tu. Je daladala zikipandisha nauli, tusilalamike kisa tu nchi fulani wanalipa bei juu zaidi for the same service
Jibu la kisomi kabisa.
 
Ukiona hawafai achana nao yaani huwa siweki vocha kwa line ya voda, wamebaki kunitumia sms Za ajabuajabu za bahati nasibu
 
Huku kwetu TCRA inawaangalia tu hawa jamaa, wamepunguza kiasi cha MB unachopata to almost half
Halafu unavocompare vifurushi vya nchi mbalimbali mbona huangalii cost of living na purchasing power

e.g a bus ride in Canada costs 2.50 CAD dollars,which is almost 4000 tsh, lakini nauli ya daladala kwa Tz ni tsh 400 tu. Je daladala zikipandisha nauli, tusilalamike kisa tu nchi fulani wanalipa bei juu zaidi for the same service
Umeongea vyema sana,Hongera.

Ni kama sinema fulani inachezwa,mtoa inawezekana hajaijua ila naye ni mmojawapo wa Washiriki wa Movie.

Swali la Msingi,Why Tanzania iwe mentioned kihivyooo?? Iweje ianze Mada yake kisha iwe connected na kujua what is going on TV against Mada?

Ninachojua,kuna Staff wanaswap baina ya SA na TZ,ndiyo maana nasema hii kama Movie.....unatafutiwa mbaali kama Sniper kisha mtu anataka kujenga Hoja hahaha kwa kulinganisha Nchi na Nchi.

Mamlaka Husika zipo na Taratibu zipo zifuatwe ila si kutaka kuleta Siasa za Mbaali namna hii.
 
Mbona umekazania sana hili?? Wewe ni mfanyakazi wa voda tanzania ?
 
inaonekana una hisa voda wewe...
voda saizi ni jina tu lakini huduma zao hovyo kabisa, wao wanaona MB ni anasa
 
Vifurushi vya Voda vinaisha kwa style ya mwendo kasi,ghafla utasikia mb zako za kifushi cha 500 zimebaki 22 mara baada ya dk chache tu utaona msg mb zako zimekwisha zote hata kama Kuna back ground activities ila si kwa speed hiyo maana updates zote unakuwa umeziweka close mpaka utakapoamua kuupdate....yani wanatupiga sema tumewazoea tu kuhama unaona usumbufu kwa wenye namba yako.
 
Voda Afrika kusini kifurushi cha mwezi 1GB kwa rand 149 ambayo ni kama shilingi 22,000/. Huko Tanzania unaweza kutumia 32,000/ kupata 16GB kwa mwezi (1GB kwa shilingi 2,000/)
 
Back
Top Bottom