Ghazwat
JF-Expert Member
- Oct 4, 2015
- 23,718
- 66,262
Patashika ya Ligi Kuu Tanzania Bara Vodacom Premier League VPL, kuendelea tena leo February 4, 2020 ambapo, Simba SC, Wekundu wa Msimbazi, wanawakaribisha Maafande wa Polisi Tanzania, mchezo utakaopigwa kwenye dimba la Uwanja wa Taifa.
Mchezo wa leo ni wa kufunga mzunguko wa kwanza kwa timu zote mbili, unatarajiwa kuwa mkali na wa kusisimua kwa muda wote wa dakika 90.
Simba SC katika mechi 4 zilizopita ameshinda zote huku Polisi Tanzania wakishinda mechi 3 na sare moja hivyo Simba SC, ambao ndo Vinara wa VPL wakiwa na alama 47 wanaingia dimbani wakiwa na lengo la kuvuna alama tatu muhimu ili Kuweka Rekodi Ya Kufikisha Alama 50, kwa mzunguko huu wa kwanza wenye timu 20.
Kocha Msaidizi Suleiman Matola amsema ligi ni ngumu na hakuna mechi ndogo hivyo wamejiandaa kupambana kama walivyopambana katika mechi zilizopita wakiwa na lengo la kushinda ili kujiimarisha pale juu kwenye msimamo.
Naye Kocha Msaidizi wa Polisi Tanzania Ally Mtui, anasema mchezo utakuwa mgumu hasa ukizingatia wapinzani wao kutopoteza mechi nyingi hivyo wanaangalia namna ya kufanya ili kuweza kushinda mchezo huo.
Kumbuka mechi ni kuanzia saa 1:00 usiku, Usikose Ukaambiwa..!
...Line Up Angalia Kwenye Post #20.
Mchezo wa leo ni wa kufunga mzunguko wa kwanza kwa timu zote mbili, unatarajiwa kuwa mkali na wa kusisimua kwa muda wote wa dakika 90.
Simba SC katika mechi 4 zilizopita ameshinda zote huku Polisi Tanzania wakishinda mechi 3 na sare moja hivyo Simba SC, ambao ndo Vinara wa VPL wakiwa na alama 47 wanaingia dimbani wakiwa na lengo la kuvuna alama tatu muhimu ili Kuweka Rekodi Ya Kufikisha Alama 50, kwa mzunguko huu wa kwanza wenye timu 20.
Kocha Msaidizi Suleiman Matola amsema ligi ni ngumu na hakuna mechi ndogo hivyo wamejiandaa kupambana kama walivyopambana katika mechi zilizopita wakiwa na lengo la kushinda ili kujiimarisha pale juu kwenye msimamo.
Naye Kocha Msaidizi wa Polisi Tanzania Ally Mtui, anasema mchezo utakuwa mgumu hasa ukizingatia wapinzani wao kutopoteza mechi nyingi hivyo wanaangalia namna ya kufanya ili kuweza kushinda mchezo huo.
Kumbuka mechi ni kuanzia saa 1:00 usiku, Usikose Ukaambiwa..!
...Line Up Angalia Kwenye Post #20.