NALIA NGWENA
JF-Expert Member
- Oct 6, 2016
- 10,206
- 12,747
Ukweli usemwe japokuwa ni mchungu, hamasa imekua kubwa sana katika kuwahamsisha mashabiki wa Simba sc lakini mwitikio sifuri.
Zimesambazwa tickets za bure kwenye matawi, viongozi wa Simba sc wanadai kuwa wameshusha kiingilio mpaka elfu 3000 kwa mzunguko Lakini nyuma ya pazia ni bure.
NALIA NGWENA nawapa sababu za mashabiki wa Simba sc kususia kununua tickets za mchezo wa Asec mimos utakaopigwa tare 25/11.
Mosi, kipigo kitakatifu (mbwa mwizi) walichokishuhudia mashabiki wa Simba sc dhidi ya mtani wao, hii imewanyong'onyesha sana mashabiki na kujiona kuwa hawana timu.
Pili, Matokeo mabovu ya Simba sc kwenye mechi za kimataifa, mashabiki wanajua kuwa hata wakihudhuria matokeo mazuri kwao ni sale tu tofauti na hapo labda wachezee kichapo.
Ikumbukwe toka Simba sc ianze kushiriki michuano hii ya kimataifa msimu huu haijawahi kushinda Bali imetoka sale michezo yote mpaka kufuzu makundi.
Tatu, mashabiki hawana Imani na kocha Cadena na msaidizi Wake Suleimani matola, mashabiki wanaamini makocha Hawa walioachiwa timu kwa muda mfupi hawana mbinu za kumfunga Asec.
Nne, uongo wa viongozi wa Simba sc akiwemo msemaji wao Ahmedy ally, kiufupi mashabiki wamechoka na wamemzoea kwa porojo zake zisizo na mashiko ukija kwenye uhalisia hakuna kitu.
Tano, kikosi kibovu Cha Simba sc hili lipo wazi haina kikosi Cha kuwafurahisha Wana Simba sc Bali Wana kikosi Cha kuwapa presha mashabiki wa Simba hii NI moja ya sababu kuu inayoifanya mashabiki wasiende uwanjani.
Maoni Yangu: yakifanyiwa kazi hayo, mashabiki watakuja uwanjani pasipo kufanyiwa hamasa ya visipika.
Nawasilisha hoja.
Zimesambazwa tickets za bure kwenye matawi, viongozi wa Simba sc wanadai kuwa wameshusha kiingilio mpaka elfu 3000 kwa mzunguko Lakini nyuma ya pazia ni bure.
NALIA NGWENA nawapa sababu za mashabiki wa Simba sc kususia kununua tickets za mchezo wa Asec mimos utakaopigwa tare 25/11.
Mosi, kipigo kitakatifu (mbwa mwizi) walichokishuhudia mashabiki wa Simba sc dhidi ya mtani wao, hii imewanyong'onyesha sana mashabiki na kujiona kuwa hawana timu.
Pili, Matokeo mabovu ya Simba sc kwenye mechi za kimataifa, mashabiki wanajua kuwa hata wakihudhuria matokeo mazuri kwao ni sale tu tofauti na hapo labda wachezee kichapo.
Ikumbukwe toka Simba sc ianze kushiriki michuano hii ya kimataifa msimu huu haijawahi kushinda Bali imetoka sale michezo yote mpaka kufuzu makundi.
Tatu, mashabiki hawana Imani na kocha Cadena na msaidizi Wake Suleimani matola, mashabiki wanaamini makocha Hawa walioachiwa timu kwa muda mfupi hawana mbinu za kumfunga Asec.
Nne, uongo wa viongozi wa Simba sc akiwemo msemaji wao Ahmedy ally, kiufupi mashabiki wamechoka na wamemzoea kwa porojo zake zisizo na mashiko ukija kwenye uhalisia hakuna kitu.
Tano, kikosi kibovu Cha Simba sc hili lipo wazi haina kikosi Cha kuwafurahisha Wana Simba sc Bali Wana kikosi Cha kuwapa presha mashabiki wa Simba hii NI moja ya sababu kuu inayoifanya mashabiki wasiende uwanjani.
Maoni Yangu: yakifanyiwa kazi hayo, mashabiki watakuja uwanjani pasipo kufanyiwa hamasa ya visipika.
Nawasilisha hoja.