Vodacom nimewachoka

Qurie

JF-Expert Member
Joined
Aug 9, 2015
Posts
3,645
Reaction score
3,889
Kwakweli Vodacom nawahama Bora nirudi tigo Kuna kifurushi Cha size yako napata mb za kutosha kwa sh elfu Moja week nzima au niende halotel kwenye kile kifurushi Cha royal bundle haki voda siweki Tena vocha.... Yaan elfu mbili Mia tano (2500) mnanipa MB 800??
Line ya tigo nnayo na leo lazima nisajili line ya halotel tusinyanyasane bakini na hao hao ambao hawana uchungu na hela...
 
Mimi Nina elfu mbili kwenye salio na bando la data nilikua nimejiunga na bado lipo lakini naona kila Siku wanakata mia,Jana ikabaki 1,900 Leo asubuhi imebaki 1,800 hawa jamaa ni wezi kweli aisee
 
Offer yao ya dar super uni sikuhizi hawana.
Wanapendelea dar hawa majamaa.

Size yako ya tigo ni kiboko.
Kwa laini ya chuo ila, maana maisha aya inabidi tuwe wanafunzi wa chuo tu sasa
Tigo nna line ya chuo..... Na tigo nao wakizingua nawahama vile vile.....
Ashukuriwe Mungu watoa huduma wa mitandao ya cm wapo wengi ingekua Kuna mtoa huduma mmoja tungekoma
 
Mimi Nina elfu mbili kwenye salio na bando la data nilikua nimejiunga na bado lipo lakini naona kila Siku wanakata mia,Jana ikabaki 1,900 Leo asubuhi imebaki 1,800 hawa jamaa ni wezi kweli aisee
Wezi haswaaaa..... Na ukiwapigia cm hawana Cha maana Cha kukusaidia.... Hi tabia yao ya kukata salio kidogo kidogo nliamuaga kutokuweka salio la kawaida kwa cm nlikia naweka mpesa tuuu Sasa,,, Sasa ivi hata mpesa cweki TENAAA .... Najua mimi mmoja tuu nikiwahama hawapati hasara yoyote lakn ndo tayar washampoteza mteja ivyooo
 
Kwakweli hili la kukata salio kimyakimya linashangaza sana,kuanzia leo siweki salio tena,
 
Tena ukienda mikoani hautaki hata tumia voda: kuna sehemu nilikuwa yani kwa siku natumia 2000 afu napata MB 200.

Nikajihamia zangu tigo, na wiki mbili sasa
Japo nao wwkizingua naenda nyumban TTCL
Turudi nyumbani kumenoga ttcl
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…