Vodacom mtandao usio wakutegemea

Vodacom mtandao usio wakutegemea

hippocratessocrates

JF-Expert Member
Joined
Jul 1, 2012
Posts
3,598
Reaction score
1,545
Salaam.

Hivi karibuni kumekuwa na malalamiko karibu kila kona hasa kwa watumiaji wa mtandao huu(mimi nikiwa mmoja wapo). Pesa(Salio) kupungua kila wakati tena ukiwa hujafanya matumizi yoyote ya kupiga simu, kutuma ujumbe mfupi au kutumia intanet i(off mobile data connection).

Binafsi nimekuwa mhanga wa tatizo hili kwa maana ilifika hatua matumizi yanakimbilia sabini elfu(70,000/=Tshs) kwa mwezi. Nimetafuta msaada bila mafanikio, tatizo hili lilishawahi kunitokea mwaka huu mwanzoni, nimeshazunguka sana Mlimani City (HQ) kwani nilidhani shida ni katika 'line' au simu yangu tu.

Majibu ya wafanyakazi/watumishi wao wa kitengo cha huduma kwa wateja hayaridhishi na wakati fulani yanakatisha tamaa.

Hapa jamvini, watu wameshalalamika sana na hata 'Sticky thread' kuanzishwa lakini hakuna mabadiliko. Hakuna msaada hata kwa member ajiitaye Vodacom Tanzania.

Sasa leo tena vifurushi kubadilika tena,kila siku wana jipya, na jipya lao ni bovu kuliko lililopita. Hapa sasa 'nimeomba poo'.
 
Vodacom ni majamba wezi kabisaaa, na nina mpango wa kufanya kampeni ya kukusanya line zao kwa wananchi ili kuzirudisha ofsini kwao.hamia airtel bana
 
Vodacom ni majamba wezi kabisaaa, na nina mpango wa kufanya kampeni ya kukusanya line zao kwa wananchi ili kuzirudisha ofsini kwao.hamia airtel bana

Hahahaha..mkuu kuzirudisha wanaweza kudhani za kampuni! Ila nimependa wazo lako. Ninehamia leo baada ya kukuta kifurushi xha 999Tshs unapata MB 10 tu(asubuhi), then tukalalamika sana wakabadilisha wakaweka kiwe kifurushi cha 899 ndio 10MB, dk 18 na sms 300 halafu kile cha 999 ndio upate dk 21 na 100MB sijui na sms ngapi.

"Vodacom kazi ni kwako"
 
Mimi, jumatatu natafuta line ya airtel sitaki tena ujinga wa voda!
 
Vodacom ni majamba wezi kabisaaa, na nina mpango wa kufanya kampeni ya kukusanya line zao kwa wananchi ili kuzirudisha ofsini kwao.hamia airtel bana

Mkuu wazo jema hilo!! utakapokuwa unakusanya line zao pitia na ya kwangu, maana nimewachoka hawa voda! hovyo kabisaa hii kampuni
 
mi mwenyewe nahama voda kabisaa... naiweka kapuni very soon
 
Kuna watu wananishangaa kwa kuwa na simcard nne.kumbe niliona mbali,kama unatumia data sana airtel na zantel wako vizuri sana.kama una kazi ya kuwasilia na na watu wengi wafanyabiashara hivi tigo itakusaidia.Mambo mbalimbali ya kiofisi tumia voda kwa mawasiliano.

makampuni haya wakati mwingine wanakubaliana kushusha au kufanya mabadiriko ktk huduma zao.Ni wakati wetu sasa nasi kuungana kusitisha huduma zao walau kwa siku mmoja.Sasa napndekeza tarehe 01/12/2014 iwe ni siku ya" kutotumia simu tanzania"
 
Kuna watu wananishangaa kwa kuwa na simcard nne.kumbe niliona mbali,kama unatumia data sana airtel na zantel wako vizuri sana.kama una kazi ya kuwasilia na na watu wengi wafanyabiashara hivi tigo itakusaidia.Mambo mbalimbali ya kiofisi tumia voda kwa mawasiliano.

makampuni haya wakati mwingine wanakubaliana kushusha au kufanya mabadiriko ktk huduma zao.Ni wakati wetu sasa nasi kuungana kusitisha huduma zao walau kwa siku mmoja.Sasa napndekeza tarehe 01/12/2014 iwe ni siku ya" kutotumia simu tanzania"

Hahaha...mkuu, hizi ideas ni nzuri pia...kuna mtu pia alipendekeza kwa jinsi voda walivyo tutia hasara, tunaweza kukopa (Nipige tafu ya 900) na roughly tukifanya hivyo watu kama laki tatu au laki nne, tunaziacha na lines kabisa, then tunaweza kumpa mkuu Ezekiel azirudishe.
 
Last edited by a moderator:
hawa voda ni majanga tuu ,kuanzia m-pesa ada za kutuma ,kutoa pesa zimekuwa mwiba ,na ni heri hata kama unatumapesa utume kwa njia ya benki ,ukatoe kwenye atm at least kiwango chochote unaktwa sh 700 kulikon hawa voda kila kiwango cha hela kina ada yake ,

kingine ni kupunguza dakika ,na mb ,na hii ni sera chafu inayofanywa na maccm walio na hisa kubwa huko voda cz ndo waliona influence kubwa lengo ni kukusanya hela za kampen uchaguz ujao kwa maana nchi wabisan wameaitisha misaada ,kingine ni mbinu chafu za maccm kutotaka transparency ,na quick flow of news and information kwenye hii mitandao ya kijamii inayotumia internet data bundle kama whatsapp ,jamiiforum ,facebook ,instagram na nyinginezo ,

hebu hawa waliona dhamana ya hii mitandao wawajali wateja wao wasifanye mambo kwa maslai ya watu au vikundi fulan
 
Mkuu,hwawezi kuboresha wala kubadirisha.kwa sababu lengo ni kuiba na si kingine.


Naisikitikia ngazi fulani kuonyesha dhahiri kushindwa.bado tatizo ni kubwa sana ndugu zangu wadanganyika.kila sehemu ni uharo tu.

Sent from my radio
 
Kuna ndugu zao tigo leo nashangaa kifurush cha extream cha 499 kimekua et dk 7 sms 300 na mb 30. Wanatujazia masms cjui ya kaz gani huku wakijua sku hizi matumizi makubwa ni kwa internet
 
Back
Top Bottom