Vodacom acheni kutuibia

Ngosi

JF-Expert Member
Joined
Oct 4, 2011
Posts
391
Reaction score
191
Ndugu wana jamvi la jamii forum, huu mtandao wa voda nakua namashaka nao jinsi siku zinavyosogea, walianzia CHEKA BOMBASTICK YA 900 kwa dk 60, wakatoa wakaweka cheka ya dk 25, sasa hv sh 500 unapewa dk 10, inamaana dk 1 sh 50. Huu ni wizi
 
Ni kweli mkuu, wanachokifanya voda kwenye vifurushi vyao kwa sasa ni wizi mtupu, tena mchana kweupe. Nafanya mpango wa kuwahama hivi karibuni
 
Hivi TCRA siku hizi wako wapi?,kwani sasa hivi kinachoendelea kwenye Voda ni Ulaghai tu.Ukijiunga na vifurushi vyao na ukabakiza hela kwenye Simu basi hapo imekula kwako kwani hutaletewa ujumbe wa kuisha kwa kifurushi hadi hapo utakapo ulizia salio kwa sms.
 
Mkuu cheka ya 900 is temporary suspended nadhani kuna maboresho yanatakiwa kufanywa, tuwe tu watulivu wakati technicians wakifanya yao.
Kama unaweza nunua ile ya elfu 15 ya mwezi mzima sekunde 27000, sie tuna za staff elfu 15 sekunde 54000
 
Mkuu cheka ya 900 is temporary suspended nadhani kuna maboresho yanatakiwa kufanywa, tuwe tu watulivu wakati technicians wakifanya yao.
Kama unaweza nunua ile ya elfu 15 ya mwezi mzima sekunde 27000, sie tuna za staff elfu 15 sekunde 54000

We kimeo nini ...ivi unafikiri kila mtu anuwezo wa kununua iyo ya mwezi kwa mkupuo ...kibaya zaidi unatuambia mambo ya staff nini sijui .sasa hiyo inatuhusu vipi sisi wateja. Inaonyesha wewe ni kibarua wa voda unatuletea porojo zako hapa
 
Hatutakiwi kudhani, kama wana maboresho walipaswa kuwaeleza wateja what's going on. maelezo yako yamekaa kiushabiki mno lakini katika suala linalohitaji umakini


Mkuu cheka ya 900 is temporary suspended nadhani kuna maboresho yanatakiwa kufanywa, tuwe tu watulivu wakati technicians wakifanya yao.
Kama unaweza nunua ile ya elfu 15 ya mwezi mzima sekunde 27000, sie tuna za staff elfu 15 sekunde 54000
 
Sh 500 wangetoa dk 20 km zaman na sio dk 10, kwa ss hv wamepigwa bao na Airtel na 0715
 
Wanakuambia sh 600 dk 25 ukinunua unapata 15

Dooh inabidi wajiangalie sana. Siku hizi wanaboa sana. Mwanzoni nilikuwa na line 2 zote za kwao. Walipozidi upuuzi wao nikaitupa moja nikaweka 071X. Nina mpango wa kuitupa na hii ya pili!
 
Ndugu wana jamvi la jamii forum, huu mtandao wa voda nakua namashaka nao jinsi siku zinavyosogea, walianzia CHEKA BOMBASTICK YA 900 kwa dk 60, wakatoa wakaweka cheka ya dk 25, sasa hv sh 500 unapewa dk 10, inamaana dk 1 sh 50. Huu ni wizi

Leo nimeshangaa na kukasirika zaidi niliponunua bundle ya 4200 nikapewa sekunde 6000 badala ya 8200.
Narudi kwa ndugu zangu wa HAKATWI MTU HAPA afadhali wao wana better deals
 
Mkuu cheka ya 900 is temporary suspended nadhani kuna maboresho yanatakiwa kufanywa, tuwe tu watulivu wakati technicians wakifanya yao.
Kama unaweza nunua ile ya elfu 15 ya mwezi mzima sekunde 27000, sie tuna za staff elfu 15 sekunde 54000

Sasa mi nikitaka hiyo ya staff nafanyaje ili niinjoi hizo sekunde 54000? manake huu mwingine ni wizi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…