vodacom 100M!!???

RealTz77

JF-Expert Member
May 18, 2009
738
40
wana JF naomba kutoa hoja, tumezoea kuona companies nyingi kufanya promotions mabalimbali, lakini hili la kutoa 100M kwa mtu mmoja wakati una wateja Mil 5, sio busara. wapo wateja wengi ambao kutoka 100M ungewapatia watu 1000 shs milion moja moja, sasa hapa hata kurekebisha maisha ya wateja tungesema its ok,but single person getting 100M in TZ by just sending an sms, aah its disgusting, probability ndo hivyo inamwangukia mwenye nacho, so tabaka la maskini na tajiri linakuzwa!! unakuta mtu kama huyu mshindi wala hatumii hela yake kujiingiza ktk promotion may be anawekewa na ofice shs laki5 kila mwezi,so laki2 akiziweka ktk promotion anatuma tu sms kweli ataacha kujishindia?so natoa wazo tu hizi zawadi kwa nchi kama zetu ziwe za kiwango kizuri ziwafaidishe wateja wanahitaji kweli hela, si kumpa mtu ambae tayari anjiweza! pia wateja hawa ndo wataipigia debe kampuni kwani kila mtu atavutiwa nae ajiunge au aqwe mteja!! natoa hoja
 
Ulichosema ni kizuri lakini wahusika sijui hata kama waliwahi kufikiria kitu kama hicho;labda tuwajulishe kwamba hivyo ndiyo sivyo ila hii ndiyo safi.Huwezijua unaweza ukawa umewatoa matongotongo na ukabewa shavu pia.
Ila ukipewa shavu usinisahau,anyway is up to you to let them know or to reserve your idea right here.
 
wana JF naomba kutoa hoja, tumezoea kuona companies nyingi kufanya promotions mabalimbali, lakini hili la kutoa 100M kwa mtu mmoja wakati una wateja Mil 5, sio busara. wapo wateja wengi ambao kutoka 100M ungewapatia watu 1000 shs milion moja moja, sasa hapa hata kurekebisha maisha ya wateja tungesema its ok,but single person getting 100M in TZ by just sending an sms, aah its disgusting, probability ndo hivyo inamwangukia mwenye nacho, so tabaka la maskini na tajiri linakuzwa!! unakuta mtu kama huyu mshindi wala hatumii hela yake kujiingiza ktk promotion may be anawekewa na ofice shs laki5 kila mwezi,so laki2 akiziweka ktk promotion anatuma tu sms kweli ataacha kujishindia?so natoa wazo tu hizi zawadi kwa nchi kama zetu ziwe za kiwango kizuri ziwafaidishe wateja wanahitaji kweli hela, si kumpa mtu ambae tayari anjiweza! pia wateja hawa ndo wataipigia debe kampuni kwani kila mtu atavutiwa nae ajiunge au aqwe mteja!! natoa hoja
kwa kweli sioni tatizo
 
Kibaya zaidi hizo 100m wala hazikutoka mfukoni mwa Vodacom,ni zetu sisi wenyewe wateja maana ilikuwa ukiandika neno TUZO POINT na kupeleka namba 123 ndo unaingizwa kwenye droo na hiyo ni baada ya kukatwa sh 40.- kwenye akaunti yako kama gharama ya kuingizwa kwenye droo. Sasa hebu fikiria wateja milioni tano kila mmoja ajaribu bahati yake kwa sms kumi maana yake Vodacom wanavuna jumla ya sh bilioni mbili,sasa jiulize kazawadi kenyewe kama ni jumla labda milioni mia mbili je wao faida yao sh ngapi? si mabilioni kama sio matrilioni? si voda tu hata celtel zawadi nyumba,Tigo zawadi gari mchuma yote wizi mtupu! TCRA/BAHATI NASIBU YA TAIFA mpoooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooooo?????????
 
its true sometimes sioni hata sababu ya wao kutokuona hilo tatizo, unapoweka zawadi worth 100M for a single person hata wateja nao wanakuwa hawana uhakika na ushiriki unakuwa mdogo kwa kuwa probability ya 1 in 5M ni ndogo sana, lakini kama ile 100M ingewekkwa kwa wateja hata laki moja tu...kila mtu angejiona mshindi na angeshiriki kadri anavyoweza........i think its a wake up call to them kama kweli wanaliona hili...japo lipo tatizo kwa waandaji kwamba wakati mwingine ni ishu...
 
thanks Fidel unawaza far sio kama huyo anaesema haoni tatizo.

Mkuu zawadi zingine kwa wale wateja maskini wanao tumia 5000 vocha kwa mwezi wangekuwa wanapewa bonus ya vocha hata 500 tu inatosha. Lakini kumpa mtu mmoja 100M naona kama kuna kamchezo flani hivi nyuma ya pazia.
 
Vodacom si serikali, wala main interest yao si welfare ya watanzania directly (of course wanataka clientelle yenye purchasing power ili waweze kuvuna)

Probably Vodacom wameangalia business model yao wakaona ukitoa zawadi kubwa moja utavutia watu wengi zaidi kuliko ukitoa zawadi ndogo nyingi.

Kama unataka kuwasakama Vodacom, wasakame kwa misingi ya kwamba maamuzi yao si mazuri kwa biashara yao.Kuwasakama Vodacom kwa misingi ya kutokuwa fair kwa wananchi si kuitendea haki Vodacom, katika mfumo wa biashara huru, Vodacom iko pale kutengeneza faida, na kama mfumo utakaoiletea faida zaidi ni wa kumpa mtu mmoja shilingi ,ilioni mia moja badala ya kuwapa watu mia moja shilingi milioni moja, so be it.

That is the free market for you. Kuna watu walimwaga kahawa Brazil ili mradi kusiwe na oversupply itakayoletea bei kushuks, some would say nonsensical but it worked for them. Business decision must not always make sense to all parties.
 
duuh hii kali,nadhani wanachofanya vodacom si kibaya, nadhani ukifuatilia toka shindano lilivyoanza, utaona mnarudia kuusema mchanganuo walioufanya katika kushindanisha zawadi,na hata sasa kama ni wafuatiliaji wazuri wa taarifa za habari juzi nilimuona kama meneja wao akielezea mfumo mzima wa zawadi wanazozitoa, hivyo ni muhimu tukatoa cream ya habari kuliko kuandika povu la habari,mimi nina line yao tokea kitambo, they have quality service
 
VodaJamaa
Nawahurumia wateja wa VODA kwani hawajui kwamba wanakamuliwa na anayewakwapulia vijisent vyao kuleee.....
 
Back
Top Bottom