Vituko vya UDOM - Wanafunzi kumwita mhadhiri shemeji!!

Ubumuntu

JF-Expert Member
Oct 21, 2010
14,316
10,782
Salaam wana JF!

Sote tunakifahamu chuo chetu kikuu cha Dodoma. Ni chuo ambacho kumekua na vituko vingi vikiripotiwa toka pale. Mfano,wanafunzi kufundishwa na wahadhiri wenye shahada moja! Kuitwa chuo cha kata kutokana na kua na uhaba wa wahadhiri wenye sifa na vigezo! Makamu msaidizi wa mkuu wa chuo kujiita kondoo mweusi,mara kuku anayeatamia! Kuitwa chuo cha chama (CCM). Chuo kutoa shahada ya uzamivu kwa mkwere wakati chuo hakijawahi hata kutoa mwanafunzi 1 wa shahada hiyo n.k.

Ila hiki kituko cha wanafunzi kuwaita baadhi ya wahadhiri shemeji,mimi kimeniacha hoi.

Kutokana na chuo kua na wahadhiri wengi vijana,kumetokea tabia ya wahadhiri hao kujisevia wanafunzi wa kike,kiasi kwamba hadi wanafunzi wenzao wanafahamu tabia hizo na mwishowe kuamua kuwaita wahadhiri hao wanaotembea na wanafunzi wenzao wa kike,mashemeji!

Hakika UDOM kuna vijambo na vituko!
 
Hiyo ya mashemeji nafikiri ipo kila chuo maana hata maprof nao wamo kwenye kujisevia
 
Mambo makubwa kwenye vyuo vya kisasa. Maprofesa kuitwa mashemegi hayo ni mapya (made in Tanzania) hata huko Ulaya hakuna.
 
salaam wana jf!

Sote tunakifahamu chuo chetu kikuu cha dodoma. Ni chuo ambacho kumekua na vituko vingi vikiripotiwa toka pale. Mfano,wanafunzi kufundishwa na wahadhiri wenye shahada moja! Kuitwa chuo cha kata kutokana na kua na uhaba wa wahadhiri wenye sifa na vigezo! Makamu msaidizi wa mkuu wa chuo kujiita kondoo mweusi,mara kuku anayeatamia! Kuitwa chuo cha chama (ccm). Chuo kutoa shahada ya uzamivu kwa mkwere wakati chuo hakijawahi hata kutoa mwanafunzi 1 wa shahada hiyo n.k.

Ila hiki kituko cha wanafunzi kuwaita baadhi ya wahadhiri shemeji,mimi kimeniacha hoi.

kutokana na chuo kua na wahadhiri wengi vijana,kumetokea tabia ya wahadhiri hao kujisevia wanafunzi wa kike
,kiasi kwamba hadi wanafunzi wenzao wanafahamu tabia hizo na mwishowe kuamua kuwaita wahadhiri hao wanaotembea na wanafunzi wenzao wa kike,mashemeji!

Hakika udom kuna vijambo na vituko!
sasa wewe ndugu, university ni adult education, au hujui acha ushamba, kufa kwa kiu ukiwa baharini ni dhambi
 
Salaam wana JF!

Sote tunakifahamu chuo chetu kikuu cha Dodoma. Ni chuo ambacho kumekua na vituko vingi vikiripotiwa toka pale. Mfano,wanafunzi kufundishwa na wahadhiri wenye shahada moja! Kuitwa chuo cha kata kutokana na kua na uhaba wa wahadhiri wenye sifa na vigezo! Makamu msaidizi wa mkuu wa chuo kujiita kondoo mweusi,mara kuku anayeatamia! Kuitwa chuo cha chama (CCM). Chuo kutoa shahada ya uzamivu kwa mkwere wakati chuo hakijawahi hata kutoa mwanafunzi 1 wa shahada hiyo n.k.

Ila hiki kituko cha wanafunzi kuwaita baadhi ya wahadhiri shemeji,mimi kimeniacha hoi.

Kutokana na chuo kua na wahadhiri wengi vijana,kumetokea tabia ya wahadhiri hao kujisevia wanafunzi wa kike,kiasi kwamba hadi wanafunzi wenzao wanafahamu tabia hizo na mwishowe kuamua kuwaita wahadhiri hao wanaotembea na wanafunzi wenzao wa kike,mashemeji!

Hakika UDOM kuna vijambo na vituko!

Chuo kikuu ni sehemu ambayo wanafunzi ni watu wazima na wana uhuru wa kujiamulia mtu wa kufanya naye mapenzi hata kama ni mhadhiri. Hiyo inajulikana sehemu zote duniania, ndiyo maana kumekuwa na hadithi nyingi za wanandoa waliojuana huku mmoja akiwa mhadhiri na mwingine akiwa ni mwanafunzi. Tatizo kubwa ni pale kunapokuwa na differential authority baina yao. Kwa mfano kama mhadhiri akiwa anafundisha somo ambalo msichana au mvulana anayefanya naye mapenzi anahudhuria. Kutopkana na conflict of interests, hali hiyo hairuhusiwe na ni kosa kubwa sana ikijulikana kwa uongozi wa chuo. Inapotokea hivyo, inabidi mhadhiri aachie somo hilo lifundishwe na wahadhiri wengine.
 
Salaam wana JF!

Sote tunakifahamu chuo chetu kikuu cha Dodoma. Ni chuo ambacho kumekua na vituko vingi vikiripotiwa toka pale. Mfano,wanafunzi kufundishwa na wahadhiri wenye shahada moja! Kuitwa chuo cha kata kutokana na kua na uhaba wa wahadhiri wenye sifa na vigezo! Makamu msaidizi wa mkuu wa chuo kujiita kondoo mweusi,mara kuku anayeatamia! Kuitwa chuo cha chama (CCM). Chuo kutoa shahada ya uzamivu kwa mkwere wakati chuo hakijawahi hata kutoa mwanafunzi 1 wa shahada hiyo n.k.

Ila hiki kituko cha wanafunzi kuwaita baadhi ya wahadhiri shemeji,mimi kimeniacha hoi.

Kutokana na chuo kua na wahadhiri wengi vijana,kumetokea tabia ya wahadhiri hao kujisevia wanafunzi wa kike,kiasi kwamba hadi wanafunzi wenzao wanafahamu tabia hizo na mwishowe kuamua kuwaita wahadhiri hao wanaotembea na wanafunzi wenzao wa kike,mashemeji!

Hakika UDOM kuna vijambo na vituko!

Kwa hiyo wanafunzi walitaka wahadhiri wakihitaji kuoa wakatafute machangudoa? Au waende vijijini? Nao hao wasichana wengine si ajabu wakaishia kuolewa na hao mashemeji, sasa kuna ubaya gani hapo?

Kibaya tu ni kama uhusiano wa mhadhiri na mwanafunzi unahusisha suala la Marks au kama kuna suala la ubakaji. Wale wote ni watu wazima, kama wametongozana na kukubaliana hakuna shida kabisa. Ebu fikiria Mwalimu wa Sociology anatembea na mwanafunzi wa uhandisi baada ya kutongozana vizuri tu, kuna tatizo gani hapo?.

Au labda wanafunzi wanafikiri Mhadhiri asingechukua mwanafunzi fulani, wao (wanafunzi) wangeweza kumpata huyo demu kirahisi?
 
Kwa hiyo wanafunzi walitaka wahadhiri wakihitaji kuoa wakatafute machangudoa? Au waende vijijini? Nao hao wasichana wengine si ajabu wakaishia kuolewa na hao mashemeji, sasa kuna ubaya gani hapo?

Kibaya tu ni kama uhusiano wa mhadhiri na mwanafunzi unahusisha suala la Marks au kama kuna suala la ubakaji. Wale wote ni watu wazima, kama wametongozana na kukubaliana hakuna shida kabisa. Ebu fikiria Mwalimu wa Sociology anatembea na mwanafunzi wa uhandisi baada ya kutongozana vizuri tu, kuna tatizo gani hapo?.

Au labda wanafunzi wanafikiri Mhadhiri asingechukua mwanafunzi fulani, wao (wanafunzi) wangeweza kumpata huyo demu kirahisi?



Hoja inakua je ikitokea huyo mhadhiri anajisevia mwanafunzi anaemfundisha,inakuaje hapo? Huoni kama kunaeza tokea conflicting interests kwny masuala ya marking and continuous assessment? Pia huoni kama wanafunzi wengine watahisi ka mwenzao atapendelewa? Tabia hii inaweza sababisha uvujifu wa mitihani hususani pale wanafunzi watakapomshauri mwanafunzi mwenzao wa kike anaeseviwa na mhadhiri,kwenda kumpumbaza mhadhiri(kwa maluvi davi) ili amwonyeshe mtihani.

Ni kweli ni adult learning na mahusiano yanaruhusiwa ila mazingira ya kutokea kwa conflicting interests yanafanya tabia hii kua haifai. Hii ni sawa na kuchanganya siasa na biashara.
 
kazaaazi kwelikwli. Na walishatangaza kazi mwisho wa kutuma maombi ni 28 Feb 2011. Mashemeji watongezeka hasa ukichukulia HESLB wanasuasua kuwapa pesa.
 
Hawa vijana ni ukosefu wa adabu tu, utamwitaje mtu shemeji wakati huna uhakika na mambo yaliyokuwa yanakwenda nyuma ya kitasa? Ndo maana katika dini ya kiisilamu kumshika ugoni ni lazima fataki ikutwe ndani ya mtutu na uwe na masahahidi watatu wasio na ususiano wowote.
 
Hoja inakua je ikitokea huyo mhadhiri anajisevia mwanafunzi anaemfundisha,inakuaje hapo? Huoni kama kunaeza tokea conflicting interests kwny masuala ya marking and continuous assessment? Pia huoni kama wanafunzi wengine watahisi ka mwenzao atapendelewa? Tabia hii inaweza sababisha uvujifu wa mitihani hususani pale wanafunzi watakapomshauri mwanafunzi mwenzao wa kike anaeseviwa na mhadhiri,kwenda kumpumbaza mhadhiri(kwa maluvi davi) ili amwonyeshe mtihani.

Ni kweli ni adult learning na mahusiano yanaruhusiwa ila mazingira ya kutokea kwa conflicting interests yanafanya tabia hii kua haifai. Hii ni sawa na kuchanganya siasa na biashara.

Na wala si lazima conflicting interests zitokee. Wote tumesoma vyuoni. Nilipokuwa chuoni niliwahi kushuhudia mwanafunzi akishindwa mtihani kwenye somo analofundisha mume wake. Na mwingine alishindwa somo alilofundisha baba yake. Kwa hiyo kama mhadhiri anafuata maadili ya kazi wala hakuna matatizo yoyote.

Kwa upande mwingine habari zote kuhusu uhusiano wa mwanafunzi na mhadhiri zinaweza zikawa uzushi tu. Mara nyingi kwenye vyuo, rumours za shemeji shemeji huwa zinaanzishwa na wanafunzi wa kiume. Moja wapo ya sababu huwa ni wivu kwenye marks. Kwa mfano mwanaume akizidiwa marks na msichana, lazima atasingizia tu kuwa yule msichana kagawa mwili. Ila ikitokea mvulana ameongoza mtihani kwenye somo linalofundishwa na mwalimu wa kike, hamna kinachosemwa. Na tatizo linakua zaidi iwapo msichana ni mrembo au hajatulia kitabia au amewatolea nje wanafunzi wa kiume na wakati huo huo anafaulu mtihani. Lazima mhadhiri atafikiriwa kuwa amepewa uroda. Lakini si lazima iwe kweli.
 
Na wala si lazima conflicting interests zitokee. Wote tumesoma vyuoni. Nilipokuwa chuoni niliwahi kushuhudia mwanafunzi akishindwa mtihani kwenye somo analofundisha mume wake. Na mwingine alishindwa somo alilofundisha baba yake. Kwa hiyo kama mhadhiri anafuata maadili ya kazi wala hakuna matatizo yoyote.

Kwa upande mwingine habari zote kuhusu uhusiano wa mwanafunzi na mhadhiri zinaweza zikawa uzushi tu. Mara nyingi kwenye vyuo, rumours za shemeji shemeji huwa zinaanzishwa na wanafunzi wa kiume. Moja wapo ya sababu huwa ni wivu kwenye marks. Kwa mfano mwanaume akizidiwa marks na msichana, lazima atasingizia tu kuwa yule msichana kagawa mwili. Ila ikitokea mvulana ameongoza mtihani kwenye somo linalofundishwa na mwalimu wa kike, hamna kinachosemwa. Na tatizo linakua zaidi iwapo msichana ni mrembo au hajatulia kitabia au amewatolea nje wanafunzi wa kiume na wakati huo huo anafaulu mtihani. Lazima mhadhiri atafikiriwa kuwa amepewa uroda. Lakini si lazima iwe kweli.

Thanks Nanren you have said it all!
 
Mimi sioni tatizo kama wawili wamekubaliana kuwa na mahusiano yasiyo vunja sheria. Labda niulize, je, ni kosa kwa mhadhiri kuoana na mwanafunzi wa chuo kikuu?? kama siyo kosa basi hapo hakuna tatizo ila tatizo litakuja kama mhadhiri atavujisha mitihani kwa ajiri ya mahusiano ya mapenzi.
 
Salaam wana JF!

Sote tunakifahamu chuo chetu kikuu cha Dodoma. Ni chuo ambacho kumekua na vituko vingi vikiripotiwa toka pale. Mfano,wanafunzi kufundishwa na wahadhiri wenye shahada moja! Kuitwa chuo cha kata kutokana na kua na uhaba wa wahadhiri wenye sifa na vigezo! Makamu msaidizi wa mkuu wa chuo kujiita kondoo mweusi,mara kuku anayeatamia! Kuitwa chuo cha chama (CCM). Chuo kutoa shahada ya uzamivu kwa mkwere wakati chuo hakijawahi hata kutoa mwanafunzi 1 wa shahada hiyo n.k.

Ila hiki kituko cha wanafunzi kuwaita baadhi ya wahadhiri shemeji,mimi kimeniacha hoi.

Kutokana na chuo kua na wahadhiri wengi vijana,kumetokea tabia ya wahadhiri hao kujisevia wanafunzi wa kike,kiasi kwamba hadi wanafunzi wenzao wanafahamu tabia hizo na mwishowe kuamua kuwaita wahadhiri hao wanaotembea na wanafunzi wenzao wa kike,mashemeji!

Hakika UDOM kuna vijambo na vituko!

Fanya utafiti kwanza kabla ya kwenda hewani, mambo haya mara nyingi ni wivu wa anafunzi wa kiume.
 
Hii inanikumbusha Binti Mmoja anaejiheshimu wakati anafanya raundi za internship pale Muhimbili, hao madaktari bingwa karibu katika kila raundi walikuwa wakimsumbuwa kutaka ngono na kumwambia "hafaulu" mpaka wamle, ilibidi afike mpaka kwa waziri Meghji (wakati huo), kwani wakuu wa chuo alipowapelekea malalamiko ya kudhalilishwa na kutishwa walimbeza. Meghji akalivalia njuga hilo suala akatia timu mpaka Muhimbili akawaita wakuu na madaktari husika kwa majina akakaa na kuongea nao, haijulikani walicho-ongea, lakini baada ya hicho kikao akasalimika na akawa anaheshimiwa ingawa alibezwa sana lakini. Alimaliza internship ki usalama.

Nimeongea hayo kuonesha jinsi ngono na udhalilishwaji wa wanafunzi ulivyotapakaa vyuoni, na si vyuoni tu, hata makazini.

Hapa utaona wanawake wenyewe ndio huwa dhaifu na wengine huendekeza na kuona kuwa hiyo ndio njia ya mkato ya kuuwa ndege watatu kwa jiwe moja, 1) mitihani atafaulu 2) michuzi atapata 3) raha (kama si karaha) za ngono atapata.

Wenye msimamo kama huyo binti nilie muhadithia hapo juu, huwa si rahisi kuwarubuni.
 
kati ya wanaoitwa shemeji kikwete hayumo kweli?.....maana ni mzee wa totoz kishenzi ndiyo maana ZE UTAMU ILIFUNGIWA
 
Back
Top Bottom