Ubumuntu
JF-Expert Member
- Oct 21, 2010
- 14,316
- 10,782
Salaam wana JF!
Sote tunakifahamu chuo chetu kikuu cha Dodoma. Ni chuo ambacho kumekua na vituko vingi vikiripotiwa toka pale. Mfano,wanafunzi kufundishwa na wahadhiri wenye shahada moja! Kuitwa chuo cha kata kutokana na kua na uhaba wa wahadhiri wenye sifa na vigezo! Makamu msaidizi wa mkuu wa chuo kujiita kondoo mweusi,mara kuku anayeatamia! Kuitwa chuo cha chama (CCM). Chuo kutoa shahada ya uzamivu kwa mkwere wakati chuo hakijawahi hata kutoa mwanafunzi 1 wa shahada hiyo n.k.
Ila hiki kituko cha wanafunzi kuwaita baadhi ya wahadhiri shemeji,mimi kimeniacha hoi.
Kutokana na chuo kua na wahadhiri wengi vijana,kumetokea tabia ya wahadhiri hao kujisevia wanafunzi wa kike,kiasi kwamba hadi wanafunzi wenzao wanafahamu tabia hizo na mwishowe kuamua kuwaita wahadhiri hao wanaotembea na wanafunzi wenzao wa kike,mashemeji!
Hakika UDOM kuna vijambo na vituko!
Sote tunakifahamu chuo chetu kikuu cha Dodoma. Ni chuo ambacho kumekua na vituko vingi vikiripotiwa toka pale. Mfano,wanafunzi kufundishwa na wahadhiri wenye shahada moja! Kuitwa chuo cha kata kutokana na kua na uhaba wa wahadhiri wenye sifa na vigezo! Makamu msaidizi wa mkuu wa chuo kujiita kondoo mweusi,mara kuku anayeatamia! Kuitwa chuo cha chama (CCM). Chuo kutoa shahada ya uzamivu kwa mkwere wakati chuo hakijawahi hata kutoa mwanafunzi 1 wa shahada hiyo n.k.
Ila hiki kituko cha wanafunzi kuwaita baadhi ya wahadhiri shemeji,mimi kimeniacha hoi.
Kutokana na chuo kua na wahadhiri wengi vijana,kumetokea tabia ya wahadhiri hao kujisevia wanafunzi wa kike,kiasi kwamba hadi wanafunzi wenzao wanafahamu tabia hizo na mwishowe kuamua kuwaita wahadhiri hao wanaotembea na wanafunzi wenzao wa kike,mashemeji!
Hakika UDOM kuna vijambo na vituko!