LOTH HEMA
JF-Expert Member
- Dec 6, 2015
- 26,826
- 41,338
Wajuba kwenye mahusiano ya kindoa huko ukweni kuna vituko vingi sana. Hebu tuangalie vichache. Unakuta familia ina mabinti kama watatu, wanne, watano na kuendelea wameolewa na wanaume wenye vipato na hadhi tofauti.
Mkwe mwenye kipato kidogo huishia kudharauliwa na kutumwa kazi za hovyo hovyo na hapewi heshima kama watozi wenzake. Mara akapasue kuni, mara akalime, kuchunga na udhalilishaji mwingine ukweni.
Lakini wengine hawatumwi kipuuzwi wanapewa heshima kubwa, wanapikiwa misosi mizuri ya heshima, wanachinjiwa kuku, mbuzi, wanakunywa mchuzi, kulamba asali na maziwa lakini kapuku ugali dona bamia imetoka hiyo?
Mimi ushenzi huo sikubali na hawataniona ukweni ili heshima iwepo. Nyumbani nako unaoa lakini mke wako naye anatumikishwa kazi za hovyo hovyo lakini wake za ndugu zako wanaheshimiwa kwa kuwa waume zao wana ajira safi fedha ipo. Mke wangu akishushiwa heshima nitakuwa mkali kutaka heshima sawa kwa wake zetu. Huwa sipendi ujinga ukweni na nyumbani, tuheshimiane
Mkwe mwenye kipato kidogo huishia kudharauliwa na kutumwa kazi za hovyo hovyo na hapewi heshima kama watozi wenzake. Mara akapasue kuni, mara akalime, kuchunga na udhalilishaji mwingine ukweni.
Lakini wengine hawatumwi kipuuzwi wanapewa heshima kubwa, wanapikiwa misosi mizuri ya heshima, wanachinjiwa kuku, mbuzi, wanakunywa mchuzi, kulamba asali na maziwa lakini kapuku ugali dona bamia imetoka hiyo?
Mimi ushenzi huo sikubali na hawataniona ukweni ili heshima iwepo. Nyumbani nako unaoa lakini mke wako naye anatumikishwa kazi za hovyo hovyo lakini wake za ndugu zako wanaheshimiwa kwa kuwa waume zao wana ajira safi fedha ipo. Mke wangu akishushiwa heshima nitakuwa mkali kutaka heshima sawa kwa wake zetu. Huwa sipendi ujinga ukweni na nyumbani, tuheshimiane



