Vituko mitandaoni. Tupia chako

πŸ˜…πŸ˜…
The poor ex must be emotionally immature...

➑️➑️➑️ Na huyo ex ni lazima awe Msukuma jamani kha! Wasukuma tuliwakoseaga nini Watanzania? Tunataniwa mpaka na Wanyaki dah! πŸ˜πŸ˜πŸƒπŸΏβ€β™‚οΈπŸƒπŸΏβ€β™‚οΈπŸƒπŸΏβ€β™‚οΈ
 
App ya zamani ilikuwa nzuri mtu unaweka tu picha mara moja badala ya hizi steps zote.
 
Kufuatia mahojiano na pacha waliokuwa wakisoma Chuo Kikuu Ardhi wakieleza jinsi walivyoweza kufanyiana mtihani, uongozi wa chuo hicho umesema unafanya uchunguzi wa jambo hilo.

Katika mahojiano hayo ya Wasafi FM yaliyofanyika Machi 6 mwaka huu, pacha mmoja alikiri kumfanyia pacha mwenzake mtihani wa marudio (supplementary) wa Hydrolojia kwa kutumia kitambulisho cha mwenzake baada ya kufeli mtihani huo.

β€œTulikuwa chuo sasa unajua chuo tunasoma kozi ambayo kuna masomo ambayo tunaendana kwahiyo sasa kuna somo moja ambalo linaitwa Hydrology tukawa tunaingia class moja lakini bahati mbaya mwenzangu akapata supp mimi nikawa nimetoboa, sasa nikamwambia hapo kwenye supp tulia nitafanya mimi [..] akanipa kitambulisho chake nikamaliza akatoboa supp na hawakuwahi kujua,” mmoja wa pacha alieleza.

Aidha, uongozi wa chuo hicho umesema baada ya kufanya utafiti na kubaini ukweli wa taarifa hizo, umma utajulishwa juu ya matokeo ya uchunguzi huo.
 
Fadhila Thomas Kiria wa USA River, Arusha amepotea katika mazingira ya kutatanisha akiwa mjini Moshi, asubuhi ya tarehe 4/3/2024 na hadi leo hajulikani halipo. Tarehe tajwa hapo juu Fadhila alikua dukani anapofanya kazi, Moshi mjini. Akalalamika kichwa kumuuma, akaacha simu na pochi juu ya meza dukani, akatoka kwenda kununua dawa. Lakini hakurudi mpaka leo. Ameacha mtoto mchanga wa wa miezi 5 anayenyonya.

Juhudi za kumtafuta maeneo mbalimbali ya Moshi na Arusha hazijazaa matunda. Taarifa imetolewa Polisi lakini bado hajaonekana. Ndugu wamemtafuta hospitali zote za Moshi, ikiwa ni pamoja na vyumba vya kuhifadhia maiti (mochwari) lakini hawajampata. Haijulikani kama yu hai au amefariki, au labda alipata tatizo la afya ya akili kutokana na maumivu ya kichwa. Tunaomba yeyote atakayemuona awasiliane na mama yake kwa simu nambari; 0762122114 au dadaye Berha: +255765688085. Asanteni na Mungu awabariki
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…