Vitu vinavyonikera ndani ya ndoa

Vitu vinavyonikera ndani ya ndoa

zandile

Member
Joined
Jul 3, 2014
Posts
22
Reaction score
18
Hivi Ladies kuolewa maana yake ni nini?

Mimi kuna vijambo vinanichosha mpaka imekuwa kero na kuona kama ndoa ni ngumu. Ni takribani mwaka mmoja na nusu sasa mme wangu kazi iliisha yupo nyumbani huku akiangaika kutafuta kazi sehemu zingine .

Hiyo sio big deal mie nafanya kazi thanks God kamshahara kangu kanasaidia kucover matatizo yote ya nyumbani ingawa sio kama tukiwa wawili. Kinachonichosha sana ni ratiba ya mme wangu.

Mimi nina watoto wawili wa kiume mmoja 5 years na mwingine 9 month. Mme hata mtoto akiwa analia eti yeye hawezi kumbembeleza anamwangalia tu ukimuuliza anasema yeye amfanyeje wakati hana maziwa ya kumnyonyosha, mimi hapa usiku silali mtoto anasumbua asubuhi kuamkia kazini, jioni kufika kumwangalia mtoto na kuandaa maakuli ya familia.

Nina binti anaenisaidia nikiwa kazini. Lakini mme anaamka saa nne kitanda hagusi kutandika mpaka nitoke kazini nakikuta hivyo hata net haijatolewa kutandika ndio basi tena pia hata akivua nguo za ndani atarundika hapo nije kufua mie.

Anapiga mswaki na kukaa kwenye kochi kusubiri atengenezewe chai na apelekewe, atabadilisha chanel mpaka lunch atakula atabadilisha Channel zake baadae anawasha gari kwenda kutembea.

Saa mbili au saa tatu atarudi atakula atakamata tena remote mpaka saa sita ataingia kulala na ukali sasa kitu kidogo tu manung'uniko.


Hivi jamani wanaume mkioa kazi yenu huwa inakuwa kutoa matumizi, kula na kulala tu?

Hakuna mnachoweza kusaidia?

Ladies hivi wote mko kwenye hali hii?
 
hmmm kwanza pole...huyo mumeo bana anamatatizo...
Sio wote kwenye hali hiyo..kuna wanaume wengine wako safi mpaka raha,unasaidiwa kufua,kulisha mtoto,yaani kazi zooteee pale msaada unapohitajika/anapoona ni vyema kufanya...lakini kumbuka hiyo inategemea na malezi ya kwao..Mtu ambaye hajawahi kufanyishwa mazoezi ya kazi kwao usitarajie atakuja kufanya baadae.
Ikumbukwe pia mwingine anakuwa anajua kazi ila kufanya/kukusaidia anaona utamdhalau kuonekana mume ----- au kwakuwa hana kazi,kwahiyo hapo anajitutumua aonekane bado yumo..
 
Ulifanyiwa kitchen party wewe...??? Siri za ndani hizo!

Huo ni utashi wa mtu mwenyewe, inawezekana kukosa kazi kunampa mawazo mengi sana na kupelekea stress!! Jaribu kuwa nae close na kwa upendo na utani unaeweza kumtania kuhusu kitanda!! Usitumie maneno makali coz anaweza kuhisi kukosa kwake kazi ndiko kunakufanya umfokee!
 
huyo ana uzembe wa asili au ndo wale mfumo dume umeota mizizi damuni kwao

Nope! Si kila kitu ni mfumo dume, hali aliyonayo ya kukosa kazi inaweza kuchangia kumpa stress. Mtu mwenye stress unaweza ukamchukia kama hujamjua, hujikuta anawaza muda wote na asijue alifanyalo ni kosa!!

Swali ni kwamba, alikuwa hivyo mwanzoni akiwa na kazi?? Tabia halisi ni tofauti na stress ujue, inahitajika njia makini kubaini tatizo lake
 
Nadhani hapo ndo busara zako zahitajika zaidi.....kabla hajawa hana kazi alikuwaje....?.....nahisi amekata tamaa......na kila analopanga anaona haliendi.....so jaribu kuwa nae karibu.....mpe moyo....usianze na wewe kununanuna kwa hayo anayokufanyia.......uvumilivu unahitajika hapo mpaka mambo yake yakikaa vizuri tena.......na pia kama waweza mtafutie mtaji afanye japo biashara kwa sasa......
 
Pole mwaya..... huyo kidume ndivyo alivyo na huwezi kumbadili maana hiyo iko kwenye damu. Lakini shost tabia hizo za uvivu hukuzigundua mkiwa wachumba? wanaume kama hawa huwa hawawezi hata kufuta viatu vyao na kuvipanga sehemu yake.

Na humu JF wapo kibaoooo kutwaaaaa na vilaptop/visim vyao hawajisogezi. Subiri kidogo utawaona tu....

Amani moyoni mwako jipe mwenyewe! Fanya shughuli zako usishughulike naye afanye sawa na asipofanya sawa tu... atabaki mumeo daima. Upo hapo zandile?
 
Last edited by a moderator:
Hapa tukiangalia juu juu tunaweza kutoa ushauri mbovu wa kuharibu ndoa! Nawashauri wadau msichukulie poa poa sana!
:focus:
Kitendo cha kusema hana kazi na mambo yote unafanikisha wewe, huo sio uungwana! Mwenyewe si umesema kama anahangaika kutafuta?

Naamini hayo manung'uniko yako yamerise kwa kasi kubwa baada ya kuona masuala ya misosi unafanikisha wewe! Unataka malipo kana kwamba naye achukue jukumu lako! Naamini akiosha vyombo utafurahia kitu ambacho si kizuri!

Hizo kazi unazonung'unikia hapo ni wajibu wako wa msingi!

Nakubaliana nawe 100% kwamba mapenzi ni kusaidiana! But unahitajika kuwaza zaidi ya hapo! Kitendo cha kufukuzwa/kusimamishwa/kuacha kazi kimeathiri huyo mmeo! Kisaikologia ana adjustment disorder! Unatakiwa kumpa moyo na kumfariji na sio kumnung'unikia tu!

Nna uhakika huyo mme anakupenda sana!

In nature kuna me hawapendi kufanya kazi ulizojitaja especially wanapokutwa na majanga eg: kufukuzwa kazi!

Huenda huyo mmeo anajiuliza hivi: "Kwa kua sina kazi, na kwa vile mkewa wangu ana kazi na anawajibika, jee fact hizo zinifanye nifanye kazi za kike? How if ikiwa ni ubushoke? Kwanini kufukuzwa kazi iwe sababu ya kuondoa amani yangu!
...
Nakushauri kaa naye chini uongee naye kwa upendo, acha kumlalamikia sana! Malalamiko hayajengi yanabomoa tu! Naamini na nitaendelea kuamini kwamba ukifanya hivyo mtaishi kwa amani!
...
Waweza pita na hapa huenda ukajifunza kitu: https://www.jamiiforums.com/mahusiano-mapenzi-urafiki/696522-makundi-manne-ya-binadamu.html

Wish you all the best!
 
%kubwa ya wanaume wako hivyo awe na kazi asiwe na kazi.
hawajishughulishi yani labda uwe unaumwa
mi nlikua naishi mbali mme wangu mi nlikua kazini
yani nkienda kumtembelea nyumba km wenyewe wamehama yani nyumba chafu shuka uliyoitandika ulivyokua unaondoka ukirudi unaikuta hajali
so ndugu yangu vumilia
ukiongea nae asa hv atajihis unamnyasa kwa sababu hana kazi
 
Hapo issue ni kuwa jamaa sasa kawa mzigo maana kama hizo tabia nina uhakika hazijaanza leo lkn ukawa unamvumilia sababu na yy anachangia tena labda zaidi kwenye pato la familia!

Jamaa kachokwa sababu haleti chochote home kuchangia na hii ndiyo zenu madada wengi!Yalinikuta kama haya nilifukuzwa kwa kuitwa "mbweha"usiku wa manane miezi 7 baada ya kupoteza kazi ehehehehe
 
Huyo mme wako anajua wajibu wake,big up kwake.
a

Wajibu gani anaoujua, imagine ushindwe kutandika hata kitanda eti wajibu? ukiuliza umeoa, hata kama ni stress za kukosa kazi jamani ndio ashindwe hata kumbembeleza mtoto anapolia?? wanaume wengi wana mifumo dume , wanapooa wanadhani wamepata haousegirl na sio msaidizi.Badilikeni wanaume!!!
 
Hii thread imenichekesha san nitachangia baadae, wacha nimuachie lara 1 akamilishe somo kake.
 
Last edited by a moderator:
Umepata hata muda wa kuzungumza nae kweli?! Huu ni muda wa kumfariji na kuonesha upo pamoja nae katika kipindi hiki kigumu,pengine unam-mistreat maana unajiona ushakuwa 'fazahaus'... Zungumza nae kwa upendo,hakuna mwanaume timamu anaekubali kuwa chini ya mwanamke.. Sidhan kama ulikumkuta na kiburi hicho mlipoanza,wakati mwingine kiburi kinajengeka humo humo ndani ya nyumba...
 
Mi nadhani ni tabia ya mtu ambayo haifichiki coz nadhani umemjua toka mwanzo kinachokusumbua ni kuwa anashinda nyumbani unatamani hata kuna siku achukue nguo zote afue! Swali je zamani alikuwa hivo?
 
Hayo mmeyaongea na mumeo au unaumia tu moyoni. Hatua ya kwanza yaweke wazi kwake uone anasema nini. Hatua nyingine inategemea majibu yake!

Last week nilikuwa naosha Vyombo ,akaniita mama F naomba unitengenezee coffee akiwa ameshika remote anaangalia TV

Nikamwambia naosha vyombo my dear ila kila kitu kipo mezani please nisaidie kutengeneza wala hakunyanyua mguu anasubiri nikatengeneze ,na hapo mtoto nimeweka mgongoni wangu alikuwa mgonjwa

Nikatengeneza kikombe chake nikampa akasema asante basi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom